Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gt sura 62
  • Somo Juu ya Unyenyekevu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Somo Juu ya Unyenyekevu
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Atoa Somo Katika Unyenyekevu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Somo Muhimu Kuhusu Unyenyekevu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • “Mkakae kwa Amani Ninyi kwa Ninyi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Alikuwa Mshikamanifu Licha ya Majaribu
    Igeni Imani Yao
Pata Habari Zaidi
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
gt sura 62

Sura 62

Somo Juu ya Unyenyekevu

BAADA ya kuponya yule mvulana mwenye roho mwovu katika jimbo lililo karibu na Kaisari ya Filipi, Yesu anataka kurudi nyumbani Kapernaumu. Hata hivyo, yeye anataka kuwa peke yake pamoja na wanafunzi wake katika kisafari hicho ili yeye aweze kuwatayarisha zaidi kwa ajili ya kifo chake na madaraka yao baada ya hapo. “Mwana wa binadamu atatiwa mikononi mwa wanadamu,” yeye awaeleza, “nao watamuua, lakini, ajapouawa, yeye atainuka siku tatu baadaye.”

Hata ingawa Yesu alisema mapema zaidi juu ya jambo hilo, na mitume watatu waliona kwa kweli mgeuzo-sura wake wakati ambapo “mwondoko” wake ulizungumzwa, bado wafuasi wake hawana ufahamu kuhusu jambo hilo. Ingawa hakuna yeyote kati yao anayejaribu kukana kwamba yeye atauawa, kama Petro alivyofanya mapema zaidi, wao wanaogopa kumuuliza zaidi juu ya jambo hilo.

Mwishowe wao wanaingia Kapernaumu, ambayo imekuwa aina fulani ya makao-kituo wakati wa huduma ya Yesu. Pia huo ndio mji wa makao ya Petro na hesabu fulani ya mitume wengine. Hapo, wanaume ambao wanakusanya ile kodi ya hekalu wanafikia Petro. Labda wakijaribu kuhusisha Yesu katika jambo fulani la kuvunja desturi inayokubaliwa, wao wanauliza: “Je! mwalimu wenu halipi ile kodi [ya hekalu] ya drakma mbili?”

“Ndiyo,” Petro anaitikia.

Yesu, ambaye huenda akawa alifika kwenye nyumba ile muda mfupi baadaye, ana habari juu ya jambo ambalo limetukia. Kwa Hiyo hata kabla Petro hajatokeza jambo hilo kumweleza, Yesu anauliza: “Wewe unafikiri nini, Simoni? Ni kutoka kwa nani wale wafalme wa dunia wanapokea ushuru au kodi ya kichwa? Kutoka kwa wana wao au kutoka kwa wageni?”

“Kutoka kwa wageni,” Petro anajibu.

“Kwa kweli, basi, wana wako huru na kodi,” Yesu anaonelea. Kwa kuwa Baba ya Yesu ndiye Mfalme wa ulimwengu wote mzima, yule Mmoja ambaye anaabudiwa kwenye hekalu, kwa kweli si takwa la kisheria kwa Mwana wa Mungu kulipa ile kodi ya hekalu. “Lakini kwamba sisi tusisababishe wao kukwazika,” Yesu anasema, “wewe nenda kwenye bahari, tupa ndoana, na uchukue yule samaki wa kwanza anayekuja juu na, wakati wewe unapofungua kinywa chake, wewe utapata sarafu steta [drakma nne]. Ichukue uwape hao kwa ajili yangu nawe.”

Wakati wanafunzi wanapokuja pamoja baada ya kurudi kwao Kapernaumu, labda wakiwa kwenye nyumba ya Petro, wao wanauliza: “Kwa kweli nani aliye mkubwa katika ufalme wa mbingu?” Yesu anajua jambo ambalo linawafanya watokeze swali lao, kwa kuwa ana habari juu ya jambo lililokuwa likiendelea miongoni mwao wakati walipokuwa wamebaki-baki nyuma yake wakati wa kurudi kwao kutoka Kaisaria ya Filipi. Kwa hiyo yeye anauliza: “Ni jambo gani ambalo nyinyi mlikuwa mkibishania barabarani?” Kwa kuona haya, wanafunzi wanaendelea kimya, kwa maana wao walikuwa wamebishana miongoni mwao wenyewe juu ya ni nani angekuwa mkubwa zaidi ya wote.

Baada ya karibu miaka mitatu ya kufundisha kwa Yesu, je! linaonekana kuwa jambo lisiloaminika kwamba wanafunzi wangekuwa na bishano kama hilo? Haya basi, hiyo inafunua lile vutano imara la kutokamilika kwa kibinadamu, na pia la malezi ya kidini. Dini ya Kiyahudi ambamo wanafunzi walikuwa wamelelewa ilikazia cheo au daraja katika shughuli zote. Zaidi ya hilo, labda Petro, kwa sababu ya ahadi ya Yesu ya kupokea “funguo” fulani za kuelekeza kwenye Ufalme, alihisi kuwa mkubwa zaidi. Yakobo na Yohana huenda wakawa na mawazo yanayofanana na hayo kwa sababu ya kuwa wamependelewa kushuhudia mgeuko-sura wa Yesu.

Lolote liwalo, Yesu anafanya wonyesho wa kugusa hisia katika jitihada ya kusahihisha mielekeo yao. Yeye anaita mtoto, anamsimamisha katikati yao, anamzungushia mikono, na kusema: “Isipokuwa nyinyi mnageuka kabisa na kuwa kama watoto wachanga, kwa vyovyote nyinyi hamtaingia katika ufalme wa mbingu. Basi, yule awaye yote ambaye atajinyenyekeza mwenyewe kama huyu mtoto mchanga huyo ndiye mkubwa zaidi ya wote katika ufalme wa mbingu; na yule awaye yote anayempokea mtoto mmoja mchanga kama huyo kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia.”

Hiyo ni njia ya ajabu kama nini ya kusahihisha wanafunzi wake! Yesu hawakasirikii na kuwaita wenye kujigamba, wenye pupa, au wenye kujitakia makuu. Sivyo, bali yeye anatoa kielezi cha fundisho la kusahihisha kwa kutumia watoto wachanga, ambao kwa tabia ni wenye kiasi na wasiojitakia makuu na ambao kwa ujumla hawana fikira za kuwa na madaraja miongoni mwao wenyewe. Hivyo Yesu anaonyesha kwamba wanafunzi wake wanahitaji kukuza sifa hizo ambazo ni tabia ya watoto wanyenyekevu. Kama Yesu anavyomalizia: “Yeye ambaye anajiendesha mwenyewe kama mmoja aliye mdogo zaidi miongoni mwenu nyinyi nyote ndiye mmoja aliye mkuu.” Mathayo 17:22-27; 18:1-5; Marko 9:30-37; Luka 9:43-48, NW.

▪ Warudipo Kapernaumu, Yesu anarudia fundisho gani, nalo linapokewaje?

▪ Kwa nini Yesu hako chini ya wajibu wa kulipa ile kodi ya hekalu, lakini kwa nini yeye anailipa?

▪ Labda ni jambo gani ambalo lilichangia lile bishano la wanafunzi, na Yesu anawasahihishaje?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki