Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rq somo la 7 kur. 14-15
  • Kumkaribia Mungu Katika Sala

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kumkaribia Mungu Katika Sala
  • Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Habari Zinazolingana
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mkaribie Mungu Kupitia Sala
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Namna ya Kupata Msaada kwa Sala
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Mungu Anataka Tufanye Nini?
rq somo la 7 kur. 14-15

Somo la 7

Kumkaribia Mungu Katika Sala

Kwa nini ni jambo la maana kusali kikawaida? (1)

Twapaswa kusali kwa nani, na jinsi gani? (2, 3)

Ni nini habari zifaazo kwa sala? (4)

Wapaswa usali wakati gani? (5, 6)

Je, Mungu husikiliza sala zote? (7)

1. Sala ni kusema na Mungu kwa unyenyekevu. Wapaswa usali kwa Mungu kikawaida. Hivyo waweza kuhisi uko karibu naye kama vile na rafiki mpendwa. Yehova ni mkuu na mwenye nguvu sana, hata hivyo yeye husikiliza sala zetu! Je, wewe husali kwa Mungu kikawaida?—Zaburi 65:2; 1 Wathesalonike 5:17.

2. Sala ni sehemu ya ibada yetu. Hivyo, twapaswa kusali kwa Mungu, Yehova, pekee. Yesu alipokuwa duniani, sikuzote alisali kwa Baba yake, si kwa yeyote mwingine. Twapaswa kufanya vivyo hivyo. (Mathayo 4:10; 6:9) Hata hivyo, sala zetu zote zapaswa kusemwa katika jina la Yesu. Hilo laonyesha kwamba twastahi cheo cha Yesu na kwamba tuna imani katika dhabihu yake ya fidia.—Yohana 14:6; 1 Yohana 2:1, 2.

3. Tunaposali twapaswa kusema na Mungu kutoka moyoni mwetu. Hatupaswi kuzikariri sala zetu wala kuzisoma kutoka katika kitabu cha sala. (Mathayo 6:7, 8) Twaweza kusali tukiwa katika kikao chochote kile chenye staha, wakati wowote ule, na mahali popote pale. Mungu aweza kusikia hata sala zilizo kimya zinazosemwa moyoni mwetu. (1 Samweli 1:12, 13) Ni vizuri kutafuta mahali pa kimya mbali na watu wengine ili kusema sala zetu za kibinafsi.—Marko 1:35.

4. Unaweza kusali juu ya habari gani? Lolote lile liwezalo kuathiri urafiki wako naye. (Wafilipi 4:6, 7) Sala ya kigezo yaonyesha kwamba twapaswa kusali kuhusu jina na kusudi la Yehova. Twaweza pia kuomba kwamba mahitaji yetu ya kimwili yaandaliwe, dhambi zetu zisamehewe, na kupata msaada ili kukinza kishawishi. (Mathayo 6:9-13) Sala zetu hazipaswi ziwe zenye ubinafsi. Twapaswa kusali tu kuhusu mambo yanayopatana na mapenzi ya Mungu.—1 Yohana 5:14.

5. Waweza kusali wakati wowote ule ambao moyo wako wakusukuma umshukuru au umsifu Mungu. (1 Mambo ya Nyakati 29:10-13) Wapaswa kusali unapokuwa na matatizo na imani yako inapojaribiwa. (Zaburi 55:22; 120:1) Yafaa kusali kabla hujaila milo yako. (Mathayo 14:19) Yehova hutualika tusali “kila wakati.”—Waefeso 6:18.

6. Twahitaji hasa kusali ikiwa tumefanya dhambi nzito. Katika nyakati hizo twapaswa kuomba rehema na msamaha wa Yehova. Tukiungama dhambi zetu kwake na kufanya tuwezavyo kabisa tusizirudie, Mungu yuko “tayari kusamehe.”—Zaburi 86:5; Mithali 28:13.

7. Yehova husikiliza sala za watu waadilifu pekee. Ili sala zako zisikiwe na Mungu, ni lazima uwe ukijaribu uwezavyo kuishi kulingana na sheria zake. (Mithali 15:29; 28:9) Ni lazima uwe mnyenyekevu unaposali. (Luka 18:9-14) Wewe wahitaji kujitahidi kufanya kulingana na yale unayosali. Hivyo utathibitisha kwamba una imani na kwamba kwa kweli unamaanisha yale unayosema. Ndipo tu Yehova atakapojibu sala zako.—Waebrania 11:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki