Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gf somo la 5 kur. 8-9
  • Rafiki za Mungu Wataishi Katika Paradiso

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Rafiki za Mungu Wataishi Katika Paradiso
  • Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Habari Zinazolingana
  • Maisha Bora Yameahidiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • “Utakuwa Pamoja na Mimi katika Paradiso”
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Paradiso
    Amkeni!—2013
  • “Tutaonana Paradiso!”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
gf somo la 5 kur. 8-9

Somo La 5

Rafiki za Mungu Wataishi Katika Paradiso

Paradiso haitakuwa kama ulimwengu tunamoishi leo. Mungu hakutaka kamwe dunia ijae matatizo na huzuni, maumivu na kuteseka. Wakati ujao, Mungu ataifanya dunia iwe paradiso. Paradiso itakuwaje? Hebu tuone mambo ambayo Biblia inasema:

Watu wema. Paradiso itakuwa makao ya rafiki za Mungu. Watatendeana mema. Wataishi kulingana na njia za Mungu za uadilifu.—Mithali 2:21.

Chakula tele. Njaa haitakuwako katika Paradiso. Biblia inasema hivi: “Na uwepo wingi wa nafaka [au, chakula] katika ardhi juu ya milima.”—Zaburi 72:16.

Nyumba nzuri na kazi yenye kufurahisha. Katika dunia iliyo Paradiso, kila familia itakuwa na makao yake binafsi. Kila mtu atafanya kazi inayoleta furaha ya kweli.—Isaya 65:21-23.

Amani ulimwenguni kote. Watu hawatakuwa wakipigana wala kufa vitani. Neno la Mungu linasema hivi: “[Mungu] avikomesha vita.”—Zaburi 46:8, 9.

Afya njema. Biblia yaahidi hivi: “Hapana mwenyeji [wa Paradiso] atakayesema, Mimi mgonjwa.” (Isaya 33:24) Pia, hakuna mtu atakayekuwa kilema wala kipofu wala kiziwi wala hakuna yeyote atakayeshindwa kuongea.—Isaya 35:5, 6.

Mwisho wa maumivu, huzuni, na kifo. Neno la Mungu lasema hivi: “Kifo hakitakuwapo tena, wala ombolezo wala kupaaza kilio wala umivu halitakuwapo tena kamwe. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”—Ufunuo 21:4.

Watu wabaya hawatakuwako. Yehova anaahidi hivi: “Waovu watatengwa na nchi, nao wafanyao hila watang’olewa.”—Mithali 2:22.

Watu watapendana na kuheshimiana. Ukosefu wa haki, kuonewa, pupa, na chuki hazitakuwapo tena. Watu wataungana nao wataishi kulingana na njia za Mungu za uadilifu.—Isaya 26:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki