Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rq somo la 13 kur. 26-27
  • Unaweza Kuipataje Dini ya Kweli?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unaweza Kuipataje Dini ya Kweli?
  • Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Habari Zinazolingana
  • Unawezaje Kuitambua Ibada ya Kweli?
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Unaweza Kuitambua Ibada ya Kweli Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ibada Ambayo Mungu Anakubali
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Jinsi ya Kutambua Dini ya Kweli
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
Pata Habari Zaidi
Mungu Anataka Tufanye Nini?
rq somo la 13 kur. 26-27

Somo la 13

Unaweza Kuipataje Dini ya Kweli?

Je, dini zote zinampendeza Mungu, au ni moja tu? (1)

Kwa nini kuna dini nyingi sana zinazodai kuwa za Kikristo? (2)

Unaweza kutambuaje Wakristo wa kweli? (3-7)

1. Yesu alianzisha dini moja ya kweli ya Kikristo. Kwa hiyo leo ni lazima kuna shirika, au kikundi, kimoja tu, cha waabudu wa kweli wa Yehova Mungu. (Yohana 4:23, 24; Waefeso 4:4, 5) Biblia hufundisha kwamba ni watu wachache tu walio katika barabara nyembamba iongozayo kwenye uhai.—Mathayo 7:13, 14.

2. Biblia ilitabiri kwamba baada ya kifo cha mitume, mafundisho bandia na mazoea yasiyo ya Kikristo yangeingia polepole ndani ya kutaniko la Kikristo. Watu wangevuta waamini wawafuate badala ya kumfuata Kristo. (Mathayo 7:15, 21-23; Matendo 20:29, 30) Hiyo ndiyo sababu sisi huona dini nyingi sana tofauti-tofauti zinazodai kuwa za Kikristo. Twaweza kutambuaje Wakristo wa kweli?

3. Alama yenye kutokeza zaidi ya Wakristo wa kweli ni kwamba wao wana upendo wa kweli miongoni mwao wenyewe. (Yohana 13:34, 35) Wao hawafundishwi kufikiri kwamba wao ni bora kuliko watu wa jamii au rangi nyingine. Wala hawafundishwi kuchukia watu kutoka nchi nyinginezo. (Matendo 10:34, 35) Kwa hiyo wao hawashiriki katika vita. Wakristo wa kweli hutendeana kama ndugu na dada.—1 Yohana 4:20, 21.

4. Alama nyingine ya dini ya kweli ni kwamba washiriki wayo wanaistahi sana Biblia. Wao huikubali kuwa Neno la Mungu na huamini yale inayosema. (Yohana 17:17; 2 Timotheo 3:16, 17) Wao huliona Neno la Mungu kuwa lenye maana zaidi kuliko mawazo au desturi za kibinadamu. (Mathayo 15:1-3, 7-9) Wao hujaribu kuishi kulingana na Biblia katika maisha yao ya kila siku. Kwa hiyo wao hawahubiri jambo moja kisha wanafanya jingine.—Tito 1:15, 16.

5. Ni lazima pia dini ya kweli iheshimu jina la Mungu. (Mathayo 6:9) Yesu alifanya jina la Mungu, Yehova, lijulikane kwa wengine. Ni lazima Wakristo wa kweli wafanye vivyo hivyo. (Yohana 17:6, 26; Warumi 10:13, 14) Ni watu gani katika jumuiya yako wanaoambia wengine kuhusu jina la Mungu?

6. Ni lazima Wakristo wa kweli wahubiri kuhusu Ufalme wa Mungu. Yesu alifanya hivyo. Sikuzote aliongea kuhusu Ufalme. (Luka 8:1) Aliwaamuru wanafunzi wake wahubiri ujumbe uu huu duniani pote. (Mathayo 24:14; 28:19, 20) Wakristo wa kweli wanaamini kwamba Ufalme wa Mungu pekee ndio utaleta amani na usalama wa kweli kwenye dunia hii.—Zaburi 146:3-5.

7. Ni lazima wanafunzi wa Yesu wasiwe sehemu ya ulimwengu huu mwovu. (Yohana 17:16) Wao hawahusiki katika mambo ya kisiasa ya ulimwengu wala katika ubishi mbalimbali wa kijamii. Wao huepuka mwenendo wenye kudhuru, mazoea, na mitazamo iliyo ya kawaida ulimwenguni. (Yakobo 1:27; 4:4) Je, unaweza kutambua kikundi cha kidini katika jumuiya yako ambacho kina alama hizi za Ukristo wa kweli?

[Picha katika ukurasa wa 26, 27]

Wakristo wa kweli hupendana, hustahi Biblia, na huhubiri kuhusu Ufalme wa Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki