Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • T-15 kur. 2-5
  • Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani
  • Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uzima Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu
  • Jinsi Jambo Hilo Linavyowezekana Kwako Wewe
  • Ishi Milele Juu ya Dunia-paradiso
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Baada ya Har-Magedoni, Dunia-Paradiso
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Kutabiri Wakati Wetu Ujao
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Kuishi Milele Si Ndoto Tu
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani
T-15 kur. 2-5

Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani

Wakati unapotazama mandhari iliyo juu ya trakti hii, wewe unakuwa na hisia za namna gani? Je! moyo wako hautamani sana amani, furaha, na ufanisi unaoonekana hapo? Hakika unafanya hivyo. Lakini je! hiyo ni ndoto tu, au wazo la msisimuko tu, kuamini kwamba hali hizo zitakuja kuwako duniani?

Watu walio wengi labda wanafikiri hivyo. Hali halisi zilizopo leo ni vita, uhalifu, njaa, magonjwa, uzee—kutaja hali chache tu. Hata hivyo kuna sababu kwa tumaini. Ikitazama kwenye wakati ujao, Biblia inaeleza juu ya “mbingu mpya na dunia mpya ambazo sisi tunangojea kulingana na ahadi yake [Mungu], na katika hizo uadilifu utakaa.”—2 Petro 3:13, NW; Isaya 65:17.

“Mbingu mpya” hizo na “dunia mpya,” kulingana na Biblia, si mbingu mpya za vitu vyenye kuonekana wala si dunia mpya halisi. Dunia na mbingu za kimwili zilifanywa zikiwa kamilifu, na Biblia inaonyesha kwamba zitabaki milele. (Zaburi 89:36, 37; 104:5) “Dunia mpya” itakuwa jamii ya watu wenye uadilifu wakiishi duniani, na “mbingu mpya” zitakuwa ufalme mkamilifu wa kimbingu, au serikali, itakayotawala juu ya jamii hiyo ya watu wa kidunia. Lakini je! inafaa kikweli kuamini kwamba inawezekana kuwe na “dunia mpya,” au ulimwengu mpya mtukufu?

Basi ufikirie uhakika wa kwamba hali bora kabisa za namna hiyo zilikuwa sehemu ya kusudi la kwanza la Mungu kwa dunia hii. Yeye aliweka watu wawili wa kwanza katika Paradiso ya Edeni ya kidunia na kuwapa mgawo mzuri sana: “Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze [dunia, NW], na kuitiisha.” (Mwanzo 1:28) Ndiyo, kusudi la Mungu lilikuwa kwamba wao wawe na watoto na hatimaye waieneze Paradiso yao juu ya dunia yote. Ingawa wao baadaye walichagua kutokumtii Mungu, na hivyo wakathibitika kuwa wasiofaa kuishi milele, kusudi la kwanza la Mungu halikubadilika. Na ni lazima litimizwe katika ulimwengu mpya!—Isaya 55:11.

Kwa kweli, wakati wewe unaposali ile Sala ya Bwana, au Baba Yetu, ukiomba Ufalme wa Mungu uje, unakuwa ukisali ili serikali yake ya kimbingu iondoe kabisa uovu duniani na kutawala juu ya ulimwengu mpya huo. (Mathayo 6:9, 10) Na sisi tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu atajibu sala hiyo, kwa kuwa Neno lake linaahidi hivi: “Wenye haki watairithi [dunia, NW], nao watakaa humo milele.”—Zaburi 37:29.

Uzima Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu

Ufalme wa Mungu utaleta manufaa za kidunia zisizoweza kulinganishwa na kitu cho chote, ufanye kila jambo jema ambalo Mungu alikusudia hapo kwanza ili watu wake wafurahie duniani. Chuki na maoni ya ubaguzi zitakoma, na hatimaye kila mtu duniani atakuwa rafiki ya kweli wa kila mtu mwingineye yote. Katika Biblia, Mungu anaahidi kwamba ‘atakomesha vita hata mwisho wa dunia.’ “Taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.”—Zaburi 46:9; Isaya 2:4.

Dunia nzima italetwa hatimaye kwenye hali ya paradiso iliyo kama bustani. Biblia inasema: “Nyika na mahali palipo ukiwa patafurahi; jangwa litashangilia na kuchanua maua kama waridi. Maana katika nyika maji yatabubujika; na vijito jangwani. Na mchanga ung’aao mfano wa maji utakuwa ziwa la maji, na nchi yenye kiu itakuwa chemchemi za maji.”—Isaya 35:1, 6, 7.

Kutakuwa na kila sababu ya kufurahi katika dunia-Paradiso. Watu hawataona njaa tena kamwe kwa ukosefu wa chakula. “Dunia yenyewe hakika itatoa mazao yayo,” Biblia inasema. (Zaburi 67:6; 72:16, NW) Wote watafurahia matunda ya kazi yao wenyewe, kama vile Muumba wetu anavyoahidi: “Watapanda mizabibu, na kula matunda yake. . . . hawatapanda, akala mtu mwingine.”—Isaya 65:21, 22.

Katika ulimwengu mpya wa Mungu, watu hawatafinyana-finyana tena katika majengo makubwa yenye vijumba vingi wala katika nyumba za vitongoji vya kimaskini, kwa maana Mungu amekusudia hivi: “Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake . . . Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake.” Biblia inaahidi hivi pia: “Hawatajitaabisha kwa kazi bure.” (Isaya 65:21-23) Hivyo watu watakuwa na kazi yenye matokeo mazuri, yenye kuridhisha. Maisha hayatachosha kwa kukosa upendezi.

Baada ya muda, Ufalme wa Mungu hata utarudisha uhusiano wenye amani uliokuwako katika bustani ya Edeni kati ya wanyama, na kati ya wanyama na wanadamu. Biblia inasema: “Mbwa-mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja, mtoto mdogo atawaongoza.”—Isaya 11:6-9; Hosea 2:18.

Ebu wazia, katika dunia-Paradiso magonjwa yote na hali za udhaifu wa kimwili zitaponywa pia! Neno la Mungu linatuhakikishia hivi: “Hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa.” (Isaya 33:24) “[Mungu] atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”—Ufunuo 21:4.

Jinsi Jambo Hilo Linavyowezekana Kwako Wewe

Kwa uhakika moyo wako lazima uvutwe na ahadi hizi za Mungu kuhusu uzima katika ulimwengu mpya wake wa uadilifu. Na ingawa huenda wengine wakafikiri kutimizwa kwa baraka hizo kunazidi uzuri wa kuwa kweli, hazizidi uzuri hata zisitoke kwenye mkono wa Muumba wetu mwenye upendo.—Zaburi 145:16; Mika 4:4.

Bila shaka, kuna matakwa ya kutimizwa ikiwa tutaishi milele katika Paradiso inayokuja duniani. Yesu alionyesha takwa moja kuu, akisema hivi katika sala kwa Mungu: “Hii ndiyo maana ya uzima wa milele, wapate maarifa ya kukujua wewe, Mungu wa kweli mmoja tu, na ya yeye uliyemtuma, Yesu Kristo.”—Yohana 17:3, NW.

Kwa hiyo ikiwa sisi twataka kweli kuishi katika ulimwengu mpya wa Mungu, ni lazima sisi kwanza tujue mapenzi ya Mungu ni nini kisha tuyafanye. Kwa maana ni jambo hakika kwamba: “Ulimwengu [huu] unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, bali yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anabaki milele,” ili afurahie milele baraka zitakazomiminwa na Muumba wetu mwenye upendo.—1 Yohana 2:17, NW.

Isipokuwa imeonyeshwa vingine, mitajo yote ya Biblia imetolewa katika Biblia ya Union Version na New World Translation of the Holy Scriptures (NW) ya Kiingereza.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki