Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rs uku. 233-uku. 238
  • Ngono

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ngono
  • Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mtu Akisema—
  • Maoni Yako Juu ya Ngono—Yanafanyiza Tofauti Gani?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Kuendelea Kuwa na Maoni ya Mungu Juu ya Ngono
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Maswali Kumi Kuhusu Ngono Yajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ngono Kabla ya Ndoa
    Amkeni!—2013
Pata Habari Zaidi
Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
rs uku. 233-uku. 238

Ngono

Maana: Tabia ya viumbe wa duniani ambayo ni njia ya kuzaana kutokana na wazazi wawili. Tofauti kati ya jinsia ya kiume na kike huleta mabadiliko mengi katika maisha ya wanadamu. Kwa kuwa Mungu mwenyewe ndiye Chanzo cha uhai na kwa kuwa wanadamu walikusudiwa waonyeshe sifa zake, uwezo wa kupitisha uhai kwa mahusiano ya ngono unapaswa uheshimiwe sana.

Je, Biblia inafundisha kwamba mahusiano ya ngono ni dhambi?

Mwa. 1:28: “Mungu akawabariki [Adamu na Hawa] na Mungu akawaambia: ‘Zaeni, muwe wengi, mjaze dunia.’” (Ili kutimiza amri hii ya Mungu, ingekuwa lazima wawe na mahusiano ya ngono, sivyo? Kufanya hivyo hakungekuwa dhambi bali kungepatana na kusudi la Mungu la kuijaza dunia watu. Watu fulani wamefikiri kwamba lile ‘tunda lililokatazwa’ katika Edeni lilimaanisha kwamba labda Mungu aliwazuia au hata kuwakataza Adamu na Hawa wasiwe na mahusiano ya ngono. Lakini hilo linapingana na amri ya Mungu iliyonukuliwa juu. Pia linapingana na uhakika wa kwamba, ingawa Adamu na Hawa walikula lile tunda lililokatazwa katika Edeni, mtajo wa kwanza wa kufanya kwao ngono ulikuwa baada ya kufukuzwa kutoka humo.—Mwa. 2:17; 3:17, 23; 4:1.)

Mwa. 9:1: “Mungu akambariki Noa na wanawe, akawaambia: ‘Zaeni, muwe wengi, mjaze dunia.’” (Baraka hii ya ziada, pamoja na kurudiwa kwa amri ya Mungu ya kuzaa, ilitolewa baada ya ile Gharika duniani katika siku za Noa. Maoni ya Mungu kuhusu mahusiano halali ya ngono hayakuwa yamebadilika.)

1 Kor. 7:2-5: “Kwa sababu ya kuenea kwa uasherati, kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe. Mume na ampe mke wake haki yake; lakini mke pia na amfanyie vivyo hivyo mume wake. . . . Msiwe mkinyimana haki hiyo, ila kwa makubaliano kwa wakati uliowekwa, . . . ili Shetani asiendelee kuwajaribu kwa sababu ya ninyi kukosa kujizuia.” (Jambo ambalo linaonyeshwa kuwa ni kosa ni uasherati, lakini si mahusiano ya ngono halali kati ya mume na mke.)

Je, ni makosa kuwa na mahusiano ya ngono kabla ya ndoa?

1 The. 4:3-8: “Haya ndiyo mapenzi ya Mungu . . . kwamba mjiepushe na uasherati; kwamba kila mmoja wenu ajue jinsi ya kukiweza chombo chake mwenyewe katika utakaso na heshima, si katika hamu yenye tamaa ya ngono kama ile waliyo nayo pia mataifa wale wasiomjua Mungu; kwamba yeyote asifikie hatua ya kudhuru na kuziingilia haki za ndugu yake katika jambo hilo, kwa sababu Yehova ndiye anayelipiza adhabu kwa ajili ya mambo yote haya, kama vile tulivyowaambia ninyi kimbele na pia tukawapa ushahidi kamili. Kwa maana Mungu alituita sisi bila kuruhusu nafasi ya uchafu, bali kuhusiana na utakaso. Kwa hiyo, basi, mtu anayepuuza hampuuzi mwanadamu, bali Mungu, anayeitia roho yake takatifu ndani yenu.” (Neno la Kigiriki por·neiʹa, lililotafsiriwa “uasherati,” linamaanisha tendo la ngono kati ya watu ambao hawajaoana, pia mahusiano ya ngono nje ya ndoa kwa watu waliooana.)

Efe. 5:5: “Hakuna mwasherati au mtu asiye safi au mtu mwenye pupa—maana yake ni kuwa mwabudu-sanamu—aliye na urithi wowote katika ufalme wa Kristo na wa Mungu.” (Hilo halimaanishi kwamba yeyote ambaye zamani alikuwa mwasherati hawezi kupata baraka za Ufalme wa Mungu, lakini ni lazima aache maisha hayo ili apate kibali cha Mungu. Ona 1 Wakorintho 6:9-11.)

Je, Biblia inakubali kuishi pamoja kama mume na mke bila kuoana kisheria?

Ona ukurasa wa 226-230, chini ya kichwa “Ndoa.”

Biblia inasema nini kuhusu ngono kati ya watu wa jinsia moja?

Rom. 1:24-27: “Kwa kupatana na tamaa za mioyo yao, Mungu aliwaacha katika uchafu, ili miili yao ivunjiwe heshima kati yao . . . Mungu aliwaacha katika hamu za ngono yenye kufedhehesha, kwa maana wanawake wao walibadili matumizi yao wenyewe ya asili kuwa yale yaliyo kinyume cha asili; na vivyo hivyo pia hata wanaume waliacha matumizi ya asili ya mwanamke na kuwakiana tamaa kali katika uchu wao kuelekeana wao wenyewe, wanaume kwa wanaume, wakitenda mambo machafu na kupokea ndani yao wenyewe malipo kamili, yaliyostahili kosa lao.”

1 Tim. 1:9-11: “Sheria huwekwa, si kwa ajili ya mtu mwadilifu, bali kwa ajili ya watu wenye kuasi sheria na watundu, wasiomwogopa Mungu na watenda-dhambi, . . . waasherati, wanaume wanaolala na wanaume, . . . na jambo lingine lolote linalopinga fundisho lenye afya kulingana na habari njema yenye utukufu ya Mungu mwenye furaha.” (Linganisha na Mambo ya Walawi 20:13.)

Yuda 7: “Sodoma na Gomora na majiji yaliyoyazunguka, baada ya hayo . . . kwenda kufuatilia mwili kwa ajili ya matumizi yasiyo ya asili, . . . yamewekwa mbele yetu kuwa kielelezo cha kuonya kwa kupatwa na adhabu ya hukumu ya moto wa milele.” (Jina Sodoma ndilo msingi wa neno la Kiingereza “sodomy,” ambalo kwa kawaida humaanisha tendo la ngono kati ya watu wa jinsia moja. Linganisha na Mwanzo 19:4, 5, 24, 25.)

Wakristo wa kweli wanawaonaje wale ambao wamekuwa na zoea la kufanya ngono na watu wa jinsia moja?

1 Kor. 6:9-11: “Wala waasherati, wala waabudu-sanamu, wala wazinzi, wala wanaume wanaowekwa kwa ajili ya makusudi yasiyo ya asili, wala wanaume wanaolala na wanaume . . . hawataurithi ufalme wa Mungu. Na bado wengine wenu mlikuwa hivyo. Lakini mmeoshwa mkawa safi, lakini mmetakaswa, lakini mmetangazwa kuwa waadilifu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo na kwa roho ya Mungu wetu.” (Bila kujali matendo hayo ya zamani, ikiwa sasa watu wanayaacha matendo yao machafu ya zamani, wafuate viwango vya uadilifu vya Yehova, na kuwa na imani katika uandalizi wake wa msamaha wa dhambi kupitia Kristo, wanaweza kupata msimamo safi mbele za Mungu. Baada ya kujirekebisha, wanaweza kukaribishwa katika kutaniko la Kikristo.)

Wakristo wa kweli wanajua kwamba watu ambao kweli wanataka kumpendeza Yehova wanaweza kuzishinda hata tamaa mbaya zenye nguvu, kutia ndani zile ambazo huenda zikawa za kurithiwa au zile zinazohusisha visababishi vya kimwili au vya kimazingira. Watu fulani kwa asili wanakasirika upesi. Labda zamani walikuwa wepesi kukasirika; lakini kuyajua mapenzi ya Mungu, tamaa ya kutaka kumpendeza, na msaada wa roho yake huwawezesha kujizuia. Huenda mtu akawa mlevi, lakini, akiwa na kichocheo kinachofaa, anaweza kuacha kunywa na hivyo aepuke kuwa mlevi. Vivyo hivyo, huenda mtu akahisi kuvutiwa sana na watu wa jinsia yake, lakini akitii shauri la Neno la Mungu, anaweza kubaki safi bila kufanya ngono na watu wa jinsia yake. (Ona Waefeso 4:17-24.) Yehova haturuhusu tuendelee kufikiri kwamba mwenendo mbaya ni sawa tu; kwa fadhili lakini kwa uthabiti yeye hutuonya juu ya matokeo naye huwapa msaada mwingi wale wanaotaka ‘kuvua utu wa zamani pamoja na mazoea yake, na kujivika utu mpya.’—Kol. 3:9, 10.

Je, labda maoni ya Biblia kuhusu ngono yamepitwa na wakati nayo yanawazuia watu bure?

1 The. 4:3-8: “Haya ndiyo mapenzi ya Mungu . . . kwamba mjiepushe na uasherati . . . Kwa hiyo, basi, mtu anayepuuza hampuuzi mwanadamu, bali Mungu, anayeitia roho yake takatifu ndani yenu.” (Maoni ya Biblia kuhusu ngono si jambo tu ambalo lilisitawishwa na wanadamu fulani walioishi miaka mingi iliyopita. Yanatokana na Muumba wa wanadamu; yanaonyesha wazi jambo linalotakiwa ili kupata kibali chake; pia huandaa miongozo inayosaidia familia kuwa thabiti na safi, na kuwa na mahusiano yenye furaha nje ya familia. Wale wanaofuata shauri hilo wanajilinda wenyewe wasipatwe na madhara makubwa moyoni na magonjwa mabaya yanayotokana na mwenendo usio wa adili. Shauri la Biblia ni la kisasa kabisa katika kutimiza mahitaji ya wale wanaotaka kuwa na dhamiri safi mbele za Mungu na kuishi bila kukata tamaa.)

Mtu Akisema—

‘Mna maoni gani kuhusu ngono kati ya watu wa jinsia moja?’

Unaweza kujibu hivi: ‘Ni maoni yanayosemwa katika Biblia. Ninaamini kwamba yale ambayo inasema ni muhimu zaidi kuliko maoni ya mwanadamu yeyote, kwa sababu Biblia hutupa mawazo ya Muumba wa wanadamu. (1 Kor. 6:9-11) Utaona kwamba baadhi ya watu hawa waliokuja kuwa Wakristo, hapo zamani walifanya ngono na watu wa jinsia yao. Lakini kwa sababu ya kumpenda Mungu, na kwa msaada wa roho yake, walibadilika.’

Au unaweza kusema: ‘Ninapojibu hilo, ninaweza kusema nimeona kwamba watu wengi ambao hawaoni ngono kati ya watu wa jinsia moja kuwa jambo la aibu hawakubali Biblia kuwa ni Neno la Mungu. Je, una maoni gani kuhusu Biblia?’ Mtu huyo akidai kwamba anaiamini Biblia, unaweza kuongezea: ‘Ngono kati ya watu wa jinsia moja si suala jipya. Biblia inasema maoni ya Yehova Mungu yasiyobadilika kwa kutumia maneno yaliyo wazi sana. (Labda tumia habari katika ukurasa wa 235, 236.)’ Mtu huyo akionyesha shaka juu ya kuwako kwa Mungu au juu ya Biblia, unaweza kuongezea: ‘Ikiwa hakuna Mungu, ni jambo linalopatana na akili kwamba hatuwezi kuwajibika kwake nasi tunaweza kuishi kama tunavyopenda. Kwa hiyo swali ni hili, Je, kuna Mungu na je, mimi nipo kwa sababu aliniumba [pia, unaweza kusema, Je, Biblia iliongozwa na roho ya Mungu]? (Tumia habari kutoka ukurasa wa 215-221 au 32-42.)’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki