Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ws sura 10 kur. 82-89
  • Alichoapa Mungu Kutendea Wanadamu—Sasa ni Karibu!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Alichoapa Mungu Kutendea Wanadamu—Sasa ni Karibu!
  • Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Aingia na Kiapo
  • Ni Kwa Kadiri Gani?
  • Waokokaji Kutoka Mataifa Yote
    Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • Mtii Mungu Ili Ufaidike Kutokana Na Ahadi Zake Zenye Kiapo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Agano la Mungu Pamoja na “Rafiki” Yake Tayari Lafaidi Mamilioni
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • “Fanyeni Mioyo Yenu Kuwa Imara”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
ws sura 10 kur. 82-89

Sura 10

Alichoapa Mungu Kutendea Wanadamu—Sasa ni Karibu!

1, 2. (a) Ni katika maana gani Mungu anaapa, na kwa sababu gani? (b) Mungu anasema nini kwenye Isaya 45:23? (c) Ni semi gani za nabii Isaya tunazoweza kukubaliana nazo?

JE! MUNGU anaapa? Ndiyo, Mungu anaapa, lakini yeye hatumii maneno mabaya, akifoka kwa hasira na kupoteza kujiweza. Sikuzote yeye anaapa ili kutia nguvu yale ambayo ametangaza kuwa kusudi lake. Kunawapa uhakika zaidi wale watakaohusika. Hivyo, wanadamu wote watafanya vema kusikiliza maneno yake kwenye Isaya 45:23: “Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.”

2 Leo, miaka zaidi ya 2,700 baada ya unabii huo, je! sisi tunasadikishwa kwamba usemi wa nabii huyo kwenye Isaya 45:24 ni wa kweli: “Kwa [Yehova], peke yake, iko haki na nguvu; naam, watu watamwendea yeye, na wote waliomkasirikia watatahayarika”? Ikiwa ndivyo, basi tunaweza pia kukubaliana na maneno ya Isaya yanayofuata katika mstari wa 25: “Katika [Yehova] wazao wote wa Israeli watapewa haki, na kutukuka.”

3, 4. (a) Ni kwa sababu gani unabii wa Isaya 45:25 haupasi kutufanya tufikirie ile Jamhuri ya Israeli? (b) Je! Kumekuwako kushindwa katika utimizo wa Isaya 45:23-25, na kwa sababu gani unajibu hivyo?

3 Tunaposoma Isaya 45:25, je! tuifikirie Jamhuri ya Israeli? Hapana! Waisraeli hao hawamhesabii ushindi wao Mungu wa Maandiko ya Kiebrania matakatifu yao. Kwa sababu ya heshima yenye makosa hata wanakataa kutamka jina lake.

4 Kwa kusema hivyo, je! tunatoa hoja kwamba unabii wa Isaya 45:23-25 umekosa kutimizwa kufikia mwaka huu? Hapana! Hapajakosa utimizo wa unabii huo katika wakati wa Yehova uliowekwa. Kwake, kushindwa kwa unabii wake ni jambo lisilowezekana! Si kwamba tu neno lake lenyewe ni lenye kutumainika na kutegemeka bali ndivyo ilivyo hata zaidi wakati Yehova anapoapa juu yalo, akiongeza kiapo chake, kuthibitisha mambo.

Mungu Aingia na Kiapo

5. Maneno ya Waebrania 6:13-18 yanaelezaje juu ya Mungu akiingia na kiapo katika ile ahadi kwa Abrahamu?

5 Kwa habari hii, tunasoma kwenye Waebrania 6:13-18 hivi: “Kwa maana Mungu, alipompa [Abrahamu] ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake, akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza. Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi. Maana wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuliko wao; na kwao ukomo wa mashindano yote ya maneno ni kiapo, kwa kuyathibitisha. Katika neno hilo, Mungu akitaka kuwaonyesha zaidi sana wairithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati; ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uwongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu.”

6. (a) Kulikuwako msukumo gani kwa Mungu kuapa kwa nafsi yake mwenyewe kwa habari ya ile ahadi yake kwa Abrahamu? (b) Yehova angeweza kumtumiaje “rafiki” yake?

6 Kwa ujumla, kunakuwa na msukumo wenye nguvu wa kuapa, wa kutoa kiapo. Sana sana ndivyo ilivyo wakati Mungu mwenyewe ndiye anayeapa kwa kupenda, kwa kujitolea. Msukumo huo unatolewa katika habari hii wakati Yehova anaporipotiwa akiapa, ndiyo, akiapa kwa nafsi yake mwenyewe. Ile ahadi iliyofungwa kwa kiapo ambayo Yehova alifanya kwa Abrahamu, rafiki yake, inahusu sisi sote leo. Yehova alithamini wakati Abrahamu alipotenda kupatana na mwaliko wa kimungu akaacha nchi ya kwao kwenda kwenye nchi ambayo Yehova angewapa wazao wa Abrahamu iwe mali yao. Kwa usalama Yehova angeweza kufanya jina la huyu “rafiki” yake kuwa kubwa na kumtumia kwa ajili ya kuwabariki wengine. Yehova angeweza kwa uzuri kumwambia hivi: “Na mimi nitabariki wale wanaokubariki wewe, na yeye anayeita ovu lishuke juu yako mimi nitalaani, na jamaa zote za ardhi kwa hakika zitajibariki zenyewe kupitia wewe.”—Mwanzo 12:3, NW; Isaya 41:8.

7. (a) Ni kwa mwujiza gani Mungu alimpendelea Abrahamu wakati mke wake alipokuwa na umri wa miaka 90? (b) Abrahamu alionyeshaje imani na utii wake kwa njia ya pekee?

7 Sara mke wa Abrahamu alipokuwa na umri wa miaka 90, akiwa amepita sana umri wa kuzaa watoto, kwa mwujiza Mungu alimpa pendeleo la kumzalia Abrahamu mwana wao mpendwa, Isaka, katika kuendeleza ahadi yake ya ajabu kwa Abrahamu. Abrahamu alijithibitisha kuwa tayari na mwenye nia ya kutoa hata mwana huyu wa bei kubwa sana awe dhabihu ya kibinadamu katika kutii amri ya Mungu wake, Yehova. Wonyesho huu wa pekee wa imani na utii ulimwendesha sana Yehova hivi kwamba alimwambia “rafiki” yake Abrahamu, hivi:

8, 9. (a) Yehova aliitikiaje kwa wonyesho huo wa imani na utii wa Abrahamu? (b) Mungu alijiweka mwenyewe kuwa na daraka kwa nani?

8 “‘Kwa mimi mwenyewe naapa,’ ndio usemi wa Yehova, ‘kwamba kwa sababu ya uhakika wa kwamba umefanya jambo hili na wewe hukuzuia mwana wako, yule wako mmoja tu, bila shaka mimi nitabariki wewe na bila shaka mimi nitazidisha mbegu yako kama nyota za zile mbingu na kama chembe za mchanga ulio juu ya ufuo wa bahari; na mbegu yako itachukua milki ya lango la adui zake. Na kupitia mbegu yako wewe mataifa yote ya dunia kwa hakika yatajibariki yenyewe kwa sababu ya uhakika wa kwamba wewe umesikiliza sauti yangu mimi.’”—Mwanzo 22:15-18, NW.

9 Hapa ndipo mahali pa kwanza katika Biblia ambapo Yehova anaripotiwa kuwa akiapa. Kwa sababu hangeweza kuapa kwa mwingine aliye mkuu kuliko yeye, yeye aliapa kwa nafsi yake mwenyewe, akijifunga mwenyewe kwa kiapo. Kwa njia hiyo alijifanya mwenyewe kuwa na daraka kwake yeye mwenyewe wala si kwa mwingine. Ni lazima iwe kwa sifa yake mwenyewe kwamba anatimiza tangazo lake mwenyewe la kusudi.

Ni Kwa Kadiri Gani?

10. Mungu alifanya agano lake na Abrahamu muda mrefu kadiri gani uliopita, na kwa hiyo ni ulizo gani linalotokea?

10 Abrahamu aliingia nchi ya ahadi ya Kanaani karibu miaka 4,000 iliyopita. Kwa hiyo kufikia sasa, ni kwa kadiri gani agano lililofanywa 1943 K.W.K. limetimizwa?

11. (a) Ni jambo gani linaloonyeshwa na Jamhuri ya Israeli kuwa mwanachama wa UM, na kukiwa na matokeo gani? (b) Je! Wale wazao wa asili wa Abrahamu wanatimiza matakwa ya kuwa ndio ule “uzao” ulioahidiwa?

11 Leo, kuna ile Jamhuri ya Israeli katika Mashariki ya Kati. Kwa faida yayo yenyewe, yenyewe ni mwanachama wa Umoja wa Mataifa. Huo UM unaonyesha kukataliwa kwa ufalme wa Yehova Mungu kupitia kwa ule “uzao” ulioahidiwa wa Abrahamu na hivyo utaharibiwa katika “ile vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi,” Har–Magedoni. Kila mwanachama wa UM huo, kutia ndani Jamhuri ya Israeli, atafutiliwa mbali asiwepo. Kwa kusikitisha, wazao wa asili, wa kimwili wa Abrahamu, hawatimizi matakwa ya kuwa ndio “uzao” wa Kimasihi ulioahidiwa ambao kupitia huo Yehova Mungu atawabariki wanadamu wote.—Ufunuo 16:14-16.

12, 13. (a) Tofauti na babu yake Daudi, kwa sababu gani “Mwana-Mfalme wa Amani” hatatawala akiwa peke yake? (b) Je! Ilikuwa lazima Wakristo waliopakwa mafuta wangojee mpaka kusimamishwa kwa Ufalme 1914 ndipo wapokee ile baraka iliyoahidiwa, na twajuaje?

12 Kwa wazi kabisa ili kila mtu aweze kuona, Masihi aliyeahidiwa hatawali katika Yerusalemu wa kidunia huko Mashariki ya Kati, ili kutimiza agano la Kiabrahamu. Tofauti na babu yake wa kale Daudi, Masihi na “Mwana-Mfalme wa Amani” hatatawala akiwa peke yake. Aliahidi kuwashirikisha pamoja naye katika utawala wake wale mitume waaminifu 12 pamoja na wanafunzi wengine waliozaliwa kwa roho, wenye hesabu 144,000. (Ufunuo 7:1-8; 14:1-4) Kungali na mabaki ya wanafunzi hao hapa duniani. Wamefanyiwa jambo gani katika kutimiza lile agano la Kiabrahamu ambalo juu yalo Mungu aliapa? Mmoja mwenye kutokeza sana aliyetazamiwa kuwa mshiriki wa ufalme huo, mtume Paulo, aliandika kwenye Wagalatia 3:8 hivi: “Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri [Abrahamu] habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa.”

13 Wakristo waliochaguliwa kutoka miongoni mwa mataifa hawakulazimika kungojea mpaka baada ya kusimamishwa kwa Ufalme 1914 ndipo wapokee baraka iliyoahidiwa, kwa maana mtume Paulo aliendelea kusema hivi: “Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na [Abrahamu] aliyekuwa mwenye imani.” (Wagalatia 3:9) Paulo alikuwa Mkristo na alikuwa akibarikiwa, na ndivyo na Wakristo wengine wote waliozaliwa kwa roho wa siku zake.a Vivyo hivyo leo, mabaki, ambao ndio Wakristo waliozaliwa kwa roho wanaoshikamana na imani katika Masihi akiwa ndiye “uzao” mkuu wa Abrahamu kwa ajili ya kubariki wanadamu wote, wanapata baraka iliyoahidiwa.

14. (a) Wakristo waliopakwa mafuta wamebarikiwaje kipekee kulingana na agano la Kiabrahamu? (b) Hilo limemthibitishaje Yehova?

14 Kwa kujiweka wakfu wenyewe kwa Yehova na kuonyesha wakfu huo kwa ubatizo wa maji na kisha kuzaliwa kwa roho ya Mungu kuingia kwenye hali ya kiroho, Wakristo hao wamekuwa wana wa kiroho wa Abrahamu Mkubwa Zaidi, Yehova Mungu. Vilevile wamekuwa warithi washirika pamoja na Yesu Kristo, Isaka Mkubwa Zaidi. (Warumi 8:17) Wao wanabarikiwa kweli kweli kipekee kulingana na lile agano la Kiabrahamu. Yehova amekuwa akitimiza alichoapa kufanya, hivyo akijithibitisha mwenyewe kuwa msema-kweli, Yeye awezaye kutimiza kikamilifu alichoapa kwa uzito kufanya katika jina lake mwenyewe.

15. Mtume Paulo anasema kwamba kila mshiriki wa mabaki ya Wakristo waliozaliwa kwa roho ni nini?

15 Kila mshiriki wa mabaki ya Wakristo waliozaliwa kwa roho ni Myahudi katika maana ya kiroho. Ni kama alivyosema mtume Paulo: “Maana yeye si Myahudi aliye Myahudi kwa nje tu, wala tohara siyo ile ya nje tu katika mwili; bali yeye ni Myahudi aliye Myahudi kwa ndani; na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko.”—Warumi 2:28, 29.

16. Wayahudi wa kiroho wanakuwa jamii gani iliyotabiriwa kwenye Zekaria 8:23?

16 Katika huu “umalizio wa mfumo wa mambo,” Wakristo hao waliozaliwa kwa roho, ambao ni Wayahudi kwa ndani wakiwa na tohara ya mioyo yao, ndio wanakuwa jamii ya Myahudi iliyotabiriwa kwenye Zekaria 8:23, ambapo pameandikwa hivi: “[Yehova] wa majeshi asema hivi, Siku hizo watu [wanaume] kumi, wa lugha zote za mataifa, wataushika upindo wa nguo yake yeye aliye Myahudi; naam, wataushika wakisema, Tutakwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu yu pamoja nanyi.”

17. (a) Ni nani wanaowakilishwa na wale “watu [wanaume] kumi” wanaotaka kwenda kumwabudu Yehova pamoja na mabaki ya kisasa ya Wayahudi wa kiroho? (b) Kwa kushirikiana na Wayahudi wa kiroho katika ibada ya Yehova, washiriki wa “kondoo wengine” wanafurahia nini sasa?

17 “Watu” ambao hao “watu [wanaume] kumi” wanataka kwenda nao kwenye ibada ya Yehova Mungu ndio mabaki ya leo ya Wayahudi hao wa kiroho, ile jamii ambayo ndiyo yule “mtumwa mwaminifu mwenye akili” wa Mathayo 24:45-47. Kwa kuwa nambari hii 10 inawakilisha ukamilifu wa namna ya kidunia, wale “watu [wanaume] kumi, wa lugha zote za mataifa” wangewakilisha wale kondoo wote wa mfano waliotabiriwa kwenye Mathayo 25:32-46. Hao ni wa ile jamii ya “kondoo wengine” ambao Yesu alisema angewaleta kwenye ushirika pamoja na mabaki yenye mfano wa kondoo wawe pamoja nao “kundi moja” katika uangalizi wa yule “mchungaji mmoja,” yeye mwenyewe. (Yohana 10:16) Kwa njia hiyo wanapata mwonjo wa kimbele wa baraka za agano la Kiabrahamu kupitia “uzao” wa yule Abrahamu Mkubwa Zaidi, Yehova Mungu. Kwa hakika, basi, alichoapa Mungu kuwatendea wanadamu wote ni karibu!

[Maelezo ya Chini]

a Yakitaja jina “Wakristo,” maneno ya maelezo ya chini ya Reference Bible kwenye Matendo 11:26 yanasema hivi: “Hebrew [Kiebrania], Meshi·chi·yimʹ, ‘Messianists’ [‘Wanamesia’].”

[Picha katika ukurasa wa 89]

Biblia ilitabiri kwamba watu kutoka mataifa yote wangekuja kushirikiana na Israeli wa kiroho

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki