Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ws sura 1 kur. 4-12
  • Tamaa ya Amani na Usalama Ulimwenguni Pote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tamaa ya Amani na Usalama Ulimwenguni Pote
  • Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mwanzo wa Enzi Kuu Yenye Ushindani
  • Njia ya Kufurahia Amani Pamoja na Mungu
  • Mchungaji Juu ya Wengi Zaidi ya “Kundi Dogo”
  • Amani na Usalama wa Kweli Ni Karibu!
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Amani ya Kimungu kwa Wale Wanaofundishwa na Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Acha “Amani Ya Mungu” Ilinde Moyo Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Amani Kutoka kwa Mungu Wakati Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
ws sura 1 kur. 4-12

Sura 1

Tamaa ya Amani na Usalama Ulimwenguni Pote

1, 2. Ni uhitaji gani wa haraka walio nao wanadamu wote, na kwa sababu gani?

AMANI na usalama ndivyo tunavyotaka hapa duniani. Ule uhitaji wa hali kama hiyo inayotamanika haujapata kuwa wenye haraka zaidi kama ulivyo leo. Ndivyo ilivyo si kwetu tu watu mmoja mmoja bali pia kwa jamaa nzima ya kibinadamu kuizunguka dunia.

2 Ndiyo sababu idadi ya watu iliyopo duniani sasa inaishi katika wakati usio na kifani! ‘Inawezaje kuwa hivyo,’ labda unauliza, ‘kwa kuwa tumekwisha songa mbele sana katika kile kipindi chenye kuogopesha sana cha historia yote ya kibinadamu, kile kizazi cha silaha za nyukilia?’

3. (a) Ni nini inayosemekana kuwa ndiyo sababu ya mataifa kuwa na kombora la nyukilia? (b) Akili ya kawaida ingeonyesha nini?

3 Angalau mataifa manane yanaripotiwa kuwa yana uwezo wa kufanyiza kombora la nyukilia. Na inakadiriwa ya kwamba kufikia mwaka wa 2000 mataifa 31 yangekuwa na silaha za nyukilia. Sababu yao ya kuwa na kombora hilo lipitalo makombora yote inasemekana kuwa ni ile ya kujilinda, ni kizuizi kwa mataifa mengine yaliyo na silaha za namna hiyo, ni tisho la kuzuia kulipa kisasi cha nyukilia. Hali ikiwa kama ilivyo katika mambo ya ulimwengu, akili ya kawaida ingeonyesha kwamba inayapasa mataifa yakubali kuishi pamoja kwa kuvumiliana.

4. Ingawa Muumba hakuzuia jitihada za wanadamu za kutafuta usalama, yeye ana kusudi gani kuhusu jambo hilo?

4 Hata hivyo, je! ni amani inayofanyizwa na mwanadamu tunayotaka, pamoja na usalama ambao mwanadamu anaweza kutoa? Ijapokuwa Muumba hajawazuia wanadamu kuleta na kudumisha amani na usalama ulimwenguni pote, yeye ana njia yake mwenyewe kamilifu ya kutosheleza tamaa yetu ya asili kwa ajili ya amani na usalama. Yeye ana wakati wake mwenyewe uliowekwa wa kuwaondolea mbali wale wote wanaoharibu usalama wa wale wanaotaka kumwabudu. Jinsi tunavyoweza kuwa na furaha kujua kwamba wakati wake wa kufanya hilo umekaribia karibu!

5. Mtunga Zaburi aliyeongozwa na Mungu alisema nini kuhusu dunia, nalo ni nini kusudi la Muumba kwa mwanadamu?

5 Baada ya maelfu ya miaka ya historia ya kibinadamu yenye msukosuko, inapasa kutarajiwa kwamba bila shaka kungekuwako tamaa kubwa duniani pote kwa ajili ya amani na usalama. Dunia imekuwa makao ya asili ya mwanadamu tangu ule mwanzo wenyewe wa kuwako kwa wanadamu. Mtunga zaburi aliyeongozwa na Mungu alisema: “Mbingu ni mbingu za [Yehova], bali [dunia] amewapa wanadamu.” (Zaburi 115:16) Tangu ule mwanzo wenyewe, lilikuwa kusudi lenye upendo la Muumba mwanadamu afurahie uzima kwa ukamili katika makao yake ya kidunia aliyopewa na Mungu.

6. Ni kwa njia gani mwanadamu wa kwanza na wazao wake wangeweza kutenda kama Mungu?

6 Kulingana na masimulizi ya Mwanzo 2:7, “Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” Hakuna kiumbe kingine chenye uhai duniani kilichokuwa na namna ya uhai kama wa mwanadamu ama kiwango cha uwezo wa mwanadamu—kuweza kutenda kama Mungu katika kutumia uwezo wa kutawala. Zaidi ya hilo, uwezo huo wa kutawala hakupewa kiumbe binadamu wa kwanza pekee bali pia ungeweza kutumiwa na kufurahiwa na watoto wake.

7. Adamu alimpataje mke, naye alisema nini wakati kiumbe huyo mkamilifu alipoletwa kwake?

7 Kwa sababu hiyo, Muumba alimpa Adamu mke. Mke huyo angekuwa ndiye mama ya wanadamu wote wakaaji wa dunia ambao wangetokea wakati ujao. Ndiyo sababu, alipoletewa kiumbe huyo mkamilifu, mwanamume huyo angeweza kusema: “Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu.” Kwa hiyo yeye akamtamka mwanamke wa jamii ya kibinadamu, ’ish·shahʹ, ambayo ndiyo namna ya kike ya neno la Kiebrania linalotafsiriwa mwanamume, yaani, ’ish.—Mwanzo 2:21-23.

8. Ni maagizo gani ambayo Muumba aliwapa watu hao wawili wa kwanza?

8 Huyo Muumba na Baba wa kimbingu alisema hivi kwa hao watu wawili wa kwanza: “Zaeni mkaongezeke, mkaijaze [dunia], na kuitiisha.” (Mwanzo 1:28) Utaratibu huo ulikuwa jambo jipya kabisa katika historia ya viumbe vyenye akili. Wakaaji wa kiroho wa mbingu zisizoonekana hawakutokezwa kupitia njia hiyo ya kuzaana.

9. Zaburi 8:4, 5 inaelezaje mpango wa kimungu wa mambo?

9 Si ajabu kwamba, wakati wa dunia kuumbwa, ‘nyota za asubuhi ziliimba pamoja, na wana wote wa Mungu walipiga kelele kwa furaha.’ (Ayubu 38:7, NW) Wakati huo, kila kitu kilikuwa chenye amani na upatani katika ulimwengu wote mzima. Katika zaburi ya nane, mtunga zaburi akiwa anapendezwa sana na mpango huo wa mambo wa kimungu, alipaza sauti hivi kwa habari ya mwanadamu: “Pia wewe uliendelea kumfanya mdogo punde kuliko walio mfano wa Mungu, na ndipo ukamvika taji kwa utukufu na fahari.” (Mistari 4, 5, NW) Kulingana na zaburi hii, Mungu aliweka vitu vyote hapa duniani chini ya miguu ya wanadamu.

Mwanzo wa Enzi Kuu Yenye Ushindani

10. (a) Kabla ya mimba kutungwa ya mtoto wa kwanza wa kibinadamu, ni jambo gani lilitukia? (b) Kwa njia hiyo ni nini ingeweza kuanzishwa juu ya jamii ya kibinadamu?

10 Kwa kushangaza, kabla ya mimba kutungwa ya mtoto wa kwanza wa kibinadamu, uasi ulitokea katika tengenezo la Yehova Mungu la ulimwengu mzima. Hali hiyo ingeongoza kwenye kusimamishwa kwa enzi kuu mpya, utawala mpya wa namna ya juu, juu ya wanadamu—ikiwa wanadamu wangetenganishwa na kuwekwa katika hali ya uadui na tengenezo la Yehova la ulimwengu mzima. Enzi kuu ya kupingana na yake ingeweza kuanzishwa. Hilo lilihitaji uwongo wa kwanza usemwe, ukimwonyesha Yehova Mungu kuwa mwongo.

11. Kwa kumwonyesha Yehova Mungu kuwa mwongo, huyo mwasi wa kwanza alipata kuwa nini?

11 Kusemwa kwa uwongo huo wa kwanza kulimfanya mwasi huyo wa kwanza juu ya Mungu kuwa mwongo wa kwanza, yule Ibilisi wa kwanza, au mvunja sifa nzuri. Tofauti kabisa na yeye, Yesu Kristo alisema: “Mimi ndimi njia na kweli, na uzima.” (Yohana 14:6) Yesu aliwaambia wapinzani wake wa kidini hivi: “Ninyi ni wa baba yenu ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uwongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo na baba wa huo [uwongo].”—Yohana 8:44.

12. (a) Ibilisi aliwezeshaje ule uwongo wa kwanza usemwe, nayo matokeo yalikuwa nini juu ya Hawa? (b) Matokeo yalikuwa nini wakati Adamu alikula tunda lililokatazwa?

12 Kwa kusema kupitia nyoka katika shamba la Edeni, au paradiso ya furaha, yule Ibilisi alifanya ule uwongo wa kwanza utolewe kwa yule mwanamke wa kwanza. Yeye alidai ya kwamba Muumba wake alikuwa mwongo, kwa njia hiyo akavuruga amani ya akili ya Hawa. Yeye alimfanya mwanamke ajisikie akiwa katika hali ya kukosa usalama katika hali yake ya kuwaziwa ya kutojua, kwa hiyo akala kutokana na tunda lililokatazwa. Mwanamke alimshinda nguvu mumeye, Adamu, ili ale kutokana na tunda lililokatazwa na hivyo ajiunge naye katika uasi wake juu ya Yehova Mungu. (Mwanzo 3:1-6) Mume na mke hao wasiotii walipoteza amani yao pamoja na Mungu na walifukuzwa kutoka paradiso ya furaha wakaishi nje katika hali ya kutokuwa na usalama. Warumi 5:12 huieleza hali hii ya mambo yenye kusikitisha, ikisema: “Kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.”

13. Ni uchaguzi gani ambao lazima kila mmoja wetu afanye leo?

13 Hali ilivyo katika siku zetu inatuhitaji tufanye uchaguzi halisi. Ni uchaguzi kati ya ile enzi kuu yenye ushindani ya Shetani Ibilisi, “yule mungu wa huu mfumo wa mambo,” na ile enzi kuu ya Yehova, yeye Aliye Juu Zaidi na Mungu Mwenye Nguvu Zote wa ulimwengu wote.—2 Wakorintho 4:4, NW; Zaburi 83:18.

Njia ya Kufurahia Amani Pamoja na Mungu

14. Ni amani na usalama gani tunaoweza kuanza kufurahia hata sasa?

14 Kwa kujiletea madhara yenye maumivu makali wao wenyewe, wanadamu wengi hawatamani kukubali au kuamini mpango wa Mungu Mwenye Nguvu Zote kwa ajili ya waabudu wake wa kuwaletea amani ya kiasi na usalama hata katika hali hii ya mambo ya wanadamu yenye kuhuzunisha. Hata hivyo, “Yehova ndiye Mungu atoaye amani,” na ni pendeleo letu lenye baraka sasa kuingia katika amani na usalama ambao hautashindwa kamwe. (Warumi 16:20, NW; Wafilipi 4:6, 7, 9) Hiyo ni amani na usalama ambayo yeye anatoa hata sasa kwa kundi la watumishi wake wa kidunia, tengenezo lake lionekanalo, katika kutimiza ahadi zake ambazo daima zinategemeka. Hiyo ni amani na usalama ambayo sisi tunaweza kuifurahia tu kwa kushirikiana na tengenezo lake lionekanalo hapa duniani.

15. Je! ni jambo la upumbavu kufikiri kwamba Mungu analo tengenezo, na Yesu Kristo alitambua nini?

15 Kuamini kwamba Mungu hana tengenezo, watu waliofanywa tengenezo, ambao yeye anawatambua kipekee, kungekuwa ni kupingana na mafundisho yaliyo wazi ya Maandiko. Yesu Kristo alitambua kwamba Baba yake wa kimbingu alikuwa na tengenezo lionekanalo. Kufikia siku ya Pentekoste ya mwaka 33 W.K., lilikuwa ni tengenezo la Kiyahudi lililokuwa katika uhusiano wa agano pamoja na Yehova Mungu chini ya Torati ya Musa.—Luka 16:16.

16. (a) Musa alikuwa mpatanishi kati ya nani? (b) Yule Musa Mkubwa Zaidi, Yesu Kristo, ni Mpatanishi kati ya nani?

16 Kama vile taifa la Israeli wa kale lilivyokuwa katika uhusiano wa agano pamoja na Yehova Mungu kupitia mpatanishi Musa, ndivyo na lile taifa la Israeli wa kiroho, “Israeli wa Mungu,” lilivyo na uhusiano wa agano kupitia mpatanishi. (Wagalatia 6:16) Ni kama vile mtume Paulo alivyomwandikia Mkristo mfanyi kazi mwenzake: “Kwa sababu Mungu ni mmoja na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, mwanadamu Kristo Yesu.” (1 Timotheo 2:5) Je! Musa alikuwa mpatanishi kati ya Yehova Mungu na wanadamu kwa ujumla? Hapana, yeye alikuwa mpatanishi kati ya Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo na lile taifa la wazao wao wa kimwili. Vivyo hivyo, yule Musa Mkubwa Zaidi, Yesu Kristo, si Mpatanishi kati ya Yehova Mungu na wanadamu wote. Yeye ni Mpatanishi kati ya Baba yake wa kimbingu, Yehova Mungu, na lile taifa la Israeli wa kiroho, ambalo lina washiriki wenye kikomo 144,000. Hilo taifa la kiroho ni kama kundi dogo la watu wa Yehova wenye mfano wa kondoo.—Warumi 9:6; Ufunuo 7:4.

Mchungaji Juu ya Wengi Zaidi ya “Kundi Dogo”

17. (a) Yehova Mungu amemweka Yesu Kristo kuwa nini? (b) Yesu alisema nini kwa wale watakaorithi Ufalme wa kimbingu?

17 Katika Zaburi 23:1, Mfalme Daudi wa Israeli wa kale aliongozwa na Mungu kusema: “[Yehova] ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.” Yehova, Mchungaji Mkuu Zaidi, amemweka Yesu Kristo kuwa “Mchungaji Mwema.” (Yohana 10:11) Kwenye Luka 12:32, Yesu aliwaambia wale ambao kwao angekuwa Mchungaji Mwema hivi: “Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.”

18. (a) Ni nani leo wanaolingana na Wanethini na wana wa watumishi wa Sulemani wasio Waisraeli? (b) Wanashirikiana na nani karibu karibu?

18 Katika nyakati za kale, kulikuwako na watu wasiokuwa Wayahudi, kama vile Wanethini na wana wa watumwa wa Sulemani wasio Waisraeli ambao walishirikiana na taifa la Israeli. (Ezra 2:43-58; 8:17-20) Vivyo hivyo leo, kuna wanaume na wanawake ambao wamejiweka wakfu kabisa kwa Mungu kupitia Yesu Kristo lakini wao si Waisraeli wa kiroho. Hata hivyo, wao wanashirikiana na mabaki ya Waisraeli wa kiroho kwa sababu wamejiweka wakfu wao wenyewe kwa Yehova Mungu kupitia Yesu Kristo “ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi unaolingana kwa ajili ya wote.” (1 Timotheo 2:6, NW) Leo, hao wanazidi sana ile hesabu 144,000 ya Waisraeli wa kiroho, ambao wataurithi ule Ufalme wa kimbingu.

19. Yesu Kristo alisema nini kuonyesha kwamba yeye angekuwa Mchungaji juu ya zaidi ya lile “kundi dogo”?

19 Hivyo katika wakati wa Mungu unaofaa, Yesu Kristo angewekwa kuwa Mchungaji juu ya kundi kubwa zaidi la watu wenye mfano wa kondoo ambao wangeingia kwenye urithi wa kidunia kupitia kwake. Hao ndio aliokuwa akifikiria wakati aliposema: “Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na [Mchungaji] mmoja.” Akiwafikiria hao “kondoo wengine” mtume Yohana aliandika hivi pia kuhusu Yesu: “Naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.”—Yohana 10:16; 1 Yohana 2:2.

20. (a) Hesabu ya wale wa “kondoo wengine” inalinganaje na ile ya wale wanaobaki wa lile “kundi dogo”? (b) Uangalizi wa uchungaji wa yule Mchungaji Mwema unamaanisha nini kwao wote?

20 Leo, kuna washiriki karibu 9,000 wanaodai kuwa mabaki ya lile “kundi dogo” la kondoo wa kiroho. Kwa upande mwingine, kuna mamilioni ya waliojiweka wakfu wanaoshirikiana na mabaki ya wapakwa mafuta katika kufuata hatua za yule Mchungaji Mwema, Yesu Kristo. Wao wanapatikana katika nchi zaidi ya 200 kuizunguka dunia. Ule uangalizi wa uchungaji wa yule Mchungaji Mwema unamaanisha nini kwao? Una maana ya kwamba, wao wanafurahia amani na usalama! Kama hawangekuwa na amani miongoni mwao, hakungeweza kuwa na umoja unaotoka moyoni pamoja na ushirikiano usioweza kuvunjwa kati yao. Kama hawangekuwa na hali ya kuhangaikiana kwa upendo kwa habari ya faida zao za kiroho, hawangekuwa na usalama kama ule wanaofurahia. Hivyo tamaa yao ya amani na usalama wa duniani pote imeanza kutoshelezwa hata sasa.

[Picha katika ukurasa wa 4, 5]

Muumba ana njia yake mwenyewe kamilifu ya kutosheleza tamaa ya wanadamu kwa ajili ya amani na usalama

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki