Mpinga-Kristo
Maana: Neno mpinga-Kristo lamaanisha kuwa dhidi au badala ya Kristo. Neno hilo linahusu wote wanaokana yale ambayo Biblia inasema kumhusu Yesu Kristo, wote wanaoupinga Ufalme wake, na wote wanaowatesa wafuasi wake. Pia linatia ndani watu mmoja mmoja, mashirika, na mataifa ambayo kwa uwongo yanadai kumwakilisha Kristo au yanayojihesabia isivyofaa cheo cha Masihi.
Je, Biblia inasema kwamba kuna mpinga-Kristo mmoja tu?
1 Yoh. 2:18: “Watoto wachanga, ni saa ya mwisho, na, kama vile ambavyo mmesikia kwamba mpinga-Kristo anakuja, hata sasa kumekuwa na wapinga-Kristo wengi; uhakika ambao kutokana nao tunajua kwamba ni saa ya mwisho.”
2 Yoh. 7: “Wadanganyifu wengi wametokea katika ulimwengu, watu ambao hawamkiri Yesu Kristo kuwa alikuja katika mwili. Hao ndio yule mdanganyifu na mpinga-Kristo.” (Ona kwamba “wapinga-Kristo wengi” katika 1 Yohana 2:18 wanatajwa hapa kwa ujumla kuwa ndiye “mpinga-Kristo.”)
Je, mpinga-Kristo atakuja wakati fulani ujao?
1 Yoh. 4:3: “Kila neno lililoongozwa na roho ambalo halimkiri Yesu halitokani na Mungu. Zaidi ya hayo, ambalo mmesikia kwamba linakuja, na sasa tayari limo ulimwenguni.” (Maneno hayo yaliandikwa karibu na mwisho wa karne ya kwanza W.K.)
1 Yoh. 2:18: “Hata sasa kumekuwa na wapinga-Kristo wengi; uhakika ambao kutokana nao tunajua kwamba ni saa ya mwisho.” (Kwa kusema “saa ya mwisho” inaonekana Yohana alimaanisha mwisho wa kipindi cha mitume. Wale mitume wengine walikuwa wamekufa, na Yohana mwenyewe alikuwa mzee sana.)
Baadhi ya wale wanaotambulishwa kuwa mpinga-Kristo—
Watu wanaokana kwamba kwa kweli Yesu ndiye Masihi
1 Yoh. 2:22: “Ni nani aliye mwongo kama si yule anayekana kwamba Yesu ndiye Kristo [au, Masihi, mtiwa-mafuta]? Huyo ndiye mpinga-Kristo.”
Wote wanaokana kwamba Yesu ndiye Mwana wa pekee wa Mungu
1 Yoh. 2:22: “Huyo ndiye mpinga-Kristo, yeye anayemkana Baba na Mwana.”
Linganisha na Yohana 10:36; Luka 9:35.
Waasi-imani
1 Yoh. 2:18, 19: “Kumekuwa na wapinga-Kristo wengi . . . Wao waliondoka kwetu, lakini hawakuwa wa namna yetu.”
Wale wanaowapinga wafuasi wa kweli wa Kristo
Yoh. 15:20, 21: “Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia . . . Lakini watawatendea mambo yote haya kwa ajili ya jina langu.”
Watu mmoja-mmoja na mataifa yanayompinga Kristo akiwa Mfalme au ambayo yanadai kwa uwongo kuwa na cheo cha Kimasihi
Zab. 2:2: “Wafalme wa dunia wanachukua msimamo wao nao maofisa wakuu wamejikusanya pamoja kama mtu mmoja dhidi ya Yehova na dhidi ya mtiwa-mafuta [Kristo, au Masihi] wake.”
Ona pia Ufunuo 17:3, 12-14; 19:11-21.
Mt. 24:24: “Makristo wa uwongo na manabii wa uwongo watatokea na kutoa ishara kubwa na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale waliochaguliwa.”