Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gl kur. 14-15
  • ‘Yehova Alipowasimamisha Waamuzi’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Yehova Alipowasimamisha Waamuzi’
  • ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Habari Zinazolingana
  • Israeli Katika Siku Za Daudi Na Sulemani
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Nchi Ya Ahadi
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Israeli Na Mataifa Yaliyolizunguka
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Yesu “Katika Nchi Ya Wayahudi”
    ‘Ona Nchi Nzuri’
Pata Habari Zaidi
‘Ona Nchi Nzuri’
gl kur. 14-15

‘Yehova Alipowasimamisha Waamuzi’

Makabila na Waamuzi

UNAWEZA kuona kwa urahisi Mlima Tabori (F4) kwenye ramani, uko kusini-magharibi ya Bahari ya Galilaya, katika Bonde la Yezreeli. Ebu wazia wanajeshi 10,000 wakiwa wamekusanyika juu ya mlima huo. Yehova alitumia Mwamuzi Baraka na nabii Debora ili kuwachochea Waisraeli waungane dhidi ya Mfalme Yabini wa Kanaani, aliyekuwa amewakandamiza kwa muda wa miaka 20. Chini ya Sisera, mkuu wa jeshi, magari ya vita 900 ya Yabini yenye miundu mikali ya chuma yalitoka Haroshethi hadi kwenye mto mkavu wa Kishoni, kati ya Megido na Mlima Tabori.

Mwamuzi Baraka aliwaongoza Waisraeli hadi kwenye bonde ili kupigana na majeshi ya Sisera. Yehova aliwapa ushindi kwa kutuma mafuriko ya ghafula yaliyofanya magari ya vita ya Sisera yakwame matopeni, jambo lililowaogopesha Wakanaani. (Amu 4:1–5:31) Huo ulikuwa mojawapo wa ushindi ambao Mungu aliwapa Waisraeli katika kipindi cha Waamuzi.

Nchi ya Kanaani ilipotekwa, iligawanywa kwa makabila ya Israeli. Ona mahali yalipoishi makabila ambayo hayakuwa ya Lawi. Kabila dogo la Simeoni lilipewa majiji yaliyokuwa katika eneo la Yuda. Baada ya kifo cha Yoshua, hali ya kiroho na ya kiadili ya taifa hilo ilizorota. Waisraeli “wakawa katika dhiki kali sana,” kwa sababu ya kukandamizwa na maadui. Kwa huruma zake, ‘Yehova alisimamisha waamuzi’—watu 12 wenye imani na ujasiri—waliowakomboa Waisraeli kwa muda wa karne tatu.—Amu 2:15, 16, 19.

Mwamuzi Gideoni alitumia wanajeshi 300 tu ambao hawakuwa na silaha za kutosha, lakini walikuwa wepesi na wenye nguvu na hivyo akawashinda askari wa Midiani 135,000. Uwanja wa mapigano ulikuwa katikati ya Mlima Gilboa na More. Baada ya kupata ushindi wa kwanza, Gideoni aliwafukuza adui hadi upande wa mashariki kwenye jangwa.—Amu 6:1–8:32.

Yeftha, Mgileadi wa kabila la Manase alikomboa miji ya Israeli iliyokuwa mashariki ya Yordani kutoka kwa wakandamizaji Waamoni. Ili kupata ushindi, yaelekea Yeftha alitumia Barabara ya Mfalme iliyounganisha Ramoth-gileadi na eneo la Aroeri.—Amu 11:1–12:7.

Samsoni alipigana na Wafilisti hasa kwenye eneo la pwani karibu na Gaza na Ashkeloni. Eneo la Gaza liko katika sehemu yenye maji mengi ambayo ni mashuhuri kwa ukulima. Samsoni alitumia mbweha 300 kuteketeza mashamba ya Wafilisti ya nafaka, mizabibu, na mizeituni.—Amu 15:4, 5.

Kama inavyoonyeshwa na simulizi hilo la Biblia au inavyodokezwa na makabila yao, waamuzi walikuwa viongozi katika sehemu zote za Nchi ya Ahadi. Iwe walipigana wapi, Yehova aliwasaidia watu wake wakati wa taabu walipotubu.

[Ramani katika ukurasa wa 15]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Makabila na Waamuzi

Waamuzi

1. Othnieli Makabila ya Manase

2. Ehudi Makabila ya Yuda

3. Shamgari Makabila ya Yuda

4. Baraka Makabila ya Naftali

5. Gideoni Makabila ya Isakari

6. Tola Makabila ya Manase

7. Yairi Makabila ya Manase

8. Yeftha Makabila ya Gadi

9. Ibzani Makabila ya Asheri

10. Eloni Makabila ya Zabuloni

11. Abdoni Makabila ya Efraimu

12. Samsoni Makabila ya Yuda

Mafungu ya Makabila (Ona kichapo)

Majiji Mengine ya Manase

E4 Dori

E5 Megido

E5 Taanaki

F4 En-dori

F5 Beth-sheani (Beth-shani)

F5 Ibleamu (Gath-rimoni)

Majiji Mengine ya Simeoni

C9 Sharuheni (Shaaraimu) (Shilhimu)

C10 Beth-lebaothi (Beth-biri)

D8 Etheri (Tokeni)

D9 Siklagi

D9 Aini

D9 Hasar-susa?

D9 Ashani

D9 Beer-sheba

D10 Hasar-shuali

E9 Etamu

E9 Beth-markabothi

E9 Bethueli? (Kesili?)

E9 Sheba? (Yeshua)

E10 Baalath-beeri (Baali)

E10 Esemu

Majiji ya Makimbilio ya Walawi

E8 Hebroni

F3 Kedeshi

F6 Shekemu

H4 Golani

H5 Ramoth-gileadi

H8 Beseri

Barabara Kuu

B10 Via Maris

G10 Barabara ya Mfalme

Makabila Ya Israeli

DANI (D7)

D7 Yopa

E8 Sora

YUDA (D9)

C8 Ashkeloni

C9 Gaza

C9 Sharuheni (Shaaraimu) (Shilhimu)

C10 Beth-lebaothi (Beth-biri)

C12 Asimoni

C12 Kadeshi

D7 Yabneeli

D8 Etheri (Tokeni)

D9 Siklagi

D9 Aini

D9 Hasar-shuali

D9 Ashani

D9 Beer-sheba

D10 Hasar-shuali

E8 Lehi

E8 Bethlehemu

E8 Hebroni

E9 Etamu

E9 Beth-markabothi

E9 Bethueli? (Kesili?)

E9 Sheba? (Yeshua)

E10 Baalath-beeri (Baali)

E10 Esemu

ASHERI (E3)

E2 Tiro

E4 Haroshethi

E4 Dori

F1 Sidoni

MANASE (E5)

E6 Shamiri (Samaria)

E6 Pirathoni

F6 Shekemu

G5 Abel-mehola

EFRAIMU (E7)

E7 Timnath-sera

F6 Tapua

F6 Shilo

F7 Betheli (Luzi)

NAFTALI (F3)

F2 Beth-anathi

F3 Kedeshi

G3 Hasori

ZABULONI (F4)

E4 Bethlehemu

ISAKARI (F5)

E5 Megido

E5 Kedeshi (Kishioni)

E5 Taanaki

F4 En-dori

F5 Beth-shita

F5 Beth-sheani (Beth-shani)

F5 Ibleamu (Gath-rimoni)

BENYAMINI (F7)

F7 Gilgali

F8 Yerusalemu

DANI (G2)

G2 Dani (Laishi)

MANASE (H3)

H4 Golani

GADI (H6)

G6 Sukothi

G6 Penueli

G6 Mispa (Mispe)

G7 Yogbeha

H5 Ramoth-gileadi

H7 Raba

H7 Abel-keramimu

RUBENI (H8)

G7 Heshboni

G9 Aroeri

H7 Minithi

H8 Beseri

[Mahali Pengine]

I1 Damasko

[Milima]

F4 Ml. Tabori

F4 More

F6 Ml. Ebali

F5 Ml. Gilboa

F6 Ml. Gerizimu

[Bahari]

C5 Bahari ya Mediterania (Bahari Kuu)

F9 Bahari ya Chumvi

G4 Bahari ya Galilaya

[Mito na Vijito]

B11 B.M. la Misri

F6 Mto Yordani

G6 B.M. la Yaboki

G9 B.M. la Arnoni

G11 B.M. la Zeredi

[Picha katika ukurasa wa 14]

Mlima Tabori, katika eneo la Isakari, juu ya Bonde la Yezreeli

[Picha katika ukurasa wa 14]

Mto Kishoni uliofurika ulifanya magari ya vita ya Sisera yakwame matopeni

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki