Sura 59
Kwa Kweli Yesu Ni Nani?
WAKATI ile mashua yenye kuchukua Yesu na wanafunzi wake inapoingia ufuoni kule Bethsaida, watu wamletea mwanamume kipofu na kumwomba kwamba yeye amguse na kumponya. Yesu aongoza mwanamume huyo kwa mkono nje ya kijiji kile na, baada ya kutema mate juu ya macho yake, anauliza: “Je! wewe unaona kitu chochote?”
“Mimi naona watu,” ajibu mwanamume yule, “kwa sababu mimi naona kile ambacho kinaonekana kana kwamba ni miti, lakini wanatembea huku na huku.” Akiweka mikono yake juu ya macho ya mwanamume yule, Yesu amrudishia uwezo wake wa kuona hivi kwamba anaona waziwazi. Ndipo Yesu anapomwambia mwanamume yule aende nyumbani akimwagiza kwamba asiingie jijini.
Sasa Yesu anaondoka pamoja na wanafunzi wake kwenda kwenye vijiji cha Kaisaria Filipi, katika kaskazini ya mbali zaidi ya Palestina. Huo ni mpando mrefu, unaochukua karibu kilometa 48 kufika pale mahali pazuri ulipo Kaisaria Filipi, zapata meta 350 juu ya usawa wa bahari. Labda kisafari hicho kinachukua siku kadhaa.
Njiani, Yesu anaenda kando yeye mwenyewe kusali. Ni miezi tisa au kumi tu ambayo inabaki kabla ya kifo chake, na yeye anahangaikia wanafunzi wake. Tayari wengi wamekwisha acha kufuata yeye. Inaonekana wengine wamevurugika na kutamaushwa kwa sababu yeye alikataa jitihada za watu za kumfanya mfalme na kwa sababu yeye hakuandaa ishara kutoka mbinguni kuthibitisha umaliki wake, wakati alipotolewa mwito wa ushindani na adui zake. Mitume wake wanaamini nini juu ya utambulisho wake? Wakati wao wanapokuja mahali ambapo yeye anasali, Yesu anauliza: “Makutano ya watu wanasema kwamba mimi ni nani?”
“Watu fulani wanasema Yohana yule Mbatizaji,” wao wanajibu, “wengine Eliya, bado wengine Yeremia au mmoja wa wale manabii.” Ndiyo, watu wanafikiri Yesu ni mmoja wa wanaume hawa ambaye ameinuliwa kutoka kwa wafu!
“Ingawa hivyo, nyinyi mnasema mimi ni nani?” Yesu anauliza.
Petro anajibu kwa haraka: “Wewe ndiwe Kristo, yule Mwana wa Mungu anayeishi.”
Baada ya kukubali jibu la Petro, Yesu anasema: “Mimi nakwaambia, Wewe ni Petro, na juu ya tungamo-mwamba hili mimi nitajenga kundi langu, na malango ya Hadesi hayatalishinda nguvu.” Hapa kwanza Yesu anatangaza kwamba yeye atajenga kundi na kwamba hata kifo hakitazuia washiriki walo wakiwa mateka baada ya mwendo wao wa uaminifu duniani. Ndipo yeye anaambia Petro: “Mimi nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni.”
Hivyo Yesu anafunua kwamba Petro atapokea mapendeleo ya pekee. La, Petro hapewi mahali pa kwanza miongoni mwa wale mitume, wala yeye hafanywi ule msingi wa kundi. Yesu mwenyewe ndiye Tungamo-Mwamba ambao juu yao kundi lake litajengwa. Lakini ni kama kwamba Petro anapewa funguo tatu za kufungulia vikundi vya watu ile fursa ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni.
Petro angetumia ufunguo wa kwanza kwenye Pentekoste 33 W.K. kuonyesha Wayahudi wenye kutubu mambo ambayo lazima wafanye ili kuokolewa. Yeye angetumia ule wa pili muda mfupi baadaye kufungulia Wasamaria wenye kuamini ile nafasi ya kuingia katika Ufalme wa Mungu. Ndipo, katika 36 W.K. yeye angetumia ufunguo wa tatu kufungulia Mataifa wasiotahiriwa, Kornelio na rafiki zake, fursa iyo hiyo.
Yesu anaendelea na mazungumzo yake pamoja na mitume wake. Yeye anawatamausha kwa kuwaambia juu ya mateso na kifo ambacho yeye ataelekeana nacho karibuni katika Yerusalemu. Kwa kukosa kufahamu kwamba Yesu atafufuliwa kwenye uhai wa kimbingu, Petro anachukua Yesu kwenda kando. “Uwe mwenye fadhili kwako mwenyewe, Bwana,” yeye anasema. “Wewe hutakuwa na tukio baya hili hata kidogo.” Akigeuza mgongo wake, Yesu anajibu: “Nenda nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kwazo kwangu mimi, kwa sababu wewe unafikiri, si fikira za Mungu, bali zile za wanadamu.”
Ni wazi kwamba, watu wengine zaidi ya wale mitume wanasafiri pamoja na Yesu, kwa hiyo sasa yeye anawaita hao waje kwake naye anawaeleza kwamba halitakuwa jambo jepesi kuwa wafuasi wake. “Ikiwa mmoja yeyote anataka kunifuata mimi,” yeye asema, “acha huyo akatae uenyeji wake mwenyewe na kuchukua mti wake wa mateso naye aendelee kunifuata. Kwa maana awaye yote ambaye anataka kuokoa nafsi yake ataipoteza; lakini awaye yote ambaye anapoteza nafsi yake kwa ajili yangu mimi na zile habari njema ataiokoa.”
Ndiyo, ikiwa wao wanataka kuwa na upendeleo wake, lazima wafuasi wa Yesu wawe wenye moyo mkuu na wenye kujidhabihu. Yeye anasimulia hivi: “Kwa maana awaye yote ambaye anakuwa mwenye aibu juu yangu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki chenye uzinzi na chenye dhambi, yule Mwana wa binadamu atakuwa mwenye aibu pia juu yake wakati yeye awasilipo katika utukufu wa Baba yake pamoja na wale malaika watakatifu.” Marko 8:22-38; Mathayo 16:13-28; Luka 9:18-27, NW.
▪ Kwa nini Yesu anahangaikia wanafunzi wake?
▪ Watu wana maoni gani juu ya utambulisho wa Yesu?
▪ Petro apewa funguo gani, nazo zapasa kutumiwaje?
▪ Petro apokea sahihisho gani, na kwa nini?