Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ie kur. 19-20
  • Nafsi Kulingana na Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nafsi Kulingana na Biblia
  • Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Nafsi” Kama Kiumbe Hai
  • “Nafsi” Kama Uhai wa Kiumbe
  • Je, Una Nafsi Isiyoweza Kufa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Nafsi Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Uhai Baada ya Kifo—Biblia Husema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Nafsi Yako Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
ie kur. 19-20

Nafsi Kulingana na Biblia

“Na mutu alikuwa nafsi ya uhai.”—MWANZO 2:7.

1. Ni jambo gani tunalohitaji kuchunguza ili kuamua kile ambacho Biblia hufundisha juu ya nafsi?

KAMA tulivyoona, imani kuhusu nafsi ni nyingi na zenye umbalimbali. Hata kati ya wale wanaojidai kutegemeza imani zao juu ya Biblia, kunayo mawazo tofauti kuhusu nafsi na jambo linaloipata wakati tunapokufa. Lakini, kwa kweli Biblia inafundisha nini kuhusu nafsi? Ili kupata jibu, tunahitaji kuchunguza maana ya maneno ya Kiebrania na ya Kigiriki ambayo hutafsiriwa “nafsi” katika Biblia.

“Nafsi” Kama Kiumbe Hai

2, 3. (a) Ni neno gani hutafsiriwa kuwa “nafsi” katika Maandiko ya Kiebrania, nayo maana ya msingi ya neno hili ni gani? (b) Namna gani Mwanzo 2:7 huhakikisha kwamba neno “nafsi” laweza kumaanisha mtu mzima?

2 Neno la Kiebrania linalotafsiriwa kuwa “nafsi” ni neʹphesh, nalo laonekana mara 754 katika Maandiko ya Kiebrania (yaitwayo kwa kawaida Agano la Kale). Neʹphesh lamaanisha nini? Kulingana na The Dictionary of Bible and Religion, hilo “kwa kawaida huelekeza kwa kiumbe kizima chenye uhai, mtu mzima.”

3 Kwa mfano, Mwanzo 2:7 hueleza: “BWANA [Yehova, NW] Mungu akafanya mutu wa mavumbi ya inchi, akapuliza pumuzi ya uzima ndani ya pua yake; na mutu alikuwa nafsi ya uhai.” Angalia kwamba Adamu hakupata nafsi; yeye alikuwa nafsi—kama vile mtu anayekuwa daktari ni daktari. Kwa hiyo, neno “nafsi” laweza kueleza mtu mzima.

4, 5. (a) Toa mifano inayoonyesha kwamba neno “nafsi” huelekeza kwa mtu mzima. (b) Namna gani The Dictionary of Bible and Religion hutegemeza uelewevu wa kwamba mtu ni nafsi?

4 Kuelewa huku kunategemezwa popote katika Maandiko ya Kiebrania, ambamo tunakuta misemwa kama vile “na mutu [nafsi, NW] ye yote akifanya zambi” (Walawi 5:1), “na mutu [nafsi, NW] ye yote anayefanya kazi ya namna yo yote” (Walawi 23:30), “mutu akionekana mwenye kuiba mumoja [nafsi, NW] wa ndugu zake” (Kumbukumbu la Torati 24:7), “roho [nafsi, NW] yake ikachokozwa hata kufa” (Waamuzi 16:16), “hata wakati gani mutatesa nafsi yangu?” (Yobu 19:2), na “nafsi yangu inayeyuka kwa uzito.”—Zaburi 119:28.

5 Katika maandiko haya hakuna jambo lolote linaloonyesha kwamba nafsi ni kitu fulani chenye kivuli kinachoendelea kuishi baada ya kifo. Usemi wa kwamba ‘nafsi’ ya mpendwa imeondoka kwenda kuwa pamoja na Bwana au kusimulia juu ya ‘nafsi isiyoweza kufa,’ kungekuwa kusikoeleweka katika utamaduni wa AK [Agano la Kale],” yasema The Dictionary of Bible and Religion.

6, 7. Ni neno gani hutafsiriwa kuwa “nafsi” katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, nayo maana ya msingi ya neno hili ni gani?

6 Neno linalotafsiriwa kuwa “nafsi” zaidi ya mara mia moja katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo (yaitwayo kwa kawaida Agano Jipya) ni psy·kheʹ. Kama vile neʹphesh, neno hili mara nyingi huelekeza kwa mtu mzima. Kwa mfano, fikiria misemwa inayofuata: “Nafsi yangu yataabika.” (Yohana 12:27) “Hofu ikaanza kuwa juu ya kila nafsi.” (Matendo 2:43) “Acheni kila nafsi iwe katika ujitiisho kwa mamlaka zilizo kubwa.” (Waroma 13:1) “Semeni kwa kuliwaza nafsi zilizoshuka moyo.” (1 Wathesalonike 5:14) “Watu wachache, yaani, nafsi nane, walichukuliwa salama kupitia maji.”—1 Petro 3:20.

7 Psy·kheʹ, kama vile neʹphesh, kwa wazi yaelekeza kwa mtu mzima. Kulingana na msomi Nigel Turner, neno hili “lamaanisha kilicho cha namna ya kibinadamu, mwenyewe, mwili wenye nyama ukiwa na rûaḥ [roho] ya Mungu iliyopulizwa ndani yake. . . . Mkazo watiwa juu ya mtu mzima.”

8. Je! wanyama ni nafsi? Fasiria.

8 Katika Biblia neno “nafsi” latumiwa si tu juu ya wanadamu lakini pia juu ya wanyama. Kwa mfano, katika kuelezea uumbaji wa viumbe vya majini, Mwanzo 1:20 lasema kwamba Mungu aliamuru hivi: “Maji yajae kwa wingi na viumbe [nafsi, NW] vilivyo hai.” Na kwenye siku iliyofuata ya uumbaji, Mungu alisema: “Inchi itoe kila kiumbe [nafsi, NW] kilicho hai kwa namna yake, ngombe na mutambazi, na nyama ya inchi kwa namna yake.” (Mwanzo 1:24; linganisha na Hesabu 31:28.) Kwa hiyo, “nafsi” yaweza kuelekeza kwa kiumbe hai, iwe mwanadamu au mnyama.

“Nafsi” Kama Uhai wa Kiumbe

9. (a) Maana gani pana yaweza kutolewa kwa neno “nafsi”? (b) Je! hilo linapingana na wazo la kwamba nafsi ni mtu mwenyewe?

9 Mara nyingine, neno “nafsi” huelekeza kwa maisha ambayo mtu au mnyama hufurahia. Jambo hilo halibadili ufasirio wa Biblia juu ya nafsi kuwa mtu au mnyama. Tutumie kielezi: Tunasema kwamba mtu fulani yuko hai, kumaanisha kwamba yeye ni mtu anayeishi. Tungeweza pia kusema kwamba yeye anao uhai. Katika njia ileile, mtu anayeishi ni nafsi. Lakini, wakati yeye ni hai, “nafsi” yaweza kusemwa kama vile kitu fulani ambacho yeye anacho.

10. Toa mifano kuonyesha kwamba neno “nafsi” laweza kuelekeza kwa uhai ambao mtu au mnyama hufurahia.

10 Kwa mfano, Mungu alimwambia Musa: “Watu wote waliotafuta uzima [nafsi, NW] wako wamekufa.” (Kutoka 4:19) Kwa kweli, maadui wa Musa walikuwa wakitafuta kuondoa uhai wake. Utumizi wenye kufanana na huo wa neno “nafsi” waonekana katika misemwa inayofuata: “Tuliogopa sana kwa uzima [nafsi, NW] wetu” (Yosua 9:24) “Wakakimbia wapate kujiponyesha nafsi zao.” (2 Wafalme 7:7) “Mwenye haki anafikili uzima [nafsi, NW] wa nyama yake.” (Mezali 12:10) “Mwana wa binadamu alikuja . . . kutoa nafsi yake kuwa fidia katika kubadilishana kwa ajili ya wengi.” (Mathayo 20:28) “Alikaribia sana kifo, akihatarisha nafsi yake.” (Wafilipi 2:30) Katika kila kisa, neno “nafsi” lamaanisha “uhai.”a

11. Tuseme nini kuhusu matumizi ya Biblia ya neno “nafsi”?

11 Basi, neno “nafsi” kama linavyotumiwa katika Biblia laelekeza kwa mtu au mnyama au uhai ambao mtu au mnyama hufurahia. Ufasirio wa Biblia juu ya nafsi, ni mwepesi, wenye kupatana, na usiosongwa na falsafa zenye kutatanisha na ushirikina mwingi wa watu. Lakini, jambo gani huifikia nafsi wakati wa kifo? Ili kujibu ulizo hilo, lazima kwanza tuelewe kwa nini tunakufa.

[Maelezo ya Chini]

a Mathayo 10:28 pia hutumia neno “nafsi” kumaanisha “uhai.”

[Picha katika ukurasa wa 20]

Wote ni nafsi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki