Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ie kur. 28-29
  • Kweli Kuhusu Nafsi Ni Jambo la Maana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kweli Kuhusu Nafsi Ni Jambo la Maana
  • Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uhuru Kutoka Woga na Kukosa Tumaini
  • Uhai Baada ya Kifo—Biblia Husema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Je, Una Nafsi Isiyoweza Kufa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • “Kweli Itawaweka Ninyi Huru”—Jinsi Gani?
    Amkeni!—2012
  • Nafsi Kulingana na Biblia
    Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
Pata Habari Zaidi
Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
ie kur. 28-29

Kweli Kuhusu Nafsi Ni Jambo la Maana

“Nanyi mtajua kweli, na kweli itawaweka nyinyi huru.”—YOHANA 8:32.

1. Kwa nini ni jambo la maana kuzichunguza imani zetu kuhusu nafsi na kifo?

IMANI kuhusu kifo na uhai baada ya kifo ni matokeo hasa ya elimu ya kidini na ya kitamaduni ya mtu. Kama tulivyoona, hizo hujipanga kutoka sadikisho la kwamba nafsi hutimiza lengo layo la mwisho kisha tu kuzaliwa upya mara nyingi mpaka kwenye wazo la kwamba kipindi kimoja cha maisha kinaamua tokeo la mwisho la mtu. Kama tokeo, mtu mmoja anaweza kujihisi kuwa hakika kuhusu kuungana mwishowe na nafsi ya upeo baada ya kufa, mtu mwingine anaweza kujisikia kuwa hakika kufikia Nirvana, na bado mwingine kufikia kuvuna dhawabu ya kimbingu. Basi, kweli ni gani? Kwa kuwa imani zetu huwa na uvutano juu ya maelekeo yetu, matendo yetu na maamuzi yetu, je! hatungepaswa kuhangaikia kupata jibu kwa ulizo hilo?

2, 3. (a) Kwa nini tunaweza kuweka tumaini katika kile ambacho Biblia husema kuhusu nafsi? (b) Kama inavyoelezwa katika Biblia, ni nini kweli kuhusu nafsi?

2 Biblia, kitabu cha zamani zaidi sana katika ulimwengu, huiandika historia ya mwanadamu tangu kuumbwa kwa nafsi ya kwanza ya kibinadamu. Kwa wazi, Biblia hueleza kweli kuhusu nafsi: Nafsi yako ni wewe, wafu ni wasioishi kabisa; na wale walio katika kumbukumbu la Mungu watafufuliwa katika wakati wake unaofaa. Kujua mambo hayo kunaweza kumaanisha nini kwako?

3 “Nanyi mtajua kweli, na kweli itawaweka nyinyi huru,” akasema Yesu Kristo kwa wafuasi wake. (Yohana 8:32) Ndiyo, kweli inaweka mtu huru. Lakini, ni kutoka nini kweli kuhusu nafsi itatuweka huru?

Uhuru Kutoka Woga na Kukosa Tumaini

4, 5. (a) Kweli kuhusu nafsi inaondoa woga gani? (b) Namna gani tumaini la ufufuo lilimpa moyo binti aliyefikia mwisho wa ugonjwa wake?

4 “Watu wengi huogopa kifo na wanajaribu kuepuka kufikiri juu yacho,” yasema The World Book Encyclopedia. Mwanahistoria mmoja aonyesha kwamba “katika Mashariki neno ‘kifo’ lenyewe limekuwa karibu lisilotajwa.” Na katika tamaduni nyingine, maneno ya badala kama vile “kufariki” na “kupita” hutumiwa kwa kawaida ili kusimulia juu ya mtu anayekufa. Woga huo wa kifo leo ni woga hasa wa kisichojulikana, kwa kuwa kwa watu wengi kifo ni fumbo. Ujuzi wa kweli kuhusu jambo linalotufikia tunapokufa watuliza woga huo.

5 Tazama, kwa mfano, hali ya akilini ya binti Michaelyn mwenye umri wa miaka 15. Alikuwa na ugonjwa wa leukemia na alipambana na kifo chenye kusikitisha. Mamaye, Paula, akumbuka: “Michaelyn alisema hakuwa mwenye kusumbuliwa na wazo la kufa kwa kuwa alijua kwamba kifo ni jambo la muda tu. Tulizungumza sana kuhusu ulimwengu mpya wa Mungu na kuhusu wale wote watakaofufuliwa humo. Michaelyn alikuwa na imani ya ajabu katika Yehova Mungu na ufufuo—bila shaka yoyote.” Tumaini la ufufuo lilimweka huru binti kijana huyu kutoka woga wenye kulemea wa kifo.

6, 7. Kweli kuhusu nafsi hutuweka huru kutoka ukosefu gani wa tumani? Eleza.

6 Namna gani kweli iliathiri wazazi wa Michaelyn? “Kifo cha binti wetu mdogo kilikuwa jambo lenye kuumiza sana ambalo halijawahi kutufikia kamwe,” asema Jeff, babaye. “Lakini tunatumaini kabisa katika ahadi ya Yehova ya ufufuo, na tunatazama mbele siku moja kumshika mpendwa wetu Michaelyn katika mikono mara nyingine. Huko kutakuwa kukutana kama nini!”

7 Ndiyo, kweli kuhusu nafsi humweka mtu huru kutoka ule ukosefu wa tumaini uwezao kuletwa na kifo cha mpendwa. Hakika, hakuna kitu kiwezacho kuondoa kabisa umizo na sikitiko vinavyompata mtu wakati mpendwa anapokufa. Lakini, tumaini la ufufuo latuliza ombolezo na kufanya iwe rahisi zaidi kuvumilia umizo hilo.

8, 9. Kweli kuhusu hali ya wafu hutuweka huru kutoka woga gani?

8 Kweli ya Kimaandiko kuhusu hali ya wafu pia hutuweka huru kutoka woga wa wafu. Tangu kujifunza kweli hiyo, wengi waliokuwa hapo mwanzo wamefungwa kama kwa pingu na desturi za ushirikina kuhusu wafu hawahangaishwi tena na mambo ya kulaani, ishara mbaya, hirizi, na uchawi, wala hawatoi dhabihu zenye bei ili kutuliza roho za mababu wao waliokufa na kuwazuia kurudi ili kuwadhuru walio hai. Kwa kweli, kwa kuwa wafu “hawajui jambo lolote” mazoea kama hayo ni ya bure.—Mhubiri 9:5.

9 Kweli kuhusu nafsi, ipatikanayo katika Biblia, ni yenye kukomboa na yenye kutumainika kabisa. Lakini tazama pia tazamio la pekee ambalo Biblia yakutolea.

[Blabu katika ukurasa wa 29]

Kweli kuhusu nafsi hukuweka huru kutoka woga wa kifo, woga wa wafu, kukosa tumaini juu ya kifo cha mpedwa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki