Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • dg seh. ya 1 kur. 2-3
  • Je! Kweli Mungu Anatujali?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Kweli Mungu Anatujali?
  • Je, Kweli Mungu Anatujali?
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Yanayohitaji Kujibiwa
    Amkeni!—1991
  • Biblia Inasema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Swali la 3: Kwa Nini Mungu Anaruhusu Niteseke?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Je, Kweli Mungu Anatujali?
dg seh. ya 1 kur. 2-3

Sehemu ya 1

Je! Kweli Mungu Anatujali?

1, 2. Watu huuliza swali gani juu ya Mungu, na kwa nini?

KATIKA wakati fulani maishani mwako, huenda umeuliza: ‘Ikiwa kuna Mungu ambaye kweli anatujali, kwa nini yeye anaruhusu kuteseka kwingi sana?’ Sisi sote tumepatwa na kuteseka au tumejua mtu fulani ambaye amepatwa na kuteseka.

2 Kweli kweli, muda wote wa historia watu wamepatwa na maumivu na uchungu wa moyo kutokana na vita, ukatili, uhalifu, ukosefu wa haki, umaskini, ugonjwa, na kifo cha wapendwa. Katika karne yetu ya 20 pekee, vita vimeua watu zaidi ya milioni 100. Mamia ya mamilioni ya wengine wamejeruhiwa au wakapoteza makao na mali zao. Mambo mengi mno mabaya sana yametukia katika wakati wetu, yakitokeza huzuni kuu, machozi mengi, na hisi ya kuwa hoi upande wa idadi ya watu isiyohesabika.

3, 4. Wengi huhisije juu ya Mungu kuruhusu kuteseka?

3 Baadhi ya watu hupatwa na uchungu na kuhisi kwamba ikiwa kuna Mungu, kwa kweli yeye hatujali. Au huenda hata wakahisi kwamba hakuna Mungu. Kwa mfano, mwanamume aliyepatwa na mnyanyaso wa kikabila uliosababisha kifo cha marafiki na familia katika Vita ya Ulimwengu 1 aliuliza hivi: “Mungu alikuwa wapi wakati tulipomhitaji?” Mwingine, aliyeokoka mauaji ya kimakusudi ya mamilioni yaliyofanywa na Wanazi katika Vita ya Ulimwengu 2 alihuzunishwa sana na kule kuteseka alikoona hata akasema: “Kama ungeramba moyo wangu, ungekutia sumu.”

4 Hivyo, watu wengi hawawezi kuelewa kwa nini Mungu mwema angeruhusu mambo mabaya yatukie. Wao hutia shaka kama kweli yeye anatujali au hata kama yeye yuko. Na wengi wao huhisi kwamba sikuzote kuteseka kutakuwa sehemu ya maisha ya kibinadamu.

[Picha katika ukurasa wa 2, 3]

Je! ulimwengu mpya usio na kuteseka u karibu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki