Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gt sura 119
  • Apelekwa kwa Anasi, Kisha kwa Kayafa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Apelekwa kwa Anasi, Kisha kwa Kayafa
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Habari Zinazolingana
  • “Imempasa Kuuawa”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Yesu Apelekwa kwa Anasi, Kisha kwa Kayafa
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Kuhani Mkuu Aliyemhukumu Yesu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Kayafa Alikuwa Mpinzani Mkali wa Ibada ya Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
gt sura 119

Sura 119

Apelekwa kwa Anasi, Kisha kwa Kayafa

YESU, akiwa amefungwa kama mhalifu wa kawaida, aongozwa kwenda kwa Anasi, ambaye hapo kwanza alikuwa kuhani mkuu aliye mashuhuri. Anasi alikuwa kuhani mkuu wakati Yesu akiwa kivulana wa miaka 12 aliwastaajabisha walimu wa kirabi hekaluni. Wana kadhaa wa Anasi walitumikia baadaye wakiwa makuhani wakuu, na wakati uliopo Kayafa mwana-mkwe wake ashikilia cheo hicho.

Labda kwanza Yesu aongozwa kwenda nyumbani kwa Anasi kwa sababu ya umashuhuri wa muda mrefu wa huyo aliye mkuu wa makuhani katika maisha ya kidini ya Kiyahudi. Kituo hiki cha kumwona Anasi chamruhusu wakati Kayafa Kuhani Mkuu kuikusanya Sanhedrini, ile mahakama kuu ya Kiyahudi yenye washiriki 71, na pia kukusanya mashahidi bandia.

Sasa Anasi kuhani mkuu amuuliza Yesu maswali juu ya wanafunzi wake na juu ya fundisho lake. Hata hivyo, Yesu asema hivi kwa kujibu: “Mimi nimesema na ulimwengu waziwazi; sikuzote nalifundisha katika sinagogi na katika hekalu, wakusanyikapo Wayahudi wote; wala kwa siri mimi sikusema neno lo lote. Ya nini kuniuliza mimi? Waulize wale waliosikia ni nini niliyowaambia; wao wanajua niliyoyanena.”

Hapo, mmoja wa maofisa waliosimama karibu na Yesu ampiga kofi usoni, akisema: “Wamjibu hivi Kuhani Mkuu?”

“Kama nimesema vibaya,” Yesu ajibu, “ushuhudie ule ubaya; bali kama nimesema vema, wanipigia nini?” Baada ya kujibiana maneno hayo, Anasi apeleka Yesu kwa Kayafa akiwa amefungwa.

Kufikia sasa makuhani wote wakuu na wanaume wazee na waandishi, ndiyo, Sanhedrini yote, inaanza kukusanyika. Kwa wazi mahali pao pa mkutano ni kao la Kayafa. Hata hivyo, kufanya kesi kama hiyo katika usiku wa Sikukuu ya Kupitwa kwa wazi ni jambo lililo dhidi ya sheria ya Kiyahudi. Lakini hilo halizuii viongozi wa kidini kutofanya kusudi lao ovu.

Tayari, majuma kadhaa kabla ya hapo wakati Yesu alipomfufua Lazaro, Sanhedrini ilikuwa imeamua miongoni mwao wenyewe kwamba ni lazima afe. Na siku mbili tu mapema kidogo, siku ya Jumatano, wenye mamlaka wa kidini walifanya shauri pamoja kumkamata Yesu kwa mbinu ya ujanja ili wamuue. Wazia, yeye kwa kweli alikuwa amehukumiwa adhabu kabla ya kufanyiwa kesi!

Sasa jitihada zaendelea kutafuta mashahidi watakaotoa uthibitisho bandia ili kesi ikuzwe dhidi ya Yesu. Hata hivyo, hakuwezi kupatikana mashahidi wenye kuafikiana katika ushuhuda wao. Hatimaye, wawili waja mbele na kushikilia hivi: “Sisi tulimsikia akisema, Mimi nitalivunja hekalu hili lililofanyika kwa mikono, na katika siku tatu nitajenga jingine lisilofanyika kwa mikono.”

“Hujibu neno?” Kayafa auliza. “Hawa wanakushuhudia nini?” Lakini Yesu abaki kimya. Hata katika shtaka hili bandia, kwa aibu ya Sanhedrini, mashahidi hao hawawezi kufanya hadithi zao ziafikiane. Hivyo basi kuhani mkuu ajaribu mbinu tofauti.

Kayafa ajua jinsi Wayahudi walivyo wepesi kukasirikia mtu yeyote anayedai kuwa ndiye Mwana halisi wa Mungu. Katika pindi mbili mapema kidogo, wao walikuwa wamefanya haraka-haraka kumbandika Yesu jina la kuwa mkufuru astahiliye kifo, mara moja wakikosea kwa kuwazia kwamba alikuwa akidai kwamba yuko sawa na Mungu. Sasa Kayafa adai kwa ujanja hivi: “Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”

Bila kujali ni nini Wayahudi wafikiri, kwa kweli Yesu ndiye Mwana wa Mungu. Na kubaki kimya kungeweza kueweleka kwamaanisha kwamba anakana kuwa ndiye Kristo. Hivyo basi Yesu ajibu kwa ujasiri hivi: “Mimi ndiye, nanyi mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija na mawingu ya mbinguni.”

Hapo, Kayafa, akijionyesha kwa njia ya kutazamisha, ararua mavazi yake na kupaaza sauti: “Amekufuru; tuna haja gani tena ya mashahidi? Tazameni, sasa mmesikia hiyo kufuru yake; mwaonaje ninyi?”

“Imempasa kuuawa,” Sanhedrini yapiga mbiu. Halafu waanza kumfanyia mzaha, nao wasema mambo mengine ya kufuru dhidi yake. Wampiga kofi katika uso wake na kuutemea mate. Wengine wafunika uso wake wote na kumpiga kwa ngumi zao na kusema hivi kimadharau: “Ewe Kristo, tufumbulie; ni nani aliyekupiga?” Mwenendo huu wa kutukana, usio wa kisheria watukia wakati wa ile kesi ya usiku. Mathayo 26:57-68; 26:3, 4; Marko 14:53-65; Luka 22:54, 63-65; Yohana 18:13-24; 11:45-53; 10:31-39; 5: 16-18.

▪ Yesu aongozwa wapi kwanza, na ni nini lampata huko?

▪ Kisha Yesu apelekwa wapi, na kwa kusudi gani?

▪ Kayafa amewezaje kuifanya Sanhedrini ipige mbiu kwamba Yesu astahili kifo?

▪ Ni mwenendo gani wa kutukana, ulio kinyume cha sheria watukia wakati wa ile kesi?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki