Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbq makala 87
  • Mpinga-Kristo Ni Nani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mpinga-Kristo Ni Nani?
  • Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jibu la Biblia
  • Jinsi ya kuwatambua wapinga-Kristo
  • Mpinga-Kristo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Ni Nani Aliye Mpinga-Kristo?
    Amkeni!—2001
  • Mpinga Kristo ni Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Mpinga-Kristo Anafunuliwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
Maswali ya Biblia Yajibiwa
ijwbq makala 87
Mwinjilisti akihubiri kwenye televisheni

Mpinga-Kristo Ni Nani?

Jibu la Biblia

Mpinga-Kristo si mtu mmoja au shirika moja tu, kwa sababu Biblia inasema kwamba kuna “wapinga-Kristo wengi.” (1 Yohana 2:18) Neno “mpinga-Kristo,” linalotokana na neno ya Kigiriki linalomaanisha “dhidi ya (au badala ya) Kristo,” linafafanua mtu yeyote anayefanya mambo yafuatayo:

  • Anakataa kwamba Yesu ndiye Kristo (Masihi) au anakataa kwamba yeye ni Mwana wa Mungu.​—1 Yohana 2:​22.

  • Anampinga Kristo, Mtiwa-Mafuta wa Mungu.​—Zaburi 2:​1, 2; Luka 11:23.

  • Anajifanya kuwa Kristo.​—Mathayo 24:24.

  • Anawatesa wafuasi wa Kristo, kwa kuwa Yesu huona mambo wanayotendewa kana kwamba ni yeye anayetendewa.​—Matendo 9:5.

  • Anadai kwa uwongo kuwa Mkristo huku akitenda matendo ya uasi-sheria au ya udanganyifu.​—Mathayo 7:​22, 23; 2 Wakorintho 11:13.

Mbali na kusema tu kwamba watu mmoja-mmoja wanaotenda mambo hayo ni wapinga-Kristo, Biblia huwarejelea pia kwa ujumla kuwa yule “mpinga-Kristo.” (2 Yohana 7) Mpinga-Kristo alionekana kwa mara ya kwanza wakati wa mitume naye bado anatenda. Unabii wa Biblia ulitabiri kuhusu jambo hilo.​—1 Yohana 4:3.

Jinsi ya kuwatambua wapinga-Kristo

  • Wanaeneza mawazo ya uwongo kumhusu Yesu. (Mathayo 24:​9, 11) Kwa mfano, wale wanaofundisha Utatu au wanaosema kwamba Yesu ndiye Mungu Mweza-Yote wanapinga mafundisho ya Yesu, kwa sababu alisema hivi: “Baba ni mkuu kuliko mimi.”​—Yohana 14:28.

  • Wapinga-Kristo hawakubaliani na kile Yesu alisema kuhusu utendaji wa Ufalme wa Mungu. Kwa mfano, viongozi fulani wa kidini husema kwamba Kristo anatenda kupitia kwa serikali za kibinadamu. Hata hivyo, fundisho hilo linapingana na alichosema Yesu kwamba: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.”​—Yohana 18:36.

  • Wanasema kwamba Yesu ni Bwana wao, lakini hawatii amri zake, kutia ndani amri ya kuhubiri habari njema ya Ufalme.​—Mathayo 28:19, 20; Luka 6:​46; Matendo 10:42.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki