Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gl kur. 10-11
  • Israeli Na Mataifa Yaliyolizunguka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Israeli Na Mataifa Yaliyolizunguka
  • ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Yehova Alipowasimamisha Waamuzi’
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Israeli Katika Siku Za Daudi Na Sulemani
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Nchi Ya Ahadi
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • B4 Kumiliki Nchi ya Ahadi
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Pata Habari Zaidi
‘Ona Nchi Nzuri’
gl kur. 10-11

Israeli Na Mataifa Yaliyolizunguka

YEHOVA alimwambia Abrahamu: ‘Nenda kutoka Uru wa Wakaldayo mpaka katika nchi ambayo nitakuonyesha.’ Nchi hiyo ilikuwa inakaliwa na kuzungukwa na mataifa mengine.—Mwa 12:1-3; 15:17-21.

Watu wa Mungu walipokuwa wakitoka Misri, walijua kwamba huenda wangekabili upinzani kutoka kwa maadui kama vile “wadhalimu wa Moabu.” (Kut 15:14, 15) Waamaleki, Wamoabu, Waamoni, na Waamori waliishi katika maeneo ambayo Waisraeli wangepitia walipokuwa wakielekea Nchi ya Ahadi. (Hes 21:11-13; Kum 2:17-33; 23:3, 4) Nao Waisraeli wangekabiliana na mataifa mengine maadui yaliyoishi katika nchi ambayo Mungu alikuwa amewaahidi.

Mataifa Ambayo Yangeondolewa

Mungu aliwaambia Waisraeli ‘waondolee mbali mataifa saba yenye hesabu kubwa ya watu’—Wahiti, Wagirgashi, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi—ambao walipaswa kuangamizwa. Watu hao walikuwa na mazoea yaliyopotoka kidini na kiadili. Baadhi ya miungu waliyoabudu ilitia ndani Baali (aliyewakilishwa na nguzo za mawe zilizokuwa na umbo la uume), Moleki (ambaye watoto walitolewa dhabihu kwake), na Ashtorethi (Astarte), mungu wa kike wa nguvu za uzazi.—Kum 7:1-4; 12:31; Kut 23:23; Law 18:21-25; 20:2-5; Amu 2:11-14; Zb 106:37, 38.

Wakati mwingine eneo lote ambalo Mungu angewapa Waisraeli, kuanzia kaskazini ya Sidoni hadi “bonde la mto la Misri,” liliitwa “Kanaani.” (Hes 13:2, 21; 34:2-12; Mwa 10:19) Nyakati nyingine Biblia hutaja majina ya mataifa mbalimbali, majiji yenye kujitawala, au watu walioishi katika eneo hilo. Baadhi ya mataifa hayo yalikuwa na maeneo hususa. Kwa mfano, Wafilisti waliishi pwani, nao Wayebusi waliishi kwenye milima iliyokuwa karibu na Yerusalemu. (Hes 13:29; Yos 13:3) Baada ya muda, mataifa mbalimbali yalihamia maeneo mengine.—Mwa 34:1, 2; 49:30; Yos 1:4; 11:3; Amu 1:16, 23-26.

Waisraeli walipokuwa wakitoka Misri, yaelekea kabila la Waamori ndilo lililokuwa lenye nguvu zaidi.a (Kum 1:19-21; Yos 24:15) Waamori walikuwa wameteka nchi ya Moabu kuanzia kusini hadi kwenye bonde la mto la Arnoni, ingawa eneo lililokuwa ng’ambo ya Mto Yordani kuanzia Yeriko bado liliitwa “nchi tambarare za jangwa la Moabu.” Wafalme Waamori walitawala pia Bashani na Gileadi.—Hes 21:21-23, 33-35; 22:1; 33:46-51.

Ingawa Waisraeli walikuwa wakisaidiwa na Mungu, hawakufutilia mbali mataifa yote yaliyokuwa yamehukumiwa kuangamizwa ambayo baada ya muda yalikuja kuwa mtego kwa Israeli. (Hes 33:55; Yos 23:13; Amu 2:3; 3:5, 6; 2Fa 21:11) Naam, Waisraeli walinaswa licha ya onyo hili: “Usiifuate miungu mingine, miungu yoyote ya vikundi vya watu wanaowazunguka pande zote.”—Kum 6:14; 13:7.

[Maelezo ya Chini]

a Jina “Waamori” sawa na jina “Wakanaani” linaweza kurejelea watu wa eneo fulani kwa ujumla au kurejelea kabila fulani hususa.—Mwa 15:16; 48:22.

[Ramani katika ukurasa wa 11]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Mataifa Ambayo Yangeondolewa Kutoka Nchi Ya Ahadi

UFILISTI (D8)

C8 Ashkeloni

C9 Gaza

D8 Ashdodi

D8 Gathi

D9 Gerari

KANAANI (D8)

B10 WAAMALEKI

C12 Hasar-adari (Adari?)

C12 Kadeshi (Kadesh-barnea)

D8 Lakishi

D9 Beer-sheba

D10 WAAMORI

D11 NEGEBU

E4 Dori

E5 Megido

E5 Taanaki

E6 Afeki

E6 WAHIVI

E7 WAYEBUSI

E8 Beth-shemeshi

E8 Hebroni (Kiriath-arba)

E9 WAHITI

E9 Debiri

E10 Aradi (Mkanaani)

E10 WAKENI

E11 Akrabimu

F4 WAGIRGASHI

F6 Shekemu

F7 WAPERIZI

F7 Gilgali

F7 Yeriko

F8 Yerusalemu

G2 WAHIVI

G2 Dani (Laishi)

G3 Hasori

FOINIKE (D8)

E2 Tiro

F1 Sidoni

EDOMU

F11 SEIRI

G11 Bosra

WAAMORI (SIHONI) (G8)

G6 GILEADI

G7 Shitimu

G7 Heshboni

G9 Aroeri

SIRIA (H1)

G1 Baal-gadi

G2 WAHIVI

I1 Damasko

MOABU (H10)

WAAMORI (OGU)

G6 GILEADI

H3 BASHANI

H4 Ashtarothi

H4 Edrei

AMONI (I7)

H7 Raba

[Jangwa]

h12 JANGWA LA UARABUNI

[Milima]

E4 Ml. Karmeli

E11 Ml. Hori

G1 Ml. Hermoni

G8 Ml. Nebo

[Bahari]

C6 Bahari ya Mediterania (Bahari Kuu)

F9 Bahari ya Chumvi

G4 Bahari ya Galilaya

[Mito na kijito]

B11 B.M. la Misri

F6 Mto Yordani

G6 B.M. la Yaboki

G9 B.M. la Arnoni

G11 B.M. la Zeredi

[Picha katika ukurasa wa 10]

Kulia: Mfalme Ogu wa Amori alitawala Bashani, eneo lililokuwa mashuhuri kwa ufugaji wa mafahali na kondoo

Chini: Moabu, nyika ya Yuda ikiwa ng’ambo ya Bahari ya Chumvi

[Picha katika ukurasa wa 11]

Yehova aliwaagiza Waisraeli wayaondoe mataifa yaliyokuwa yakiabudu miungu ya uwongo, kama vile Baali, Moleki, na Ashtorethi, mungu wa kike wa nguvu za uzazi (ona picha)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki