Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gf somo la 6 kur. 10-11
  • Paradiso Iko Karibu!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Paradiso Iko Karibu!
  • Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Habari Zinazolingana
  • Maisha Bora—Karibuni!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Dunia Itakuwa Paradiso Wakati Gani?
    Msikilize Mungu Uishi Milele
  • Je, Tunaishi Katika “Siku za Mwisho”?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Je! Inaweza Kuwa Mwisho wa Ulimwengu Ni Karibu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
gf somo la 6 kur. 10-11

SOMO LA 6

Paradiso Iko Karibu!

Mambo mabaya yanayotendeka duniani leo yanaonyesha kwamba Paradiso iko karibu. Biblia ilisema kwamba tungeona nyakati mbaya kabla tu ya Paradiso kuja. Sasa tunaishi katika nyakati hizo! Yafuatayo ni baadhi ya mambo ambayo Biblia ilisema yangetendeka:

Vita vikubwa-vikubwa. “Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme.” (Mathayo 24:7) Unabii huo umetimia. Tangu mwaka wa 1914, kumekuwapo vita viwili vya ulimwengu na vita vingine vingi vidogo-vidogo. Mamilioni ya watu wamekufa katika vita hivyo.

Magonjwa yanayoenea sana. Kungekuwako “mahali pamoja baada ya pengine magonjwa ya kuambukiza.” (Luka 21:11) Je, hilo limetimia? Ndiyo. Kansa, ugonjwa wa moyo, kifua kikuu, malaria, UKIMWI, na magonjwa mengine yameua mamilioni ya watu.

Ukosefu wa chakula. Duniani kote kuna watu ambao hawana chakula cha kutosha. Kila mwaka, mamilioni ya watu hufa njaa. Hiyo ni ishara nyingine ya kwamba Paradiso itakuja hivi karibuni. Biblia inasema hivi: “Kutakuwa na upungufu wa chakula.”—Marko 13:8.

Matetemeko ya dunia. “Kutakuwa . . . matetemeko ya dunia mahali pamoja baada ya pengine.” (Mathayo 24:7) Jambo hilo pia limetimia leo. Watu zaidi ya milioni moja wamekufa katika matetemeko ya dunia tangu mwaka wa 1914.

Watu waovu. Watu wangekuwa “wapenda-fedha” na “wenye kujipenda wenyewe.” Wangekuwa “wenye kuzipenda raha badala ya kuwa wapenda-Mungu.” Watoto wangekuwa “wasiotii wazazi.” (2 Timotheo 3:1-5) Je, wewe hukubali kwamba kuna watu wengi wa aina hiyo leo? Hawamheshimu Mungu hata kidogo, nao huwasumbua wale wanaojaribu kujifunza juu ya Mungu.

Uhalifu. Pia kungekuwako “kuongezeka kwa uasi-sheria.” (Mathayo 24:12) Haikosi utakubali kwamba uhalifu ni mbaya sana kuliko ulivyokuwa miaka kadhaa iliyopita. Kila mahali, watu wamo katika hatari ya kunyang’anywa vitu, kudanganywa, au kuumizwa.

Mambo hayo yote yanaonyesha kuwa Ufalme wa Mungu uko karibu. Biblia inasema hivi: “Mwonapo mambo hayo yakitukia, jueni kwamba ufalme wa Mungu uko karibu.” (Luka 21:31) Ufalme wa Mungu ni nini? Ni serikali ya mbinguni ya Mungu ambayo italeta Paradiso hapa duniani. Ufalme wa Mungu utachukua mahali pa serikali za wanadamu.—Danieli 2:44.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki