Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • re sura 7 kur. 33-37
  • Washa Upya Upendo wa Kwanza!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Washa Upya Upendo wa Kwanza!
  • Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Kufanya Yale Matendo ya Hapo Kwanza”
  • “Yeye Ambaye Hushinda”
  • “Upendo Wako wa Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Kristo Azungumza na Makutaniko
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Kufungua Kufuli ya Siri Takatifu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Sikia Ambacho Roho Husema kwa Makundi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
re sura 7 kur. 33-37

Sura ya 7

Washa Upya Upendo wa Kwanza!

EFESO

1. Ujumbe wa Yesu wa kwanza unaelekezewa kundi gani, naye anawakumbusha waangalizi nini?

UJUMBE wa Yesu wa kwanza ni kwa kundi la Efeso, wakati ule likiwa jiji lenye kusitawi la pwani ya Esia Ndogo karibu na kile kisiwa cha Patmosi. Yeye amwamuru Yohana hivi: “Kwa malaika wa kundi katika Efeso andika: Hivi ndivyo vitu ambavyo yeye anasema ambaye hushika zile nyota saba katika mkono wake wa kulia, yeye ambaye hutembea katikati ya vile vinara vya taa saba vya dhahabu.” (Ufunuo 2:1, NW) Kama ilivyo katika zile jumbe nyingine sita, hapa Yesu anavuta fikira kwenye jambo moja linaloonyesha cheo chake chenye mamlaka. Yeye anakumbusha wale waangalizi wa Efeso kwamba wazee wote wako chini ya uangalizi wake mwenyewe wenye himaya na kwamba yeye anakagua makundi yote. Kuteremka kuingia ndani ya nyakati zetu wenyewe, yeye ameendelea kutumia ukichwa huu wenye upendo, akiwalinda wazee na akichunga kwa fadhili wote wanaoshirikiana na kundi. Wakati kwa wakati, yeye hurekebisha mipango ya kundi ili kuwezesha nuru ing’ae kwa uangavu zaidi. Ndiyo, Yesu ndiye Mchungaji Mkuu juu ya kundi la Mungu.—Mathayo 11:28-30; 1 Petro 5:2-4.

2. (a) Yesu alisifu kundi la Efeso kwa sababu ya mambo gani mema? (b) Kwa wazi wazee Waefeso walikuwa wametii shauri gani la mtume Paulo?

2 Kisha Yesu anaweka kigezo kwa zote ila mbili za jumbe zake saba kwa kufungua kwa maneno machangamfu ya kusifu. Kwa Waefeso, yeye ana ujumbe huu: “Mimi najua matendo yako, na kazi ngumu yako na uvumilivu, na ya kwamba wewe huwezi kuhimili watu wabaya, na ya kwamba uliwaweka kwenye mtihani wale ambao husema wao ni mitume, lakini wao sio, nawe uliwapata kuwa waongo. Pia wewe unaonyesha uvumilivu, na wewe umevumilia kwa minajili ya jina langu nawe hujapata kuchoka.” (Ufunuo 2:2, 3, NW) Miaka fulani kabla ya hapa, mtume Paulo alikuwa ameonya wale wazee wa Efeso juu ya “mbwa-mwitu waonezi,” wasumbuaji wa kundi waasi-imani, naye alikuwa amewaambia wazee hao ‘waendelee kuamka,’ wakifuata kielelezo chake mwenyewe cha kutochoka. (Matendo 20:29, 31, NW) Kwa kuwa sasa Yesu anawasifu kwa ajili ya kazi ngumu yao na uvumilivu na kwa ajili ya kutopata kuchoka, lazima wawe walitumia shauri hilo.

3. (a) “Mitume bandia” wametafutaje kudanganya waaminifu katika siku zetu? (b) Petro alitoa onyo gani juu ya waasi-imani?

3 Katika kipindi cha ile siku ya Bwana, pia, wametokea “mitume bandia” ambao “husema mambo yaliyopopotoka ili kuvuta mbali wale wanafunzi baada yao wenyewe.” (2 Wakorintho 11:13; Matendo 20:30; Ufunuo 1:10, NW) Wao wanaona wema katika zile dini zote za kimafarakano, wakidai kwamba Mungu hana tengenezo, na kukana kwamba Yesu hakupokea uwezo wa Ufalme katika 1914. Wao hutimiza ule unabii kwenye 2 Petro 3:3, 4, NW: “Katika siku za mwisho watakuja wadhihaki pamoja na dhihaka yao, wakiendelea kulingana na tamaa zao wenyewe na kusema: ‘Ku wapi huku kuwapo kwake kulikoahidiwa? Kwani, tangu ile siku mababu wetu walipolala usingizi katika kifo, mambo yote yaendelea sawasawa kama yalivyokuwa tangu mwanzo wa kuumba.’”

4. (a) Kiburi na uasi wa wadhihaki unadhihirishwaje? (b) Wakristo leo wanaonyesha kwamba wao wako kama Waefeso kwa kuchukua tendo gani dhidi ya wapinzani waongo?

4 Wadhihaki hawa wanaasi lile wazo la kufanya tangazo la peupe la imani yao. (Warumi 10:10) Wao wametumia uungaji-mkono wa viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo na msaada wa majarida ya habari na stesheni za TV ili kueneza ripoti za uwongo kuhusu washirika wao wa hapo zamani. Upesi wale waaminifu wanapata kuona kwamba usemi na mwenendo wa wadanganyaji hawa hauna mlio wa ukweli. Kama vile Waefeso, Wakristo leo ‘hawawezi kuhimili watu wabaya,’ kwa hiyo wanawatenga na ushirika watoke katika makundi yao.a

5. (a) Yesu alisema Waefeso walikuwa na udhaifu gani? (b) Ni onyo gani ambalo Waefeso wangalipaswa kukumbuka?

5 Hata hivyo, sasa, kama afanyavyo na matano ya yale makundi saba, Yesu anachagua tatizo moja zito. Yeye anasema kwa Waefeso hivi: “Hata hivyo, mimi nina hili dhidi yako wewe, ya kwamba wewe umeacha upendo ambao wewe ulikuwa nao hapo kwanza.” (Ufunuo 2:4, NW) Haingaliwapasa kushindwa katika hili, kwa kuwa Paulo alikuwa amewaandikia miaka 35 mapema akielekeza kwenye “upendo mkubwa [wa Mungu] ambao kwa huo yeye alitupenda sisi,” naye alikuwa amewahimiza hivi: “Iweni waigaji wa Mungu, mkiwa watoto wapendwa, na mzidi kutembea katika upendo, sawa na vile Kristo pia alivyopenda nyinyi.” (Waefeso 2:4; 5:1, 2, NW) Zaidi, maneno ya Yesu yangalipaswa kuandikwa bila kufutika juu ya mioyo yao: “Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja, na wewe lazima upende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote mzima na kwa nafsi yako yote nzima na kwa akili zako zote nzima na kwa uthabiti wako wote mzima.” (Marko 12:29-31, NW) Waefeso walikuwa wamepoteza upendo huo wa kwanza.

6. (a) Tuwe sisi ni wakale au washiriki wapya katika kundi, ni lazima sisi tujilinde na hatari na maelekeo gani? (b) Upendo wetu kwa Mungu wapaswa utusukume tufanye nini?

6 Tuwe sisi ni wakale au washiriki wapya katika kundi, lazima sisi tulinde dhidi ya kupoteza upendo wetu wa kwanza kwa Yehova. Ni jinsi gani upotezi huu unaweza kutukia? Tungeweza sisi kuruhusu ufungamano kwa kazi yetu ya kimwili, ile tamaa ya kuchuma pesa nyingi, au ule mfuatilio wa anasa uwe ndicho kitu kikubwa katika maisha zetu. Hivyo sisi tungeweza kuwa watu wenye akili za kimnofu badala ya kuwa wenye akili za kiroho. (Warumi 8:5-8; 1 Timotheo 4:8; 6:9, 10) Upendo wetu kwa Yehova wapasa usukume sisi kusahihisha mielekeo yoyote kama hiyo na ‘tufulize kutafuta Ufalme wa Mungu kwanza na uadilifu wake,’ ili ‘tujiwekee hazina katika mbingu kwa ajili yetu wenyewe.’—Mathayo 6:19-21, 31-33, NW.

7. (a) Utumishi wetu kwa Yehova wapasa kusukumwa na kitu gani? (b) Yohana alisema nini kwa habari ya upendo?

7 Acheni utumishi wetu kwa Yehova uwe sikuzote unasukumwa na upendo wenye kina kirefu kwake. Acheni sisi tuwe na uthamini wenye idili kwa yote ambayo Yehova na Kristo wametufanyia sisi. Kama Yohana mwenyewe alivyoandika baadaye: “Upendo uko hivi, si kwamba sisi tumependa Mungu, bali yeye alipenda sisi naye akatuma Mwana wake akiwa dhabihu ya kufunika kwa ajili ya madhambi yetu.” Yohana anaendelea kutuambia sisi hivi: “Mungu ni upendo, na yeye ambaye hubaki katika upendo hubaki katika muungano pamoja na Mungu na Mungu hubaki katika muungano pamoja na yeye.” Sisi tusiache kamwe ufifie upendo wetu kwa Yehova, kwa Bwana Yesu Kristo, na kwa lile Neno la Mungu lenye uhai! Upendo huu tunaweza kuonyesha si katika utumishi wa bidii tu kwa Mungu bali pia kwa utii “kwa amri hii tuliyo nayo kutoka kwake, kwamba mmoja ambaye hupenda Mungu amepaswa kuwa akipenda ndugu yake pia.”—1 Yohana 4:10, 16, 21, NW; Waebrania 4:12; ona pia 1 Petro 4:8; Wakolosai 3:10-14; Waefeso 4:15.

“Kufanya Yale Matendo ya Hapo Kwanza”

8. Yesu alisema inawapasa Waefeso kutendaje?

8 Waefeso hao lazima wawashe upya ule upendo waliokuwa nao wakati mmoja ikiwa wao hawataki kupata hasara. “Kwa hiyo,” Yesu anawaambia, “kumbuka ni kutoka nini wewe umeanguka, na utubu na kufanya yale matendo ya hapo kwanza. Usipofanya, mimi ninakuja kwako wewe, nami nitaondoa kinara cha taa chako kutoka mahali pacho, isipokuwa wewe unatubu.” (Ufunuo 2:5, NW) Wakristo katika kundi la Efeso walipokeaje maneno hayo? Sisi hatujui. Sisi tunatumaini kwamba wao walitubu na kufaulu katika kuamsha tena upendo wao kwa ajili ya Yehova. Ikiwa hawangefanya hivyo, basi taa yao ingezimwa na kinara cha taa chao kingeondolewa. Wao wangepoteza pendeleo lao la kuangaza ule ukweli.

9. (a) Ni neno gani la kutia moyo ambalo Yesu alikuwa nalo kwa ajili ya Waefeso? (b) Makundi baada ya siku ya Yohana yalishindwaje kutii shauri la Yesu kwa Waefeso?

9 Hata hivyo, Yesu ana neno hili la kutia moyo kwa Waefeso: “Ingawa hivyo, wewe una hili, ya kwamba wewe unachukia vile vitendo vya lile farakano la Nikolausi, ambalo mimi pia nachukia.” (Ufunuo 2:6, NW) Angalau wao walichukia mgawanyiko wa kimafarakano, kama na Bwana Yesu Kristo huuchukia. Hata hivyo, miaka ilipozidi kupita, makundi mengi yalishindwa kutii maneno hayo ya Yesu. Ukosefu wa upendo kwa ajili ya Yehova, kwa ajili ya ukweli, na kwa ajili ya mmoja na mwenzake ulitokeza kupeperushwa kwao na kuingizwa ndani ya giza la kiroho. Wakavunjika-vunjika kuwa mafarakano mengi-mengi yenye kugombana. Wanukuaji “Wakristo” ambao hawakuwa na upendo kwa ajili ya Yehova waliondoa jina lenyewe la Mungu kutoka hati za Kigiriki za Biblia. Ukosefu huo wa upendo pia uliruhusu nafasi ya kufundisha mafundisho ya Kibabuloni na Kigiriki kama vile moto wa mateso, pargatori, na Utatu, kwa jina la Ukristo. Kwa kutokuwa na upendo kwa ajili ya Mungu na kwa ajili ya ukweli, walio wengi wa wale ambao walidai kuwa Wakristo waliacha kuhubiri zile habari njema za Ufalme wa Mungu. Wakaja kutawalwa na jamii ya viongozi wa kidini yenye ubinafsi ambayo ikafanya ufalme wayo yenyewe hapa duniani.—Linga 1 Wakorintho 4:8.

10. Hali ya kidini katika Jumuiya ya Wakristo ilikuwaje katika 1918?

10 Hukumu ilipoanza na nyumba ya Mungu katika 1918, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wenye farakano walikuwa wakitoa waziwazi uungaji-mkono wao kwa Vita ya Ulimwengu 2, wakihimiza Wakatoliki na Waprotestanti katika pande zote mbili kuchinjana. (1 Petro 4:17) Tofauti na kundi la Efeso ambalo lilichukia yaliyokuwa yakifanywa na farakano la Nikolausi, kwa muda mrefu dini za Jumuiya ya Wakristo zilikuwa zimejawa na mafundisho yenye kupinga Mungu, yanayohitilafiana, nao viongozi wazo walikuwa wanajiunga na ulimwengu, ambao Yesu alisema wanafunzi wake lazima wasiwe sehemu yao. (Yohana 15:17-19) Makundi yao, kwa kutojua kile kichwa cha Biblia, Ufalme wa Mungu, hayakuwa vinara vya taa vyenye kuangaza ukweli wa Kimaandiko, wala washiriki wayo hawakuwa sehemu ya hekalu la kiroho la Yehova. Wanaume (na wanawake) wayo wenye kuongoza hawakuwa nyota bali walifunuliwa kuwa washiriki wa “yule mtu wa kuasi.”—2 Wathesalonike 2:3; Malaki 3:1-3.

11. (a) Ni kikundi gani cha Kikristo kwenye mandhari ya ulimwengu katika 1918 kilichozoea maneno ya Yesu kwa Waefeso? (b) Jamii ya Yohana ilifanya nini tokea 1919 na kuendelea?

11 Hata hivyo, ile jamii ya Yohana, iliibuka katika zile siku zenye msukosuko za vita ya kwanza ya ulimwengu ikiwa na upendo kwa ajili ya Yehova na kwa ajili ya ukweli ambao uliwasukuma kumtumikia kwa bidii yenye kuwaka mwali. Wao waliwapinga wale waliojaribu kuingiza faraka kupitia tendo lililokaribia sana kumfanya Charles T. Russell, msimamizi wa kwanza wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, awe sanamu ya kuabudiwa, kufuatia kifo chake katika 1916. Wakiwa wametiwa nidhamu kwa minyanyaso na misiba, kikundi hiki cha Kikristo kwa wazi kilipokea hukumu ya kupongezwa “umefanya vema” kutoka kwa Bwana-Mkubwa wao pamoja na mwaliko wa kuingia katika shangwe yake. (Mathayo 25:21, 23, NW) Wao walitambua katika mwendo wa matukio ya ulimwengu na katika mambo waliyojionea wenyewe, utimizo wa ile ishara ambayo Yesu alikuwa ametoa ya kutia alama kuwapo kwake kusikoonekana katika uwezo wa Ufalme. Kutoka 1919 na kuendelea, wao walisonga mbele washiriki utimizo zaidi wa unabii mkubwa wa Yesu: “Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.” (Mathayo 6:9, 10; 24:3-14, NW) Ikiwa upendo wao kwa Yehova ulikuwa umepungukiwa katika njia fulani, ulipepewa tokea wakati huo na kuendelea ukawa mwali wa moto.

12. (a) Kwenye mkusanyiko wa kihistoria katika 1922, ni mwito gani uliotokezwa? (b) Ni jina gani walilokubali Wakristo wa kweli katika 1931, na walitubia nini?

12 Kwenye mkusanyiko wa kihistoria, uliohudhuriwa na 18,000 wa hawa Wakristo, kwenye Sida Pointi, Ohaiyo, U.S.A., Septemba 5-13, 1922, mwito ulitokezwa: “Rudini shambani, Enyi wana wa Mungu aliye juu zaidi sana! . . . Lazima ulimwengu ujue kwamba Yehova ni Mungu na kwamba Yesu Kristo ni Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. . . . Kwa hiyo vumisheni habari, vumisheni habari, vumisheni habari, ya Mfalme na ufalme wake.” Jina la Yehova lenye thamani kubwa lilikuwa linafanywa kuwa mashuhuri zaidi na zaidi. Katika 1931 Wakristo hawa, wakikusanyika katika mkusanyiko huko Kolumbasi, Ohaiyo, U.S.A., walishangilia kulikubali na kuchukua lile jina alilolionyesha Mungu katika unabii wa Isaya—Mashahidi wa Yehova. (Isaya 43:10, 12, NW) Kwa toleo lalo la Machi 1, 1939, jina la jarida kuu la tengenezo hilo lilibadilishwa kuwa Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova, hivyo kumpa heshima ya kwanza Muumba wetu na serikali yake ya kifalme. Mashahidi wa Yehova, wakiwa na upendo kwake uliofanywa upya, wametubia kushindwa kokote ambako huenda wakawa walikuwa nako wakati uliopita katika kuheshimu na kukuza jina lake tukufu na Ufalme wake.—Zaburi 106:6, 47, 48.

“Yeye Ambaye Hushinda”

13. (a) Ni baraka gani iliyongojea Waefeso ikiwa ‘wangeshinda’? (b) Wakristo Waefeso ‘wangeshindaje’?

13 Kwa kumalizia, kama afanyavyo pia katika jumbe zake nyingine, Yesu anavuta fikira kwenye roho ya Mungu kuwa inajulisha kupitia Yesu zile thawabu kwa ajili ya uaminifu. Kwa Waefeso yeye anasema hivi: “Acheni yeye ambaye ana sikio asikie ambacho roho husema kwa makundi: Yeye ambaye hushinda mimi nitaruhusu ale ya mti wa uhai, uliomo katika paradiso ya Mungu.” (Ufunuo 2:7, NW) Wale walio na masikio ya kusikia wangekuwa na hamu nyingi ya kutii ujumbe huo muhimu, wakijua kwamba haukuja kwa kuanzishwa na Yesu bali kwamba huo ulishuka kutoka kwa Bwana Mwenye Enzi Mkuu Yehova mwenyewe kupitia roho takatifu Yake, au kani-tendaji. Wao wangeweza ‘kushindaje’? Kwa kufuata kwa ukaribu hatua za Yesu, ambaye alishika ukamilifu mpaka kifo na hivyo angeweza kusema: “Jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu!”—Yohana 8:28; 16:33; ona pia 1 Yohana 5:4.

14. Ni lazima “paradiso ya Mungu” aliyotaja Yesu iwe ilirejezea nini?

14 Kwa kuwa hao hawana tazamio la kuishi katika paradiso ya kidunia, Wakristo watiwa-mafuta, kama hao Waefeso, wanathawabishwaje kwa kula “ya mti wa uhai, uliomo katika paradiso ya Mungu”? Hiyo haingeweza kuwa Paradiso iliyorudishwa duniani, kwa kuwa Wakristo watiwa-mafuta 144,000, kutia na wale wa kundi la Efeso, wananunuliwa kutoka wanadamu wakatawale pamoja na Mwana-Kondoo, Kristo Yesu, juu ya Mlima Sayuni wa kimbingu wakiwa wana wa kiroho. (Efeso 1:5-12; Ufunuo 14:1, 4) Kwa sababu hiyo, lile rejezo hapa lazima liwe kwenye makao ya kimbingu mithili ya bustani wanayorithi hao washindi. Humo, “katika paradiso ya Mungu,” ndiyo, katika kuwapo halisi kwa Yehova mwenyewe, washindi hawa ambao wameruhusiwa wawe na kutokufa wataendelea kuishi milele, kama inavyofananishwa hapa na kula kwao ya mti wa uhai.

15. Kwa nini kitia-moyo cha Yesu kwamba washinde ni chenye upendezi wa muhimu kwa umati mkubwa wa leo?

15 Namna gani, basi, wale waungaji mkono wa kidunia washikamanifu wa wapakwa-mafuta 144,000? Umati mkubwa wa hawa Mashahidi waandamani wanashinda pia. Lakini tumaini lao hutegemea kuingia katika paradiso ya kidunia ambayo katika hiyo wao watakunywa kutoka “mto wa maji ya uhai” na kupata ponyo kutoka “majani ya miti” iliyopandwa kando-kando za mto huo. (Ufunuo 7:4, 9, 17; 22:1, 2, NW) Ikiwa wewe ni mmoja wa kikundi hiki, wewe pia na uonyeshe upendo wako mchangamfu kwa Yehova na kushinda katika ushindi wa imani. Hivyo wewe huenda ukafikia ile furaha ya uhai wa milele katika dunia Paradiso.—Linga 1 Yohana 2:13, 14.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa habari zaidi ya kihistoria juu ya kutokea kwa mitume bandia, ona kurasa 360-367 za kile kitabu cha mafundisho Kutoa Sababu Kwa Kutumia Maandiko, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Sanduku katika ukurasa wa 36]

Sifa Yenye Upendo kwa Yehova na Mwana Wake

Katika kitabu cha nyimbo kilichotokezwa na watu wa Yehova katika 1905, mlikuwamo nyimbo mara mbili zilizomsifu Yesu kuliko nyimbo zilizomsifu Yehova Mungu. Katika kitabu chao cha nyimbo cha 1928, hesabu za nyimbo zilizomhimidi Yesu zilikuwa karibu sawa na zile zilizomhimidi Yehova. Lakini katika kile kitabu cha nyimbo cha karibuni zaidi cha 1984, Yehova anaheshimiwa kwa nyimbo nyingi mara nne ya zile zinazomheshimu Yesu. Hili linapatana na maneno ya Yesu mwenyewe: “Baba ni mkuu kuliko mimi.” (Yohana 14:28) Upendo kwa ajili ya Yehova lazima utokezwe mbele zaidi, ukiambatana na upendo wenye kina kirefu kwa ajili ya Yesu na uthamini wa dhabihu yake yenye thamani kubwa na ofisi yake akiwa Kuhani Mkuu na Mfalme wa Mungu.

[Picha katika ukurasa wa 34]

Kigezo cha Yesu cha Shauri

(kwa kutaja sura na mistari katika Ufunuo)

Ujumbe kwa Mamlaka Tatizo Sahihisho

kundi la ya kutoa Pongezi la latambulishwa na/au Baraka

shauri utangulizi waziwazi kitia-moyo zitokeazo

Efeso 2:1 2:2, 3 2:4 2:5, 6 2:7

Smirna 2:8 2:9 — 2:10 2:11

Pargamamu 2:12 2:13 2:14, 15 2:16 2:17

Thiatira 2:18 2:19 2:20, 21 2:24, 25 2:26-28

Sardisi 3:1 — 3:1, 2 3:3, 4 3:5

Filadelfia 3:7 3:8 — 3:8-11 3:12

Laodikia 3:14 — 3:15-17 3:18-20 3:21

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki