Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 4/15 kur. 173-182
  • Namna Ambavyo Ufufuo Unavyowafaidi Wafu Wote Waliomo Katika “Hell”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Namna Ambavyo Ufufuo Unavyowafaidi Wafu Wote Waliomo Katika “Hell”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ZAMANI AMBAZO “HELL” ILIKUWAKO
  • “HELL” HAIKUWAKO
  • “HELL” KATIKA MAANDIKO YA KIKRISTO YA KIGIRIKI
  • “JEHANUM”
  • HAWAFUTILIWI MBALI KATIKA “HELL” MILELE?
  • Je! Kweli Kuna Mahali Penye Moto wa Mateso?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Wale Watakaopata Faida za Ufufuo Kutoka “Hell”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Ni Nani Wanaoenda Kuzimu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je, Kweli Kuna Mahali Penye Moto wa Mateso?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 4/15 kur. 173-182

Namna Ambavyo Ufufuo Unavyowafaidi Wafu Wote Waliomo Katika “Hell”

“Kama tu ungenificha katika Sheol, na kunikinga mimi humo mpaka hasira yako imepita.”​—Ayubu 14:13, Jerusalem Bible Version ya Katoliki ya Kirumi.

1, 2. (a) Dai linaloshangaza la Mnara wa Mlinzi juu ya hell linatokeza maulizo gani? (b) Ni maulizo gani ambayo huenda wale wanaoweza kuwa wakiishi wakati huo wakaelekea kuuliza juu yao wenyewe?

HAPO kale hell, au mahali panapotajwa kama penye moto zinakotesewa nafsi za watenda mabaya wasiotubu, haikuwako. Na kutakuwako wakati mwingine tena ambapo hell haitakuwako. Kwa sababu ya dai hilo linaloshangaza, huenda watu waulize: Hii itakuwaje? N’nani atakayefanya hili litukie? Je! tutaishi mpaka limetukia?

2 Tunapozungumza juu ya kuishi kwetu tukauone wakati ambapo hell haitakuwako, tunaelekea kuuliza: Je! hii itatufaidi sisi tutakaokuwa tukiishi duniani wakati huo? Je! kutoweka kwa hell kutatokeza makundi ya watu wa namna iliyo mbaya zaidi kuziharibu hali zetu za adili na za kijamii hata zaidi kuliko zilivyo leo? Shauri hilo linashtua, linaogofisha. Ingekuja faida gani kutokana na hili kwa ye yote, kwa Mungu au kwa mwanadamu, zaidi kwetu sisi ambao tayari tumesumbuliwa na taabu na wanaoileta? Haya yanaelekea kuwa maulizo magumu. Bila shaka kila mtu atapendezwa kuyasikia. Ndipo tunapoweza kufahamu kinachokuja kweli.

3. Tyndale, Luther, na Jerome walilitafsiri neno la kwanza la Kigiriki katika Mathayo 11:23 namna gani, naye Dante alipafananisha mahali penyewe kwa njia gani?

3 Sikuzote hell imekuwa na ukamatano wa kidini. Kwa hiyo Kitabu kilicho cha zamani zaidi cha kidini, Biblia, kimepaswa kutoa majibu yafaayo. Nacho chafanya lili hili. Neno la Kiingereza hell limetumiwa katika usemi kwa karne nyingi. Kwa mfano, wakati ambapo mtafsiri wa Biblia aliyeteswa, William Tyndale, alitafsiri sehemu ya Kigiriki ya Biblia ya kwanza, kulingana na kuendeleza kwake katika mwaka wa 1525 alisema hivi katika Mathayo 11:23: “Nawe Kapernaumu, wewe uliyeko juu mbinguni, utashushwa hata hell.” Wakati ambapo Dr. Martin Luther aliyatafsiri hayo Maandiko ya Kikristo ya Kigiriki katika Kijeremani katika mwaka wa 1522, alilitumia neno la Kijeremani lenye matamshi ya namna ile ile Hoelle. Lakini Mtakatifu Jerome wa Katoliki ya Kirumi alipoyatafsiri maandiko yale yale katika Kirumi kutoka Kigiriki, katika mwaka wa 383 C.E., alilitumia neno infernus. Kwa hiyo mtunga mashairi Mwitaliano wa karne ya kumi na nne, Dante Alighieri, aliliandika shairi lake lijulikanalo sana kama Mchezo wa Kuigiza wa Kimungu na kuiita sehemu yake ya kwanza Inferno. Aliionyesha “Inferno” kama shimo lenye kina kirefu lenye mizingo inayokuwa myembamba kidogo kidogo ambamo nafsi za kibinadamu zilizolaaniwa zilitaabikia mwili ulipokufa. Je! Dante alisema kweli?

4. Mfano ambao viongozi wa kidini wa Kristendomu wanafanyiza juu ya hell unategemea fundisho gani wanalolifundisha?

4 Viongozi wa kidini wa Kristendomu wamefanyiza mfano wa wanachokifahamu kuwa hell au “inferno” katika akili za watu wao wa makanisa. Ni mfano wa kuogofya. Maoni yao ya hell au “inferno” yaliyofundishwa kwa muda mrefu yanalitegemea fundisho wanalolifundisha juu ya nafsi ya kibinadamu. Wanadhani kwamba nafsi ya kibinadamu ni kitu kilicho tofauti na kilicho kando ya mwili wa kibinadamu. Vile vile, kwamba, ujapokuwa mwili wa kibinadamu unaweza kufa na kuharibika, nafsi ya kibinadamu haifi nayo haiharibiki, kwa maana ni ya kiroho na hivyo isiyoonekana, kitu ambacho hatuwezi kukigusa.

5. Wakati wa kufa nafsi inakwenda wapi, kulingana na viongozi wa kidini, nayo hell yatofautishwaje na mbinguni?

5 Kwa hiyo, kama vile wasemavyo viongozi wa kidini, wakati mwili wa kibinadamu unapokufa, nafsi ya kibinadamu haifi bali inaendelea kuishi, ijapokuwa hatuwezi kuiona kwa macho yetu ya asili. Kwa maana sasa lazima iuache mwili ambamo imekuwa ikikaa, lazima iende mahali fulani katika ulimwengu usioonekana, wa kiroho. Lakini wapi? Ikisemwa kwa vyepesi, nafsi njema zinakwenda mbinguni, lakini nafsi mbaya zinakwenda hell. Hivyo mbinguni panaonyeshwa kama mahali palipo tofauti na “hell,” na kwa kuwa mbinguni ni mahali pa furaha ya milele na baraka, hivyo lazima “hell” pawe ni mahali pa mateso ya milele. Viongozi wa kidini wanasema moto na kiberiti vimo katika hell.

6. Je! Biblia yafundisha kuna hell, na ni njia gani ya kuamua mahali hapo ni pa namna gani?

6 Kwa karne nyingi viongozi wa kidini wa Kristendomu wamefundisha maoni hayo ya hell. Kwa kuwa wanadai kwamba wanavyofundisha ni ambavyo Biblia Takatifu inasema juu ya “hell,” inatupasa twende moja kwa moja kwenye Biblia yenyewe tuone jambo lenyewe inayolisema juu ya habari hii. Oh ndiyo, neno “hell” au “inferno” linapatikana katika tafsiri za Biblia mbalimbali mara nyingi, na kulingana na tafsiri hizo Biblia yafundisha kwamba kuna hell. Lakini jambo lenyewe ni, Je! waandikaji wa Biblia walisema nini nao waliionyesha “hell” hii kuwa nini? Lazima tufuate wanavyoionyesha kuwa, wala siyo vile wengine wanavyosema waandikaji hao wa Biblia waliisema kuwa. Twaweza kujidanganya wenyewe kwa kuyapotoa wanayoyasema waandikaji hao wa Biblia.

ZAMANI AMBAZO “HELL” ILIKUWAKO

7. Ni zamani kama wakati gani twajua kwamba “hell” ilikuwako, nalo ni neno gani la lugha ya kale lililotumiwa kwanza kuitaja?

7 Twajua kwamba “hell” hii ilikuwako walau hata mwaka wa 1750 mbele ya Wakati wetu wa Kawaida, yaani zaidi ya miaka 3,720 iliyopita. Ndio mwaka ambapo ndugu wenye kijicho wa baba-mzazi mmoja na Yusufu mwana wa Yakobo walimwuza Yusufu utumwani katika Misri. Wakati fulani ulipopita ndugu hao wa baba-mzazi mmoja walimdanganya baba yao Yakobo juu ya kilichokuwa kimempata mwana wake mpendwa Yusufu. Walimpa maoni ya kwamba Yusufu alikuwa ameuawa na mnyama wa mwitu. Je! mzee wa ukoo Yakobo alisema nini akihuzunika? Je! alisema mwanawe Yusufu sasa alikuwa wapi? Yakobo alikuwa Mwebrania, nayo tafsiri ya Kikatoliki Jerusalem Bible inalionyesha neno la Kiebrania alilolitumia Yakobo, katika Mwanzo 37:35. Hapo twasoma: “Wana wake wote na binti wakaja wamfariji, lakini yeye akakataa kufarijiwa. ‘Sivyo,’ akasema, ‘mimi nitashuka Sheol nikiomboleza, kando ya mwanangu.’ “Miaka mingi kufuata hapo, wakati ndugu za baba-mzazi mmoja na Yusufu walipoomba ruhusa wamchukue ndugu mwenyewe wa Yusufu Benyamini mpaka Misri, Yakobo alilitumia tena neno la Kiebrania na kusema: “Dhara lo lote likimpata katika safari mtakayoifunga, mtanishusha mimi hata Sheol nikiinama kichwa changu chenye mvi katika huzuni.”​—Mwa. 42:38; tazama vile vile 44:29, 31.

8. (a) Ni neno gani alilolitumia Jerome katika tafsiri yake ya Kirumi ya maneno ya Yakobo? (b) Ni neno gani lililotumiwa na Tafsiri ya Biblia ya Kiingereza ya Douay, na kwa hiyo Yakobo aliamini mwanawe Yusufu alikuwa wapi?

8 Wakatoliki hawapaswi kuusahau uhakika wa kwamba tafsiri yao ya Kirumi ya Mtakatifu Jerome ya maneno ya Yakobo hapa hailitumii neno la Kiebrania Sheol. Inalitumia neno la Kirumi “infernus” na neno jingine kama hilo “inferi.” Lakini tafsiri ya Douay ya Katoliki ya Kiingereza inalitumia neno hell katika sehemu zote nne. Basi, hii yamaanisha kwamba mzee wa ukoo Yakobo aliamini kwamba mwana wake mpendwa Yusufu alikuwa katika “Sheol,” katika infernus, katika “hell.” Vile vile, Yakobo alitarajia kwenda huko akaungane na mwanawe.

9. Kwa sababu gani, kulingana na Malaki 1:2, 3, ni vigumu kwetu kuamini kwamba Yakobo alitarajia kwenda mahali kama pale ambapo viongozi wa kidini wamefundisha kwa muda mrefu?

9 Je! hii haitustaajabishi? Je! kweli Yakobo alitarajia kwenda kwenye “hell” ilivyo kama ambavyo viongozi wa kidini wa Kristendomu wameisimulia kwa watu wa makanisa kwa karne nyingi? Je! Yakobo alitarajia kwenda mahali penye mateso ya moto ya nafsi yake, ambapo asingeweza kutoka kamwe; na je! yeye aliamini kwamba mwana wake mzuri sana Yusufu alikuwamo katika mahali kama hapo? Kwa hiyo je! Yakobo na mwanawe Yusufu wamo katika mahali hapo pa mateso ya moto ya milele leo nyuma ya zaidi ya miaka 3,600 tangu kifo chao? Ni vigumu kwetu kuamini hivyo kwa maana katika kitabu kile kile cha mwisho cha Maandiko ya Kiebrania yaliyoongozwa na roho ya Mungu Bwana Mungu anasema hivi kupitia kwa nabii wake Malaki: “Nimempenda Yakobo; bali [ndugu yake pacha] Esau nimemchukia.”​—Mal. 1:2, 3.

10. Ni wakati gani Yakobo alipokwenda “hell,” naye aliungana na nani humo?

10 Kwa hakika, ni wakati gani Yakobo kama mwanamume aliyependwa na Mungu alipokwenda “Sheol,” infernus, “hell”? Hii ilikuwa alipokufa katika mwaka wa 1711 B.C.E., naye Yusufu aliyekuwa angali hai na ndugu zake wakaichukua maiti iliyotiwa dawa isioze na kuiweka katika pango la Makpela. Hii ni katika mji wa Hebroni, ambao leo umo katika nchi ya Israeli. Katika pango lile lile baba yake Yakobo Isaka alilala amezikwa, vile vile babu yake Ibrahimu. Hivyo Yakobo aliungana na Ibrahimu na Isaka katika “Sheol,” katika infernus, katika “hell.”​—Mwanzo 49:33 mpaka 50:13.

11. (a) Martin Luther na Authorized Version ya Mfalme James alisaidiaje kufahamu “hell” hii ni nini? (b) Watafsiri wa Kiyahudi walilitafsirije neno lao wenyewe la Kiebrania Sheol, nalo neno hili lina maana nyingi kadiri gani?

11 Hakuna sababu ya Biblia ya kuamini kwamba wazee hao wote watatu wa ukoo wa Kiebrania wanataabika leo katika hell ya mateso ya moto wa milele. Twasaidiwa kutoka katika ugumu huu wa kufahamu na watafsiri wengine wa Biblia. Kwa mfano, aliyekuwa padre wa Kikatoliki, Martin Luther, analitafsiri neno Sheol kama “shimo” (die Grube). Halafu katika karne iliyomfuata Luther, Biblia ya Kiingereza iliyohalalishwa na Mfalme James wa Kwanza wa Uingereza, katika mwaka wa 1611 C.E., ilitafsiri Sheol kama “kaburi.” Waebrania, Wayahudi wenyewe, wanapaswa kujua neno lao wenyewe Sheol linachomaanisha; na kwa hiyo tafsiri ya Kiingereza ya Biblia ya Jewish Publication Society of America inalitafsiri neno hili kama “kaburi.” (Mwaka wa 1917 C.E.) Ndivyo vile vile na tafsiri ya Kiingereza ya mwalimu wa Kiyahudi, Isaac Leeser. (Mwaka wa 1853 C.E.) Walakini, angalia kwamba Sheol maana yake ni kaburi la kawaida la wanadamu wote waliokufa. Tunapoufahamu uhakika huu juu ya hell kama unavyofundishwa katika Biblia Takatifu, inatusaidia kuifahamu hali ya wanadamu waliokufa.

12. Sheol linaonekana mara ngapi katika Maandiko ya Kiebrania, na ni watu gani waliolitumia neno hili humo?

12 Kwa hiyo, kuanzia na matumizi ya Yakobo ya neno la Kiebrania, “Sheol” linaonekana mara 65 katika vitabu vyote 39 vya Maandiko ya Kiebrania yaliyoongozwa na roho ya Mungu. Neno hilo lilitumiwa na nabii Musa, na Ayubu, na Samweli, Daudi, Sulemani, Isaya, Yeremia (katika Wafalme), Ezekieli, Hosea, Amosi, Yona na Habakuki.

13. Ni maneno gani ya Kiingereza yanayoonyeshwa na Biblia ya Authorized ya Mfalme James kama yanayolingana katika maana, na Mhubiri 9:5, 10 aonyesha n’nini kisichokamatana na “hell”?

13 Watafsiri wa Biblia hawakupatana katika kulitafsiri neno Sheol katika lugha zao. Kwa mfano, Biblia ya Kiingereza iliyohalalishwa na Mfalme James wa Kwanza inatafsiri “Sheol” mara 31 kama “hell,” mara 31 kama “kaburi,” na mara tatu kama “shimo.” Basi itamlazimu mtu ye yote mwenye busara kukubali kwamba katika Maandiko ya Kiebrania yaliyoongozwa na roho ya Mungu maneno “hell,” “kaburi,” na “shimo” yana maana ile ile moja. Na hakuna ukamatano wo wote na moto, kiberiti wala mateso ya milele. Tukitazama katika Biblia Douay Version ya Kiingereza katika Mhubiri 9:5, 10, twasoma: “Walio hai wanajua kwamba watakufa, bali wafu hawajui jambo jingine lo lote. . . . Jambo liwalo lote mkono wako uwezalo kulifanya, lifanye kwa bidii: kwa maana wala kazi, wala kuwaza, wala hekima, wala maarifa, hayatakuwamo katika hell [“inferi,” Kirumi], ambako wewe unaelekea kwa kasi.”

14. (a) Kwa sababu gani Ayubu angeweza kusema alivyosema juu ya hell katika Ayubu 14:13? (b) Yona na Daudi walionyeshaje kwamba wao vile vile waliufahamu uhakika huo?

14 Basi, si ajabu kwamba mzee wa ukoo Ayubu angeweza kusema hivi akiwa katika taabu yake mbaya sana: “Nani atakayenifanyia hili, kwamba wewe unilinde mimi katika hell [“infernus,” Kirumi], na kunificha mimi mpaka hasira yako imepita, na kuniwekea mimi wakati utakaponikumbuka mimi?” (Ayubu 14:13, Douay Version) Mzee wa ukoo Ayubu alijua kwamba Mungu anawakumbuka wale waliomo katika Sheol, katika “hell,” katika infernus. Ayubu aliamini kwamba Mungu angemkumbuka yeye milele kwa sababu ya ukamilifu wake wenye uaminifu kumwelekea Mungu wa kweli. Nabii Yona vile vile aliuamini uhakika huo, kwa maana alipokuwa ndani ya yule samaki mkubwa katika Bahari ya Kati alisema: “Nilimlilia Bwana kwa sababu ya taabu yangu, naye akanisikia: nililia tumboni mwa hell [“inferi,” Kirumi], nawe umeisikia sauti yangu.” (Yona 2:3, Douay) Halafu tena yuko mtunga zaburi Daudi, aliyeandika: “Kwa sababu wewe hutaiacha nafsi yangu katika hell [“infernus,” Kirumi]; wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu.”​—Zab. 15:10, Douay.

“HELL” HAIKUWAKO

15. Ni wakati gani “hell” haikuwako?

15 Sasa, hapa, ndio wakati ufaao kwetu kuuliza, tukiwa na ufahamu ulioondolewa makosa wa mambo kutoka katika Biblia yenyewe, ni wakati gani ambapo “hell” hiyo, infernus, au Sheol, haikuwako? Huu ndio wakati ambapo mwanamume wa kwanza na mwanamke, Adamu na Hawa, walikuwa katika bustani ya Paradiso ya Edeni, karibu miaka 6,000 iliyopita. Juu ya wakati huo wenye furaha twasoma: “Naye Bwana Mungu alikuwa amepanda bustani ya furaha tangu mwanzo; ambamo alimweka mwanamume aliyekuwa ameumba.” Kufuata hapo Mungu alimweka mwanamke wa kwanza humo, kando ya Adamu.​—Mwa. 2:8-23; 1:26-28, Douay.

16. Kwa sababu gani wakati huo “hell” haikuwa imetokea?

16 “Hell” au Sheol wakati huo haikuwako duniani. Hakukuwako kaburi lililokuwa limechimbwa ama na Mungu ama na mwanadamu. Kaburi la kawaida la mwanadamu lililoko leo wakati huo halikuwako. Kwa hiyo hakukuwako haja ya kitu kama hicho, kwa maana Bwana Mungu hakuwa amewaumba wanadamu mwishowe waende ama “hell” (Sheol) ama mbinguni. Yeye alitamani kwa upendo wanadamu waishi milele duniani katikati ya hali za paradiso. Ndiyo sababu alimwambia Adamu hivi, hata mbele ya mkewe Hawa kuumbwa: “Ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, wewe hutakula. Kwa maana katika siku yo yote utakapokula ya huo, wewe utakufa foo.”​—Mwa. 2:17, Douay.

17. (a) Imetupasa tuangalie nini alichokisema Mungu au asichokisema alipokuwa akimwonya Adamu juu ya kutokutii? (b) Maneno ya Mungu katika kumhukumia Adamu kifo yanapatanaje na habari za kuumba, na kwa hiyo nini ambacho kisingeweza kutukia Adamu alipokufa?

17 Ili tusije tukalipita jambo hili la maana, ebu na tuangalie, Bwana Mungu hakumwambia Adamu kwamba, katika siku iwayo yote ambapo angelila tunda lililokatazwa, angekwenda “hell” akataabike milele akijisikia katika mateso ya moto. Alimwonya Adamu kwamba angekufa foo kwa ajili ya kutokutii. Hata Adamu alipokwisha kuufuata mfano wa mkewe na kulila tunda lililokatazwa, Mungu alimwambia Adamu hivi akimhukumia kufa: “Katika jasho la uso wako wewe utakula chakula hata utakapoirudia ardhi, ambayo kwayo ulitwaliwa: maana wewe ni mavumbi, na mavumbini utarudi.” (Mwa. 3:19, Douay) Hii ilikuwa kupatana na masimulizi ya kuumbwa kwa mwanadamu, yanayosema: “Naye Bwana Mungu akafanya mwanamume kutoka kwa matope ya dunia: na akapuliza katika uso wake pumzi ya uhai; naye mwanamume akawa nafsi hai.” (Mwa 2:7, Douay) Mwanamume alipata kuwa nafsi iliyo hai ya kibinadamu alipoumbwa, na kwa hiyo hakuna nafsi iliyoendelea kuishi wala ambayo ingeweza kuteswa milele ikijisikia katika moto na kiberiti.

18. Kama inavyoonyeshwa na habari ya Mwanzo, “hell” ilianza alipokufa nani na kuzikwa?

18 Akiwa anaishi maisha yaliyolaaniwa nje ya paradiso ya furaha kwa karibu miaka 930, Adamu aliishi zaidi ya miaka 800 kufuata kifo cha mwanawe wa pili Habili. Habili mwenye haki, mwenye kumcha Mungu aliuawa na kaka yake mwenye kijicho Kaini. Kwa kuwa hakuna vifo vya wo wote wa watoto wa Adamu na Hawa vinavyotajwa mbele ya hapo, “hell” (infernus, Sheol) ilitokea Habili alipokufa na kuzikwa. Bwana Mungu alimwambia hivi Kaini mwuaji: “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako yanililia mimi kutoka nchini. Nawe sasa umelaaniwa uhame katika nchi, iliyofungua kinywa chake iipokee damu ya ndugu yako mkononi mwako.”​—Mwa. 4:1-11; 5:1-5, NW.

19. Maandiko yanasema nini juu ya Habili kuonyesha kwamba alikwenda “Sheol”, akakumbukwe akiwa humo?

19 Habili alikuwa mwanamume mwenye kumwamini Mungu. Katika Waebrania 11:4 twasoma: “Kwa imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko Kaini; kwa hiyo alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake, na kwa hiyo, ijapokuwa amekufa, angali akinena.” (Tazama vile vile 1 Yohana 3:12.) Yesu Kristo vile vile alimzungumza Habili kama mwenye haki. (Mt. 23:35) Kwa sababu hiyo Bwana Mungu anamkumbuka Habili katika kufa kwake, na kwa hiyo ni kwenye “Sheol,” “hell” au infernus alikokwenda Habili alipokufa na kuzikwa. Yeye angali amelala katika kaburi la kawaida la wanadamu waliokufa. Kifo chake kilikuwa tofauti na kile cha watenda dhambi waliohukumiwa, Adamu na Hawa. Twaweza kuwa na hakika kwamba Mungu atamkumbuka Habili kama vile atakavyomkumbuka mzee wa ukoo Ayubu katika wakati uliowekwa kwa kimungu.​—Ayubu 14:13.

“HELL” KATIKA MAANDIKO YA KIKRISTO YA KIGIRIKI

20. Ni ulizo gani linalotokezwa na mfano wa Yesu wa tajiri na Lazaro juu ya hell, na kulingana na The Jerusalem Bible, ni neno gani lililotumiwa hapa na habari za Luka?

20 Kwa kuwa sasa hivi tumemtaja Yesu Kristo, inafaa kuuliza, Je! Yesu Kristo mwenyewe hakufundisha kwamba kuna moto ulio hakika katika “hell”? Tazama alivyosema katika mfano wake wa tajiri na maskini Lazaro. Yesu alisema: “Naye tajiri akafa: naye akazikwa katika hell [“infernus,” Kirumi]. Naye akiyainua macho yake alipokuwa matesoni, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani pake: Naye akapaza sauti, na kusema: . . . Nateswa katika mwali huu wa moto.” (Luka 16:22-24, Douay) Mfano huu uliandikwa na mwanafunzi Luka katika lugha ya Kigiriki, na kwa hiyo yeye hakulitumia neno la Kiebrania Sheol. Tafsiri ya Biblia ya Jerusalem ya Katoliki inalionyesha neno la Kigiriki linalotumiwa na Luka, kwa maana yasema: “Tajiri naye akafa na kuzikwa. Katika mateso yake katika Hades akainua kichwa.” Ah, ndiyo, neno la Kigiriki Haʹdes linatumiwa hapa. Na je! mna moto katika Ha’des wa kutesea wafu, kama vile The Jerusalem Bible inavyoelekea kuonyesha?

21. Kwa sababu gani neno la Kigiriki Ha’des hapa lina maana moja na Sheol, wala siyo maoni ya Homer juu ya Ha’des?

21 Mbele ya kujibu ulizo hilo, twauliza: Kwa sababu gani neno la Kigiriki Ha’des linalotafsiriwa hapa kama “hell” (infenus) lina maana moja na neno la Kiebrania Sheol? Kwa sababu gani halina maana ya Ha’des inayofundishwa katika hadithi za kipagani za Kigiriki? Ni kwa sababu, kufuata wakati wa mtunga mashairi wa Kigiriki Homer (au mbele ya mwaka wa 700 B.C.E.) kijina cha pekee Ha’des kilikuja kumaanisha si (kuzimu) “mahali pa roho za marehemu” tu lakini vile vile “kaburi” na “kifo.” (Tazama Greek-English Lexicon, ya Liddell na Scott, iliyochapwa kwanza katika mwaka wa 1843, Kitabu cha Kwanza, ukurasa wa 21, safu ya 2, chini ya “Ha’des,” sehemu ya Pili.)

22. Kwa hiyo, wakati Septuagint Version ya Kigiriki inapomtaja Yakobo kama akitumia Ha’des, nayo Ha’des yatajwa kama ilitumiwa na Yesu, n’nini inachomaanisha na isichomaanisha?

22 Kwa hiyo, wakati Wayahudi fulani wa Alexandria, waliozungumza Kigiriki huko Misri, walipoanza kuyatafsiri Maandiko ya Kiebrania yaliyoongozwa na roho ya Mungu katika Kigiriki cha kawaida karibu mwaka wa 280 B.C.E., na kuianza inayoitwa sasa Septuagint Version ya Kigiriki, walilitumia neno Ha’des kulitafsiri neno la Kiebrania Sheol. Kwa hiyo, walipokuwa wakiyatafsiri maneno ya mzee wa ukoo Yakobo katika Mwanzo 37:34; 42:38; 44:29, 31, walionyesha Yakobo alilitumia neno “Ha’des” kumaanisha “kaburi,” wala siyo maoni ya uongo ya “Ha’des” ya Homer. Kwa hiyo, wakati neno “Ha’des” linapoonyeshwa kama likisemwa na Yesu Kristo, maana yake si mahali pa mateso ya moto ya milele.

“JEHANUM”

23, 24. (a) Yesu aliushirikisha moto na neno gani, nalo lilitumika kwa kitu gani kwa maana yenyewe lakini lilikuwa na maana gani ya mfano? (b) Yesu alionyaje juu ya Jehanum kulingana na Mathayo 5:22, 29, 30?

23 Mahali ambapo Yesu Kristo alipashirikisha na moto hapakuwa “Ha’des,” bali Jehanum. Jina hili kwa kweli lina maana ya “Bonde la Hinomu.” Hili, katika maana yake yenyewe, lina maana ya bonde la Hinomu kuelekea kusini na magharibi ya kusini ya Yerusalemu. Katika siku za Yesu hili lilitumiwa kama jaa la takataka la mji, nao moto uliochanganywa na kiberiti ulitumiwa kuimaliza takataka, hata maiti za wahalifu waliofikiriwa kuwa waovu mno kutoweza kuzikwa katika Ha’des, kaburi la kawaida la wanadamu. Katika maana ya mfano, namna ambavyo Yesu aliitumia, Jehanum ilikuwa mfano wa uharibifu kamili wa milele, kufutiliwa mbali kwa mtu milele. Maangamizi! Jina Jehanum linapatikana mara kumi na mbili tu katika Maandiko ya Kikristo ya Kigiriki yaliyoongozwa na roho ya Mungu. Yesu ndiye anayesemwa kama akilitumia neno hili katika Mathayo 5:22, 29, 30. Hapo twasoma (Rotherham’s):

24 “Kila amkasirikiaye ndugu yake atastahili hukumu,​—na mtu awaye yote atakayemwambia ndugu yake, Goigoi wewe! ataistahili baraza kuu; na mtu awaye yote atakayesema, Ewe mwasi! ataistahili jehanum yenye moto. Na ikiwa jicho lako la kuume lakufanya uanguke ling’oe, na kulitupa,​—kwa maana yakufaidi wewe kwamba kimojawapo cha viungo vyako kipotee, wala siyo mwili wako mzima kutupwa katika jehanum. Na ikiwa mkono wako wa kuume wakufanya uanguke ukate, na kuutupa,​—kwa maana yakufaidi wewe kwamba kimojawapo cha viungo vyako kipotee, wala siyo mwili wako mzima uingie katika jehanum.”​—Tazama Marko 9:43-47.

25. Ili kuonyesha kwamba Jehanum yamaanisha uharibifu wa milele, Yesu alisema nini juu ya nafsi katika Mathayo 10:28?

25 Ili kuonyesha kwamba Jehanum yafananisha uharibifu kamili wa milele, Yesu aliwaambia hivi mitume wake kumi na wawili: “Nanyi msiwe na hofu kwa sababu yao wauuao mwili,​—na nafsi hawawezi kuiua. Lakini mwogopeni yeye awezaye kuangamiza vyote viwili nafsi na mwili katika jehanum!” (Mt. 10:28, Rotherham’s) Ikiwa, sasa, kinachoitwa “nafsi” kinaangamizwa, kingewezaje kuteswa milele katika moto na kiberiti kikijisikia? Zamani za kale watesi wa kidini hawakuuchoma mwili wa aliyeitwa “mzushi” juu ya mti milele. Moto haumhifadhi mtu.

26. Katika sehemu zote ambapo neno hili la Kigiriki linapatikana, tafsiri ya Kirumi ya Jerome inatumia neno gani, na ni akina nani wanaohukumiwa kwenda mahali hapa?

26 Tazama Mathayo 18:9; 23:15, 33; Luka 12:5, na Yakobo 3:6 uone sehemu inakopatikana Jehanum. Katika sehemu hizi zote Biblia ya Kirumi ya Jerome inalitumia neno jehanum, siyo infernus. Wale ambao Mungu anahukumia uharibifu wa milele kama unavyofananishwa na Jehanum ni wale ambao, kama vile Shetani Ibilisi na malaika zake wa kishetani, hawasahihiki, wamekwisha kupita kadiri wasiweze kurudishwa kwenye haki. Ndiyo sababu Yesu, katika mfano wake juu ya kondoo na mbuzi, anawaambia wale wenye mfano wa mbuzi: “Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, kuingia katika moto wa milele, aliotayarishiwa ibilisi na malaika zake.”​—Mt. 25:41, Douay.

HAWAFUTILIWI MBALI KATIKA “HELL” MILELE?

27, 28. (a) Ni maono ya nani yenyewe yanayoonyesha kama wale wanaokwenda “hell” wanafutiliwa mbali milele? (b) Katika Zaburi 16:10, je! Daudi alijitaja mwenyewe, naye Petro alisema nini juu ya jambo hili siku ya Pentekoste?

27 Je! hii maana yake ni kwamba wale wanaokwenda “hell,” yaani, “Ha’des” au “Sheol,” hawafutiliwi mbali humo milele, hawabaki humo kwa wakati wote utakaokuja? Lazima iwe hivyo iwapo Biblia Takatifu yaonyesha kwamba mtu fulani alitoka hell (“infernus,” “Ha’des,” “Sheol”), akakae nje milele. Ebu na tukumbuke alivyoandika mtunga zaburi Daudi: “Kwa sababu wewe hutaiacha nafsi yangu katika hell [“infernus,” Kirumi]; wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu.” (Zab. 15:10, Douay; 16:10, Authorized Version) Je! hapa Daudi alikuwa akizungumza juu yake mwenyewe? Mtume wa Kikristo Petro anasema Sivyo. Katika siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 C.E., Petro alitaja zaburi hii ya Daudi na kuitumia kwa anayestahili. Petro alisema:

28 “Kwa sababu wewe hutaiacha nafsi yangu katika “hell” [“infernus,” Kirumi], wala kumtaabisha Mtakatifu wako aone uharibifu. Wewe umenijulisha mimi njia za uzima: wewe utanifanya mwenye furaha tele kwa upendeleo wako. Enyi wanaume, akina ndugu, acheni nizungumze nanyi kwa uhuru juu ya mzee wa ukoo Daudi; kwamba alikufa, akazikwa; nalo kaburi lake li pamoja nasi leo hii. Kwa hiyo basi yeye alikuwa nabii, naye alijua kwamba Mungu amemwapia yeye kwa kiapo, kwamba kutoka katika viuno vyake imempasa mmoja aketi juu ya kiti chake cha enzi. Akitangulia kuona hili, alizungumza juu ya ufufuo wa Kristo. Kwa maana wala hakuachwa katika hell [“infernus,” Kirumi], wala mwili wake haukuona uharibifu. Yesu huyu Mungu amemfufua tena, ambaye kwake sisi sote tu mashahidi.”​—Matendo 2:27-32, Douay.

29. “Imani ya Mitume” inayorudiwa kutajwa na watu wa makanisa yaonyeshaje kama hell ni mahali pa mateso ya milele motoni?

29 Watu wengi ambao wamekuwa washiriki wa makanisa watakumbuka walirudia pamoja kuitaja inayoitwa “Imani ya Mitume,” ambayo katika hiyo walisema: “Namwamini Mungu Baba Mwenyezi, Muumba wa mbingu na nchi, na Yesu Kristo Mwanawe wa pekee aliye Bwana wetu, ambaye . . . alisulibiwa, akafa, akazikwa: akashuka katika hell [“inferna,” Kirumi]; akafufuka siku ya tatu kutoka kwa wafu; akapaa mbinguni, naye sasa aketi mkono wa kuume wa Mungu Baba Mwenyezi.” Hivyo wenye kuirudia Imani hii wameonyesha imani ya kwamba Yesu Kristo ‘alishuka katika hell’. Je! kwa maneno hayo walimaanisha kwamba alishuka kuingia motoni na katika kiberiti chini ya ardhi akatesewe humo milele kwa ajili ya wanadamu? Haiwezekani kwamba walimaanisha hivyo, kwa maana katika maneno yale yale yanayofuata walisema: “akafufuka siku ya tatu kutoka kwa wafu.” Hivyo wao wenyewe, na vile vile mtume Petro, wanakiri kwamba, kwa habari ya Yesu Kristo, “hell” (infernus) siyo mahali wanadamu waliokufa wasipoweza kutoka mara wanapopaingia. Yesu hakuona mateso yo yote humo.

30, 31. (a) Kulingana na Mhubiri 9:5, 10, yalikuwa maono gani ya Kristo alipokuwa katika hell, na kwa hiyo alikuwa kana kwamba anafanya nini? (b) Kwa kuwa Yesu Kristo anaitwa “malimbuko” ya wafu waliomo katika hell, hii yamaanisha nini kwa wale wengine wote waliomo humo?

30 Yesu Kristo alikuwamo “hell” (“Ha’des” au “Sheol”) kwa vipindi vya siku tatu (Nisani 14-16, mwaka wa 33 C.E.). Kama vile Mhubiri 9:5, 10 atuambiavyo, alipokuwa humo hakujua lo lote. Hakupata kazi yo yote, kuwaza, hekima wala maarifa humo. Ajapokuwa alikuwa amekufa kweli kweli, alikuwa kana kwamba amelala, asiyetenda, asiyejua cho chote. Ndiyo sababu mtume wa Kikristo Paulo anaandika hivi juu ya ufufuo wa Kristo kutoka kwa wafu: “Lakini sasa Kristo amefufuka kutoka kwa wafu, malimbuko ya wao wanaolala.” (1 Kor. 15:20, Douay) Basi, kwa kweli ufufuo ulimfaidi Yesu Kristo, aliyekuwa mfu katika hell. Yesu Kristo alikuwa “malimbuko” tu ya wale wanaolala humo wakiwa wamekufa. Mazao yote ya wafu wa kibinadamu yataamshwa na kutolewa katika wakati wa Mungu uliowekwa. Haya ndiyo maoni ya maana katika maneno yaliyoongozwa na roho ya Mungu ya mtume Paulo:

31 “Kwa maana kwa njia ya mwanadamu kifo kilikuja, na kwa njia ya mwanadamu ufufuo wa wafu. Na kama vile katika Adamu wote wanakufa, ndivyo na katika Kristo wote watakavyohuishwa.”​—1 Kor. 15:21, 22, Douay.

32. Kwamba hell ni mahali palipo na ukombozi yaonyeshwa na maneno gani ya Yesu katika Ufunuo 1:17, 18?

32 Kwamba hell (“Ha’des” au “Sheol”) ni mahali ambapo kutoka hapo wafu wote watakombolewa kwa njia ya ufufuo twahakikishiwa na maneno ya Yesu Kristo aliyefufuliwa. Karibu mwaka wa 96 C.E., au miaka 32 Rumi ilipokwisha kuteketezwa kwa moto na Mfalme Nero, Yesu Kristo aliyefufuliwa alimtokea mtume Yohana katika njozi. Njozi hii yaonyeshwa wazi katika kitabu cha mwisho cha Biblia, kinachoitwa Ufunuo, namo humo anamwambia hivi mtume Yohana: “Mimi ndimi wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai, nami nilikuwa nimekufa, nawe tazama mimi naishi milele na milele, nami ninazo funguo za mauti na za hell [“infernus,” Kirumi].”​—Ufu. 1:17, 18, Douay.

33, 34. (a) Nini kinachoonyesha kama itakuwa lazima Yesu Kristo alipwe fedha na jamaa na rafiki mbele ya kuzitumia funguo awakomboe wale waliomo katika mauti na hell? (b) Yesu Kristo mwenyewe alikombolewa kutoka wapi, na kwa sababu gani Mungu alimkabidhi yeye “funguo”?

33 Je! kuwa kwa Yesu Kristo na “funguo za mauti na za hell” ni kwa kusudi la kuwafungia waliokufa katika hell milele? Au je! yeye anapaswa kulipwa fedha kwanza na jamaa au rafiki za waliokufa mbele ya kuzitumia funguo na kuwafungulia wale waliokufa na waliomo katika hell? Lo! namna ambavyo hilo lingekuwa jambo la kichoyo na la kibiashara kwake kuzitumia “funguo za mauti na za hell” kwa njia hiyo!

34 Kwa kuyakataa maoni hayo kabisa, Yesu aliwaambia mitume wake: “Mwana wa Adamu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia, na kuutoa uhai wake kama ukombozi kwa ajili ya wengi.” (Mt. 20:28, Douay) Alipokuwa duniani kama mwanadamu, Yesu Kristo hakutoza hata sarafu moja ya dinari ya fedha kwa ajili ya kumfufua ye yote kati ya wafu aliowafufua. Kusudi la Yesu Kristo aliyefufuliwa la matumizi ya “funguo za mauti na za hell” siyo kuwafungia wafu milele, bali kuwakomboa kwa upendo na kwa hiari. Mungu mwenyewe, aliyemfufua Mwanawe Yesu Kristo kutoka hell, alimkabidhi “funguo” hizo kwa kusudi lilo hilo.

35. (a) Yesu alisema nini juu ya wakati wenye furaha wa kutumia kwake ufunguo wa hell? (b) Kwa sababu gani au ni kwa namna gani kusudi la ufufuo ni lenye faida?

35 Akiutazamia wakati huo wenye furaha, Yesu Kristo aliwaambia Wayahudi: “Kama vile Baba alivyo na uhai ndani yake mwenyewe, ndivyo alivyompa Mwana vile vile kuwa na uhai ndani yake. Naye amempa uwezo wa kuhukumu, kwa maana yeye ndiye Mwana wa Adamu. Msistaajabie haya; kwa maana saa yaja, ambayo wote wale waliomo makaburini wataisikia sauti ya Mwana wa Mungu. Nao waliofanya mema, watatokea kuingia katika ufufuo wa uzima; bali wao waliofanya maovu, kuingia katika ufufuo wa hukumu.” (Yohana 5:26-29, Douay) Kwa wazi ufufuo huo wa wale wote waliomo katika hell ni kwa ajili ya faida yao. Ni wakati tu wo wote waliofufuliwa kutoka hell watakaporudia kufanya maovu kwa makusudi ndipo kufufuliwa kwao kutakapomalizikia katika hukumu ya laana ya uharibifu wa milele. Kwa hiyo kusudi la ufufuo ni lenye faida, faida ya milele ya wafu. Linawafungulia nafasi ya kufurahia uzima wa milele katika taratibu mpya ya Mungu.

36, 37. Nani aliyepewa njozi ya wakati ambapo hell haitakuwako, naye huyu aliisimuliaje tamasha yenyewe?

36 Katika Ufunuo uo huo kwa mtume Yohana, Yesu Kristo aliyefufuliwa alitoa njozi ya wakati ambapo hell haitakuwako. Ni wakati hii taratibu ya mambo ya kale ya kilimwengu itakapokwisha kuharibiwa, na Mungu aumbe mbingu mpya na dunia mpya, yaani, serikali mpya ya kimbinguni na jamii mpya ya kidunia ya kibinadamu. Akiisimulia tamasha ya ajabu, Yohana anaandika:

37 “Nami nikaona kiti kikubwa cha enzi kilicho cheupe, naye mtu mmoja alikuwa amekikalia, ambaye dunia na mbingu ziliukimbia uso wake, wala hapakuonekana mahali kwazo. Nami nikawaona wafu, wakubwa na wadogo, wamesimama mbele za kiti cha enzi, navyo vitabu vilifunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ndicho kitabu cha uzima; nao wafu wakahukumiwa kulingana na mambo hayo yaliyoandikwa katika vitabu vile, kulingana na kazi zao. Na bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake, nayo mauti na hell [“infernus,” Kirumi] vikawafungua wafu wake.”​—Ufu. 20:11-13, Douay.

38. (a) Kwa hiyo hell itaondolewaje, nao Ufunuo unaonyeshaje hili? (b) “Mauti” na uovu vitakomeshwaje?

38 Ah, ndiyo, wakati hell (“Haʹdes” au “Sheol”) itakapokuwa imemfungua mfu wa mwisho aliyemo ndani yake, kwa njia ya ufufuo wa wafu wote ambao Yesu Kristo aliutoa uhai wake wa kibinadamu kwa ajili yao kama ukombozi, ndipo kutakapokuwa hakuna hell tena. Kuizunguka dunia yote, wakaaji hawataona kaburi hata moja wala alama yo yote ya kaburi. Kaburi la kawaida la wanadamu litakuwa limekwisha kuharibiwa milele. Ndiyo sababu Ufunuo 20:14, 15, Douay, unaendelea kusema: “Nayo hell [“infernus,” Kirumi] na mauti vikatupwa katika kiziwa cha moto. Hii ndiyo mauti ya pili. Na mtu awaye yote asiyeonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika kiziwa cha moto.” Lo! hiyo itakuwa siku ya hukumu yenye utukufu wa namna gani! Hell itakomeshwa kabisa. Kifo ambacho wanadamu wote wamekirithi kutoka kwa Adamu na Hawa wenye dhambi kitauawa, kitakoma kwa sababu ya kuletwa kwa wanadamu wote watiifu kwenye ukamilifu wa uzima wa kibinadamu katika paradiso ya furaha iliyorudishwa. Kutenda maovu kutakomeshwa kwa kuharibiwa kwa wote watakaogeuka kuwa waovu kwa makusudi na ambao lazima wapate adhabu ya mauti ya pili.

[Ramani katika ukurasa wa 178]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Jehanum au bonde la Hinomu ilikuwa jaa la takataka la mji nayo ikawa mfano wa uharibifu wa milele

MAP OF FIRST-CENTURY JERUSALEM

TEMPLE AREA

VALLEY OF HINNOM

(GEHENNA)

RAMANI YA YERUSALEMU WA KARNE YA KWANZA (Map of First-Century Jerusalem)

ENEO LA HEKALU (Temple Area)

BONDE LA HINOMU (Valley of Hinnom)

(JEHANUM)-(Gehenna)

[Picha katika ukurasa wa 174]

Mtunga mashairi Mwitaliano Dante aliifananisha “Inferno” au “hell” kama mahali ambapo wanadamu walitaabikia kufuata kifo cha mwili. Je! Dante alisema kweli?

[Picha katika ukurasa wa 177]

Mungu hakusema kwamba iwapo Adamu angelila tunda lililokatazwa angekwenda “hell” yenye moto bali kwamba angekufa

[Picha katika ukurasa wa 181]

Ufufuo utawafungulia wafu waliofufuliwa nafasi ya kufurahia uzima wa milele. Wakati “hell” itakapokuwa imemtoa wa mwisho aliyemo ndani yake, wakaaji wa dunia hawataona mahali pa kuzikia wafu tena, kwa maana “hell” yenyewe itakomeshwa kabisa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki