Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 6/15 kur. 22-23
  • Je! Inaweza Kuwa Mwisho wa Ulimwengu Ni Karibu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Inaweza Kuwa Mwisho wa Ulimwengu Ni Karibu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • “Mwisho wa Ulimwengu” Ni Karibu!
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Je! “Mwisho wa Ulimwengu” Ni Karibu?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Uharibifu wa Ulimwengu Uliotabiriwa Utakuja Lini?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Siku za Mwisho
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 6/15 kur. 22-23

Neno la Mungu Li Hai

Je! Inaweza Kuwa Mwisho wa Ulimwengu Ni Karibu?

MUDA mfupi kabla ya kifo cha Yesu, wanne wa mitume wake walimwuliza: “Tuambie, ni lini mambo haya yatakapokuwa? na ni nini itakayokuwa ishara ya kuja kwako, na ya mwisho wa ulimwengu?” (Mathayo 24:3, Authorized Version) Tangu wakati huo, nyakati zote Wakristo wametaka kujua habari hiyo. Bila shaka, maneno “mwisho wa ulimwengu” hayana maana ya mwisho wa dunia. Bali, yanamaanisha “umalizio wa mfumo wa mambo,” kama tafsiri za kisasa za Biblia zinavyoonyesha.

Yesu aliwajibu ombi lao la kutaka ishara. Hakutaja tukio moja tu, kama vita mbalimbali, kuwa ndilo ile “ishara.” Alieleza juu ya matukio na hali nyingi mbali-mbali. Mambo hayo yote yalitabiriwa yangetukia wakati ule ambao waandikaji wa Biblia waliuita “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1; 2 Petro 3:3, 4) Unapochunguza mambo haya aliyoyatabiri Yesu, angalia namna yamekuwa yakitimizwa katika muda wa maisha ya watu wanaoishi sasa.

“TAIFA LITAONDOKA KUPIGANA NA TAIFA, NA UFALME KUPIGANA NA UFALME.”​—Mathayo 24:7, NW.

Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, iliyopigwa kuanzia mwaka wa 1914 mpaka wa 1918, ilikuwa kubwa sana kuliko vita vyote vikubwa-vikubwa vikijumlishwa pamoja wakati wa miaka 2,400 iliyotangulia mwaka wa 1914. Lakini miaka 21 tu baada ya kwisha kwa vita hiyo, Vita ya Ulimwengu ya Pili ilianza. Nayo ilikuwa na uharibifu mkubwa mara nne kuliko Vita ya Ulimwengu ya Kwanza. Tangu Vita ya Ulimwengu ya Pili ilipokwisha mwaka wa 1945, watu zaidi ya milioni 25 wameuawa katika vita vingine karibu 150 vilivyopigwa katika sehemu mbalimbali kuizunguka dunia.

“KUTAKUWAKO UPUNGUFU WA CHAKULA . . . MAHALI HAPA NA MAHALI HAPA.”​—Mathayo 24:7, NW.

Baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ilitokea njaa iliyo kubwa zaidi katika historia yote. Lakini upungufu wa chakula ulikuwa mkubwa hata zaidi baada ya Vita ya ulimwengu ya Pili. Wakati huo robo moja ya watu wa ulimwengu mzima walikuwa wakifa njaa. Mamilioni wangali wanauawa na njaa​—karibu watu milioni 50 kwa mwaka! Hata mahali mbalimbali ambako chakula ni tele, watu wengi ni maskini mno wasiweze kukinunua.

“MARADHI YA KIPUKU . . .MAHALI HAPA NA MAHALI HAPA.”​—Luka 21:11, NW.

Mara tu baada ya vita ya Ulimwengu ya Kwanza watu wengi zaidi waliuawa na homa kali ya Kispania kuliko wale waliokuwa wameuawa na ugonjwa wo wote wa kipuku katika historia ya wanadamu. Wenye kuuawa na ugonjwa huo walikuwa watu karibu milioni 21! Hata hivyo maradhi ya kipuku na magonjwa mengine yanaendelea kuwaka kama moto. Mamilioni ya watu wanauawa kila mwaka na ugonjwa wa moyo na kansa (donda baya). Magonjwa ya kisonono na kaswende yanaenea kwa haraka sana. Mgonjwa mengine yaliyo mabaya sana yanatokea nchi baada ya nchi nyingine.

KUTAKUWAKO . . .MATETEMEKO YA ARDHI MAHALI HAPA NA MAHALI HAPA.”​—Mathayo 24:7, NW.

Tangu mwaka wa 1914 mpaka sasa, kumekuwako matetemeko ya ardhi mengi zaidi na makubwa-makubwa kuliko katika kipindi kinginecho chote cha historia iliyoandikwa katika vitabu. Kwa miaka zaidi ya 1,000, tangu mwaka wa 856 W.K. mpaka wa 1914, kulikuwako matetemeko makubwa 24 tu, nayo yaliua watu karibu 1,973, 000. Lakini katika ile miaka 63 ya tangu mwaka wa 1915 mpaka wa 1978, jumla ya watu karibu 1,600,000 wamekufa katika matetemeko ya ardhi 43 yaliyo makubwa.

“KUONGOZEKA KWA KUTOKUTII SHERIA.”​—Mathayo 24:12, NW.

Kutoka sehemu zote za ulimwengu ripoti zinakuja zikieleza kwamba kuna ongezeko la kutokutii sheria na la uhalifu. Uhalifu wa matendo ya jeuri, kama kuua watu, kuingilia wanawake kinguvu na kushambulia watu kwa kuwaotea, ni mambo ambayo sasa yanaongezeka sana yasiweze kuzuiwa.

“WANADAMU WAKIZIMIA MOYO KWA SABABU YA HOFU.”​—Luka 21:26, NW.

Labda woga (hofu) ndiyo maoni ya pekee ya moyoni yaliyo katika maisha za watu leo. Muda mfupi baada ya mlipuko wa makombora ya kwanza ya nyukilia, mwanasayansi wa nguvu za atomi Harold C. Urey alisema hivi: “Sisi tutakula kwa woga, tutalala kwa woga, tutaishi kwa woga na kufa kwa woga.” Watu wanaogopa uhalifu, uchafuaji wa hewa, maji, chakula na ardhi, magonjwa, infuleshoni na mambo mengine mengi yanayotisha maisha zao zenyewe.

Ingawa kuna sehemu nyingine nyingi za ishara hiyo, zile ambazo zimeonyeshwa hapa zinatosha kuthibitisha kwamba tunaishi “siku za mwisho.” Lakini wale wanaotumikia Mungu wataokoka wafurahie maisha katika dunia itakayokuwa imesafishwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki