Maisha na Huduma ya Yesu
Kwa Kweli Yesu Ni Nani?
WAKATI ile mashua yenye kuchukua Yesu na wanafunzi wake inapoingia ufuoni kule Bethsaida, watu wanaleta mwanamume kipofu kwake na kuomba kwamba yeye aguse mwanamume huyo na kumponya. Yesu anaongoza mwanamume huyo kwa mkono nje ya kijiji kile na, baada ya kutema mate juu ya macho yake, anauliza: “Je! wewe unaona kitu cho chote?”
“Mimi naona wanaume,” anajibu mwanamume yule, “kwa sababu mimi naona kwa makini kile ambacho kinaonekana kana kwamba ni miti, lakini hiyo inatembea huku na huku.” Akiweka mikono yake juu ya macho ya mwanamume yule, Yesu anarudisha mwono wake hivi kwamba yeye anaona waziwazi. Ndipo Yesu anapoambia mwanamume yule aende nyumbani kwa agizo la kutoingia ndani ya mji.
Sasa Yesu anaondoka pamoja na wanafunzi wake kwenda kwenye kijiji cha Kaisaria Filipi, katika kaskazini ya mbali zaidi ya Palestina. Huo ni mpando mrefu unaochukua karibu kilometa 48 kufika pale mahali pazuri ulipo Kaisaria Filipi, zapata meta 350 juu ya usawa wa bahari. Labda kisafari hicho kinachukua siku kadha.
Njiani, Yesu anaenda kando yeye mwenyewe kusali. Ni miezi tisa au kumi tu ambayo inabaki kabla ya kifo chake, na yeye anahangaika juu ya wanafunzi wake. Wengi tayari wamekwisha kuacha kufuata yeye. Inaonekana wengine wamevurugika na kutamaushwa kwa sababu yeye alikataa jitihada za watu kumfanya mfalme na kwa sababu yeye hakuandaa ishara kutoka mbinguni kuthibitisha umaliki wake, wakati alipotolewa mwito wa ushindani na adui zake. Mitume wake wana itikadi gani juu ya utambulisho wake? Wakati wao wanapokuja mahali ambapo yeye anasali, Yesu anaulizia: “Makutano ya watu wanasema kwamba mimi ni nani?”
Watu fulani wanasema Yohana yule Mbatizaji,” wao wanajibu, “wengine Eliya, bado wengine Yeremia au mmoja wa wale manabii.” Ndiyo, wao wanafikiri Yesu ni mmoja wa wanaume hawa ambaye ameinuliwa kutoka kwa wafu!
“Ingawa hivyo, ninyi mnasema mimi ni nani?” Yesu anauliza.
Petro anajibu kwa haraka: “Wewe ndiwe Kristo, yule Mwana wa Mungu anayeishi.”
Baada ya kuonyesha ukubali kwa jibu la Petro, Yesu anasema: “Mimi nasema kwa wewe, Wewe ni Petro, na juu ya tungamo-mwamba hili mimi nitajenga kundi langu, na malango ya Hadesi hayatalishinda nguvu.” Hapa kwanza Yesu anatangaza kwamba yeye atajenga kundi na kwamba hata kifo hakitazuia washiriki walo wakiwa mateka baada ya mwendo wao wa uaminifu duniani. Ndipo yeye anaambia Petro: “Mimi nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbingu.”
Hivyo Yesu anafunua kwamba Petro atapokea mapendeleo ya pekee. La, Petro hapewi mahali pa kwanza miongoni mwa wale mitume, wala yeye hafanywi ule msingi wa kundi. Yesu mwenyewe ndiye ungamo-mwamba ambalo juu yalo kundi lake litajengwa. Lakini Petro atapewa funguo tatu za kufungulia, kama inavyoweza kusemwa, ile nafasi ya vikundi vya watu kuingia katika Ufalme wa mbingu.
Petro alitumia ufunguo wa kwanza kwenye Pentekosti 33 W.K. wakati yeye alipoonyesha Wayahudi wenye kutubu mambo ambayo lazima wafanye ili kuokolewa. Yeye aliutumia ule wa pili muda mfupi baadaye wakati yeye alipofungulia Wasamaria wenye itikadi ile nafasi ya kuingia katika Ufalme wa Mungu. Ndipo, katika 36 W.K. yeye alitumia ufunguo wa tatu kufungulia Wamataifa wasiotahiriwa, Kornelio na rafiki zake, nafasi iyo hiyo.
Yesu anaendelea na mazungumzo yake pamoja na mitume wake. Yeye anawafamausha kwa kueleza juu ya mateso na kifo ambacho yeye ataelekeana nacho karibuni katika Yerusalemu. Kwa kukosa kufahamu kwamba Yesu atafufuliwa kwenye uzima wa kimbingu, Petro anachukua Yesu kwenda kando. “Uwe mwenye fadhili kwako mwenyewe, Bwana,” yeye anasema, “Wewe hutakuwa na tukio baya hili hata kidogo.” Akigeuza mgongo, Yesu anajibu: “Nenda nyuma ya mimi, Shetani! Wewe ni kwazo kwangu mimi, kwa sababu wewe unafikiri, si fikira za Mungu, bali zile za wanadamu.”
Ni wazi kwamba, watu wengine zaidi ya wale mitume wanasafiri pamoja na Yesu, kwa hiyo sasa yeye anawaita hao kueleza kwamba halitakuwa jambo jepesi kuwa wafuasi wake. “Ikiwa mmoja ye yote anataka kuja baada yangu mimi,” yeye anasema, “acha huyo akatae uwenyewe wake mwenyewe na kuokota mti wa mateso wake na kunifuata mimi kwa kuendelea. Kwa maana awaye yote ambaye anataka kuokoa nafsi yake atapoteza hiyo; lakini awaye yote ambaye anapoteza nafsi yake kwa ajili yangu mimi na zile habari njema ataokoa hiyo.”
Ndiyo, wafuasi wa Yesu lazima wawe wenye ushujaa na wenye kujidhabihu ikiwa wao wanataka kuthibitika kuwa wanastahili upendeleo wake, kwa kuwa yeye anasimulia hivi: “Kwa maana awaye yote ambaye anakuwa mwenye aibu juu ya mimi na maneno yangu katika kizazi hiki chenye uzinzi na chenye dhambi, yule Mwana wa binadamu ataaibika pia juu yake wakati yeye atawasili katika utukufu wa Baba yake pamoja na wale malaika watakatifu.” Marko 8:22-38; Mathayo 16:13-28; Luka 9:18-27, NW.
◆ Kwa sababu gani Yesu anahangaika juu ya wanafunzi wake?
◆ Ni maoni gani juu ya utambulisho wa Yesu ambayo watu wanayo?
◆ Ni funguo gani ambazo Petro alipewa, na hizo zilitumiwa jinsi gani?
◆ Ni sahihisho gani ambalo Petro alipokea, na kwa sababu gani?