Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gt sura 39
  • Wenye Kiburi na Wenye Udhalili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wenye Kiburi na Wenye Udhalili
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Habari Zinazolingana
  • Wenye Kiburi na Wenye Udhalili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Ole kwa Kizazi Kisichotii
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • ‘Kupata Burudisho la Nafsi Zenu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Mathayo 11:28-30—“Njoni Kwangu, . . . Nami Nitawapumzisha”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
Pata Habari Zaidi
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
gt sura 39

Sura 39

Wenye Kiburi na Wenye Udhalili

BAADA ya kutaja sifa za wema za Yohana Mbatizaji, Yesu ageuza fikira kwenye watu wenye kiburi na vigeu-geu wanaomzunguka. “Kizazi hiki,” yeye anatangaza, “kinafanana na watoto wachanga wanaokaa mahali penye masoko, wanaopiga kelele kuambia wenzao, wakisema, ‘Sisi tuliwapigia filimbi nyinyi, lakini nyinyi hamkucheza dansi; sisi tuliomboleza, lakini nyinyi hamkujipiga-piga wenyewe kwa huzuni.’”

Yesu amaanisha nini? Yeye aeleza: “Yohana alikuja hali wala hanywi, hata hivyo watu wasema, ‘Yeye ana roho mwovu’; Mwana wa binadamu alikuja akila na kunywa, na bado watu wasema, ‘Tazama! Mwanamume mlafi na mzoevu wa kunywa divai, rafiki ya wakusanya kodi na watenda dhambi.’”

Haiwezekani kuridhisha watu. Hakuna jambo linalowafurahisha. Yohana ameishi maisha ya kuepuka mno vitu kwa kujinyima akiwa Mnaziri, kwa kupatana na tangazo la yule malaika, “Ni lazima asinywe hata kidogo divai wala kinywaji chochote kikali.” Na hata hivyo watu wasema yeye ana roho mwovu. Kwa upande mwingine, Yesu anaishi kama watu wale wengine, bila kuzoea kujiepusha mno na vitu, naye ashtakiwa kuwa afanya mambo kupita kiasi.

Watu hao ni wagumu kufurahisha kama nini! Wao ni kama wenzi wa kucheza nao, baadhi yao wakataa kuitikia kwa kucheza dansi wakati watoto wale wengine wanapopiga filimbi au wakataa kuitikia kwa huzuni wakati wenzao wanapoomboleza. Hata hivyo, Yesu anasema: “Hekima inathibitishwa kuwa adilifu kwa kazi zayo.” Ndiyo, wonyesho wa wazi—zile kazi—zinafanya iwe wazi kwamba mashtaka yaliyofanywa dhidi ya Yohana na Yesu ni ya bandia.

Yesu anaendelea kuonyesha kwamba ina masuto yasiyo na kifani ile miji mitatu ya Korazini, Bethsaida, na Kapernaumu, ambako yeye amefanya kadiri iliyo kubwa zaidi ya kazi zake za ajabu. Kama yeye angalifanya kazi hizo katika majiji ya Kifoinike ya Tiro na Sidoni, Yesu anasema majiji hayo yangalitubu katika mavazi ya gunia na majivu. Akilaumu vikali Kapernaumu, jiji ambalo inaonekana ndilo linakuwa kituo kikubwa cha makao yake katika pindi ya huduma yake, Yesu anatangaza hivi: “Litakuwa jambo lenye kuvumilika zaidi kwa nchi ya Sodoma katika Siku ya Hukumu kuliko kwenu nyinyi.”

Halafu Yesu anamsifu peupe Baba yake wa kimbingu. Anavutwa moyoni kufanya hivyo kwa sababu Mungu anaficha kweli za kiroho zenye thamani kubwa zisionwe na wenye hekima na wenye maarifa lakini anawafunulia walio dhalili, watu walio kama watoto wachanga, mambo hayo yaliyo mazuri ajabu.

Mwisho, Yesu atoa mwaliko huu unaovuta watu: “Njoni kwangu, nyinyi nyote mnaomenyeka na kulemewa na mizigo, nami nitawaburudisha nyinyi. Bebeni nira yangu na kujifunza kwangu, kwa maana mimi ni mwenye tabia pole na dhalili katika moyo, na nyinyi mtapata burudisho la nafsi zenu. Kwa maana nira yangu ni ya fadhili na mzigo wangu ni mwepesi.”

Yesu anatoaje burudisho? Anafanya hivyo kwa kuandaa uhuru wa kuondolewa katika mapokeo yenye kutumikisha ambayo viongozi wa kidini wametumia kulemeza watu, kutia ndani, kwa kielelezo, kawaida zuifu za kushika Sabato. Yeye awaonyesha pia njia ya kupata kitulizo wale wanaohisi uzito unaowalemea sana na kutawalwa na wakuu wa kisiasa na wale wanaohisi uzito wa dhambi zao kupitia dhamiri inayosumbuliwa. Awafunulia hao wenye kusumbuka jinsi dhambi zao zinavyoweza kusamehewa na jinsi wanavyoweza kufurahia uhusiano wenye thamani kubwa pamoja na Mungu.

Nira yenye fadhili ambayo Yesu awatolea ni moja ya wakfu kamili kwa Mungu, kuweza kutumikia Baba yetu wa kimbingu mwenye huruma na rehema. Na mzigo mwepesi ambao Yesu awatolea wale wanaomjia yeye ni ule wa kutii matakwa ya Mungu ya kupatia uzima, amri Zake ambazo zimeandikwa katika Biblia. Na kuzitii si mzigo wenye kulemea hata kidogo. Mathayo 11:16-30; Luka 1:15; 7:31-35; 1 Yohana 5:3, NW.

▪ Watu wenye kiburi na vigeu-geu wa kizazi cha Yesu wakoje kama watoto?

▪ Kwa nini Yesu asukumwa asifu Baba yake wa kimbingu?

▪ Ni kwa njia zipi watu wanalemewa, na ni kitulizo gani anachowatolea Yesu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki