Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • pe sura 9 kur. 81-89
  • Je! Kweli Kuna Mahali Penye Moto wa Mateso?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Kweli Kuna Mahali Penye Moto wa Mateso?
  • Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • 3. Sababu gani ni jambo lisilo la akili, vilevile lisilopatana na Maandiko, kudhani kwamba Mungu angetesa watu? 3 Fikiria hilo. Ikiwa wazo la kuchoma watu katika moto halikuingia kamwe katika moyo wa Mungu, je! linaonekana kuwa jambo la busara kwamba yeye aliumba mahali penye moto ili kuchoma wale wasiomtumikia? Biblia inasema, “Mungu ni upe-ndo.” (1 Yohana 4:8) Je! kweli Mungu wa upendo angetesa watu milele? Je! wewe ungefanya hivyo? Kujua juu ya upendo wa Mungu kunapasa kutuongoza tuchunguze Neno lake ili tuone kama kweli kuna mahali pa mateso ya milele.
  • SHEOLI NA HADESI
  • KUTOKA KATIKA SHEOLI
  • GEHENA (JEHANUM) NA ZIWA LA MOTO
  • MTU TAJIRI NA LAZARO
  • MAFUNDISHO YENYE KUONGOZWA NA IBILISI
  • Namna Ambavyo Ufufuo Unavyowafaidi Wafu Wote Waliomo Katika “Hell”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Je, Kweli Kuna Mahali Penye Moto wa Mateso?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Ni Nani Wanaoenda Kuzimu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je, Moto wa Mateso Ni Halisi? Kuzimu Ni Wapi Kulingana na Biblia?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
pe sura 9 kur. 81-89

Sura 9

Je! Kweli Kuna Mahali Penye Moto wa Mateso?

1. Dini zimefundisha nini juu ya moto?

MAMILIONI ya watu wamefundishwa na dini zao kwamba kuna mahali pa mateso ya milele. Ndipo wabaya wanapokwenda. Kulingana na kitabu Encyclopædia Britannica, “Kanisa la Roma Katoliki linafundisha kwamba hell . . . (mahali pa mateso) itaendelea milele; mateso yake hayatakuwa na mwisho.” Kitabu hicho kinaendelea kusema mafundisho hayo ya Kikatoliki “yangali yakifuatwa na vikundi vingi vya Kiprotestanti vinavyoshikilia maoni yale yale bila kubadilika.” Wahindu, Wabuddha na wafuasi wa Muhamadi vilevile wanafundisha kwamba kuna mahali pa mateso. Si ajabu kwamba watu ambao wamefundishwa hivyo wanasema mara nyingi kwamba iwapo kuna mahali pabaya namna hiyo hawataki kuzungumza juu yake.

2. Mungu alionaje juu ya kuchoma watoto katika moto?

2 Hilo linatokeza ulizo hili: Je! Mungu Mweza Yote aliumba mahali kama hapo penye mateso? Basi, Mungu alikuwa na maoni gani wakati Waisraeli walipoanza kuwachoma watoto wao katika moto kwa kufuata mfano wa mataifa jirani? Anaeleza hivi katika Neno lake: “Nao wamepajenga mahali palipoinuka pa Tofethi, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ili kuwateketeza wana wao na binti zao motoni; jambo ambalo mimi sikuliagiza, wala halikuingia moyoni mwangu.”—Yeremia 7:31.

3. Sababu gani ni jambo lisilo la akili, vilevile lisilopatana na Maandiko, kudhani kwamba Mungu angetesa watu?

3 Fikiria hilo. Ikiwa wazo la kuchoma watu katika moto halikuingia kamwe katika moyo wa Mungu, je! linaonekana kuwa jambo la busara kwamba yeye aliumba mahali penye moto ili kuchoma wale wasiomtumikia? Biblia inasema, “Mungu ni upe-ndo.” (1 Yohana 4:8) Je! kweli Mungu wa upendo angetesa watu milele? Je! wewe ungefanya hivyo? Kujua juu ya upendo wa Mungu kunapasa kutuongoza tuchunguze Neno lake ili tuone kama kweli kuna mahali pa mateso ya milele.

SHEOLI NA HADESI

4. (a) Biblia inaonyeshaje kwamba maana ya Sheoli na Hadesi ni moja? (b) Ni nini linaloo-nyeshwa na uhakika wa kwamba Yesu alikuwa katika Hadesi?

4 Kwa kupataja mahali ambapo wanadamu wanakwenda wakati wa kufa, Biblia inatumia neno “Sheoli” katika Maandiko ya Kiebrania na “Hadesi” katika Maandiko ya Kigiriki. Kwa kutazama Zaburi 16:10 na Matendo 2:31, ni wazi kwamba maneno kayo yana maana moja. Angalia kwamba katika kutumia maneno ya Zaburi 16:10 ambapo Sheoli linaonekana, Matendo 2:31 hutumia Hadesi. Inadaiwa na watu fulani kwamba Hadesi ni mahali pa mateso ya milele. Lakini kumbuka kwamba Yesu Kristo alikuwa katika Hadesi. Je! tuamini kwamba Mungu alimtesa Kristo katika mahali penye moto? Hapana! Alipokufa, Yesu alikwenda kwenye kaburi lake.

5, 6. Yale yanayosemwa juu ya Yakobo na Yusufu mwanawe, na juu ya Ayubu, yanahakikishaje kwamba Sheoli si mahali pa mateso?

5 Mwanzo 37:35, NW, hutuambia juu ya Yakobo, anayemwomboleza Yusufu mwanawe mpendwa ambaye alidhani ameuawa. Biblia inasema juu ya Yakobo hivi: “Aliendelea kukataa kufarijiwa na kusema: ‘Kwa maana nitashuka ndani ya Sheoli hali nikiomboleza mwanangu!’” Sasa ngoja kidogo ufikiri. Je! Sheoli palikuwa mahali pa mateso? Je! Yakobo aliamini kwamba Yusufu mwanawe alikwenda huko akakae milele, na je! alitaka kwenda huko wakawe pamoja? Au, wazo la Yakobo lilikuwa kwamba mwanawe mpendwa alikuwa amekufa akawa kaburini tu, kisha Yakobo pia akataka kufa?

6 Ndiyo, watu wazuri wanakwenda Sheoli. Kwa mfano, mfikirie Ayubu anayejulikana kuwa mwaminifu na mwenye ukamilifu kwa Mungu. Alipokuwa akiteswa sana, alimwomba Mungu amsaidie. Sala yake imeandikwa katika Ayubu 14:13, NW: “0 afadhali ungenificha katika Sheoli, . . . afadhali ungeniwekea ukomo wa wakati na kunikumbuka mimi!” Sasa fikiri: Ikiwa Sheoli ni mahali pa moto na mateso, je! Ayubu angetaka kwenda kukaa huko mpaka Mungu amkumbuke? Kwa wazi, Ayubu alitaka kufa aende kwenye kaburi ili mateso yake yamalizike.

7. (a) Wale walio katika Sheoli wako katika hall gani? (b) Hivyo Sheoli na Hadesi ni nini?

7 Mahali pote ambapo neno Sheoli linaonekana katika Biblia halihusiani kamwe na uhai, utendaji wala mateso. Badala yake, mara nyingi linahusiana na kifo na kutokutenda jambo lo lote. Kwa mfano, fikiria Mhubiri 9:10, NW, linalosomwa hivi: “Yote ambayo mkono wako unapata kufanya, fanya kwa uwezo wako wenyewe, kwa maana hakuna kazi wala kubuni wala maarifa wala hekima katika Sheoli, mahali unakoenda wewe.” Basi jibu linakuwa wazi sana. Sheoli na Hadesi maana yake si mahali pa mateso bali kaburi la ujumla la wanadamu wote. (Zaburi 139:8) Watu wazuri na wabaya pia wanakwenda huko Sheoli, au Hadesi.

KUTOKA KATIKA SHEOLI

8, 9. Sababu gani Yona alipokuwa katika tumbo la samaki alisema alikuwa katika Sheoli?

8 Je! watu wanaweza kutoka katika Sheoli (Hadesi)? Fikiria kisa cha Yona. Mungu alipoagiza samaki mkubwa ammeze Yona ili amwokoe asife maji, Yona alisali hivi akiwa katika tumbo la samaki huyo: “Katika taabu kubwa yangu nilimwita Yehova kwa kupaza sauti, naye akachukua hatua ya kunijibu mimi. Katika tumbo la Sheoli nilililia msaada. Wewe ukasikia sauti yangu.”—Yona 2:2, NW.

9 Yona alikuwa na maana gani kwa kusema “katika tumbo la Sheoli”? Bila shaka, lile tumbo la samaki halikuwa mahali pa moto wa mateso. Lakini lingaliweza kuwa ndilo kaburi la Yona. Kwa kweli, Yesu Kristo alisema kwa habari yake mwenyewe hivi: “Kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi.” —Mathayo 12:40.

10. (a) Kuna ushuhuda gani wa kwarnba wale walio katika Sheoli wanaweza kutoka humo? (b) Kuna ushuhuda gani zaidi wa kuonyesha kwamba Sheoli maana yake ni “kaburi”?

10 Yesu alikufa akawa katika ka-buri lake muda wa siku tatu. Lakini Biblia inaripoti hivi: “Wala yeye hakuachwa katika Hadesi Yesu huyu Mungu alimfufua.” (Matendo 2:31, 32, NW) Vivyo hivyo, kwa kuelekezwa na Mungu, Yona alifufuliwa katika Sheoli, yaani, mahali ambapo pangalikuwa kaburi lake. Hilo lilitukia wakati samaki alipomtapika nje kwenye nchi kavu. Ndiyo, watu wanaweza kutoka katika Sheoli! Kwa kweli, ile ahadi yenye kuchangamsha moyo inayotolewa katika Ufunuo 20:13, NW, ni ya kwamba ‘kifo na Hadesi zitawatoa wafu hao walio ndani vazo.’ Lo! jinsi mafundisho ya Biblia juu ya hali ya wafu yalivyo tofauti na yale ambayo dini nyingi zimekuwa zikifundisha!

GEHENA (JEHANUM) NA ZIWA LA MOTO

11. Gehena ni nini. na kulifanyika nini huko?

11 Hata hivyo huenda mtu fulani akapinga, akisema: ‘Biblia inasema juu ya moto wa Gehena na ziwa la moto. Je! hiyo haionyeshi kwamba kuna mahali pa mateso?’ Je! kweli Gehena ni mahali pa mateso ya moto, hali Hadesi inamaanisha kaburi? Kwa wazi, neno la Kiebrania “Sheoli,” na neno la Kigiriki ‘Hadesi,” yote yanamaanisha kaburi. Basi, Gehena maana yake nini? Katika Maandiko ya Kiebrania Gehena ni “lile bonde la Hinomu.” Kumbuka, Hinomu lilikuwa jina la bonde lililokuwa mwendo mfupi tu nje ya kuta za Yerusalemu ambako Waisraeli waliwatoa watoto wao wawe dhabihu katika moto. Baadaye, Mfalme Yosia mwema aliagiza bonde hilo liache kutumiwa kwa mazoea hayo mabaya sana. (2 Wafalme 23:10) Liligeuzwa kuwa mahali pakubwa sana pa kutupia takataka (uchafu).

12. (a) Katika siku za Yesu. Gehena ilitumiwa kwa kusudi gani? (b) Ni kitu gani ambacho hakikutupwa kamwe humo?

12 Hivyo wakati Yesu alipokuwa hapa duniani Gehena ndipo palipokuwa pa kutupia takataka za Yerusalemu. Mioto ilifanywa iendelee kuwaka huko kwa kuongeza kiberiti (sulfur) ili kuteketeza takataka hiyo. Smith’s Dictionary of the Bible (Kamusi ya Biblia Iliyotungwa na Smith), Kitabu I, inaeleza hivi: “Pakawa mahali pa watu wote pa kutupia takataka za mji huo, maiti za wahalifu, mizoga ya wanyama na uchafu wa kila aina nyingine.” Walakini, hakuna viumbe vilivyo hai vilivyotupwa hapo.

13. Kuna ushuhuda gani wa kwamba Gehena ilitumiwa kuwa mfano wa uharibifu wa milele?

13 Kwa kuwa waliijua hali ya mahali pa kutupia takataka za mji wao, wakazi wa Yerusalemu walifahamu maana ya Yesu alipowaambia viongozi wale waovu wa kidini: “Ninyi nyoka, ninyi wana wa majoka, mutakimbia hukumu ya Gehena namna gani?” (Matayo 23:33, ZSB) Kwa wazi Yesu hakumaanisha kwamba viongozi hao wa kidini wangeteswa. Kwani, Waisraeli walipokuwa wakichoma watoto wao wakiwa hai katika bonde hilo, Mungu alisema kwamba ubaya huo mkubwa haukuwa umeingia katika moyo wake hata siku moja! Hivyo ilikuwa wazi kwamba Yesu alikuwa akitumia Gehena kuwa mfano unaofaa wa uharibifu kamili na wa milele. Alimaanisha kwamba viongozi hao waovu wa kidini hawakustahili ufufuo. Wale waliokuwa wakimsikiliza Yesu waliweza kufahamu kwamba wale wanaokwenda Gehena, kama takataka nyingi, wangeharibiwa milele.

14. “Lile ziwa la moto” ni nini, na kuna ushuhuda gani wa kuonyesha hivyo?

14 Basi, “lile ziwa la moto” ni nini linalotajwa katika kitabu cha Biblia cha Ufunuo? Lina maana inayofanana na ile ya Gehena. Halimaanishi mateso katika hali ya kufahamu bali kifo cha milele, au uharibifu wa milele. Angalia jinsi Biblia yenyewe inavyosema hilo katika Ufunuo 20:14, NW: “Na kifo na Hadesi vilivurumishwa katika lile ziwa la moto. Hii maana yake ni kifo cha pili, hilo ziwa la moto.” Ndiyo, hilo ziwa la moto maana yake ni “kifo cha pili,” kifo ambacho katika hicho hakutakuwa na ufufuo. Ni wazi kwamba hilo “ziwa” ni mfano, kwa sababu kifo na Hadesi zinatupwa ndani yalo. Kifo na Hadesi haviwezi kuchomwa kwa njia halisi. Lakini vinaweza kuondolewa na vitaondolewa, au kuharibiwa.

15. Ni nini maana ya kusema kwamba Ibilisi atateswa milele katika “lile ziwa la moto”?

15 ‘Lakini Biblia inasema Ibilisi atateswa milele na milele katika ziwa la moto.’ Labda mtu fulani atasema hivyo. (Ufunuo 20:10) Hiyo maana yake nini? Yesu alipokuwa hapa duniani askari wa magereza nyakati nyingine waliitwa “watesaji.” Kama vile Yesu alivyosema habari ya mtu fulani katika mmoja wa mifano yake: “Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.” (Mathayo 18:34) Kwa kuwa wale wanaotupwa katika “lile ziwa la moto” wanaingia katika “kifo cha pili” ambacho katika hicho hakutakuwa na ufufuo, wanafungwa milele kwa namna ya mfano katika gereza la kifo. Wanakaa katika kifo kana kwamba wanalindwa na askari wa gereza kwa umilele wote. Bila shaka waovu hao hawateswi kwa njia halisi kwa sababu, kama tulivyokwisha kuona, mtu anapokufa anakwisha kabisa. Yeye hafahamu jambo lo lote.

MTU TAJIRI NA LAZARO

16. Tunajuaje kwamba maneno ya Yesu juu ya mtu tajiri na Lazaro ni mfano?

16 Basi, Yesu alikuwa na maana gani aliposema hivi katika mmoja wa mifano yake: “Mwombaji huyo akafa naye akachukuliwa na malaika mpaka mahali pa kifua cha Abrahamu. Pia yule mtu tajiri akafa na akazikwa. Na katika Hadesi aliinua macho yake, akiwa katika mateso, akamwona Abrahamu kwa umbali na Lazaro mahali pa kifua pamoja naye”? (Luka 16:19-31, NW) Kwa kuwa, kama tulivyokwisha kuona, Hadesi inamaanisha kaburi la wanadamu, wala si mahali pa mateso, ni wazi kwamba hapa Yesu alikuwa akisimulia mfano au hadithi. Kama ushuhuda zaidi kuonyesha kwamba hayo si masimulizi halisi bali ni mfano tu, fikiria hili: Je! mahali penye moto wa mateso ni karibu sana na mbingu hivi kwamba mazungumzo halisi yangeweza kuendelea hivyo? Tena, kama mtu tajiri angekuwa katika ziwa halisi linalowaka moto, Abrahamu angewezaje kumtuma Lazaro ili apoleze ulimi wake kwa tone moja tu la maji katika ncha ya kidole chake? Basi, Yesu alikuwa akifananisha nini?

17. Mfano huo una maana gani kwa habari ya (a) yule mtu tajiri? (b) Lazaro? (c) kifo cha kila mmoja? (d) yale mateso ya mtu tajiri?

17 Yule mtu tajiri katika mfano alifananisha viongozi wa kidini wenye kujikuza waliomkataa Yesu na baadaye wakamwua. Lazaro alifananisha watu wa cheo cha kawaida waliomkubali Mwana wa Mungu. Kifo cha mtu tajiri na Lazaro kilifananisha badiliko la hali yao. Badiliko hilo lilitokea wakati Yesu alipolisha watu walio mfano wa Lazaro ambao hawakuangaliwa kiroho, hata wakaja katika upendeleo wa yule Abrahamu Mkubwa Zaidi, yaani, Yehova Mungu. Wakati uo huo, wale viongozi wa kidini wa uongo ‘walikufa’ kwa vile hawakuwa na upendeleo wa Mungu. Wakiwa wametupiliwa mbali, waliteseka wakati wafuasi wa Kristo walipofunua kazi zao zenye uovu. (Matendo 7:51-57) Basi mfano huo haufundishi kwamba wafu fulani wanateswa mahali halisi penye moto.

MAFUNDISHO YENYE KUONGOZWA NA IBILISI

18. (a) Ni uongo gani ambao Ibilisi ameeneza? (b) Sababu gani tunaweza kuwa na hakika kwamba mafundisho ya purgatori ni ya uongo?

18 Ni Ibilisi aliyemwambia Hawa hivi: “Hakika hamtakufa.” (Mwanzo 3:4; Ufunuo 12:9) Lakini Hawa alikufa kweli; hakuna sehemu ya mwili wake iliyoendelea kuishi. Kusema kwamba nafsi inaendelea kuishi baada ya kufa ni uongo ulioanzishwa na Ibilisi. Na vilevile kusema kwamba nafsi za watu zinateswa katika moto au purgatori (toharani) ni uongo ambao Ibilisi amepanga uenezwe. Kwa kuwa Biblia inaonyesha waziwazi kwamba wafu hawana fahamu, mafundisho hayo hayangeweza kuwa ya kweli. Kwa hakika, wala neno “purgatori” wala wazo la purgatori halipatikani katika Biblia.

19. (a) Tumejifunza nini kutokana na sura hii? (b) Kujua mambo haya kumekufanya uwe na maoni gani?

19 Tumekwisha kuona kwamba Sheoli, au Hadesi, ni mahali pa kupumzikia wafu likiwapo tumaini kwa ajili yao. Watu wema na wabaya pia wanakwenda huko, kungojea ufufuo. Tumekwisha kujifunza vilevile kwamba Gehena haimaanishi mahali pa mateso, bali inatumiwa katika Biblia kuwa mfano wa uharibifu wa milele. Katika njia iyo hiyo, “lile ziwa la moto” si mahali halisi penye moto, bali linafananisha “kifo cha pili” ambacho katika hicho hakutakuwa na ufufuo. Hapo hapangeweza kuwa ni mahali pa mateso kwa sababu wazo kama hilo halikuingia kamwe katika akili wala moyo wa Mungu. Isitoshe, kutesa mtu milele kwa sababu alifanya mabaya hapa duniani kwa miaka michache ni kinyume cha kaki ya hukumu. Ni vema kama nini kuijua kweli juu ya wafu! Kunaweza kutuweka huru kweli kweli ili tusiwe na woga wala ushirikina.—Yohana 8:32.

[Sanduku katika ukurasa wa 83]

Neno Ia Kiebrania “Sheoli” lina maana moja na neno Ia Kigiriki “Hadesi”

American Standard Version

Psalm 16:10

10 For thou wilt not leave my soul

to Shēʹōl;

Neither wilt thou suffer thy

holy one to see corruption.

Acts 2:31

31 he foreseeing this spake of the resurrection of the Christ, that neither was he left unto Hāʹdēs, nor did his flesh see corruption.

[Picha katika ukurasa wa 84, 85]

Baada ya kumezwa na samaki, sababu gani Yona alisema: ‘Katika tumbo is Sheoli nikalia’?

[Picha katika ukurasa wa 86]

Gehena ilikuwa bonde la nje ya Yerusalemu. Ilitumiwa kuwa mfano wa kifo cha milele

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki