Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gl kur. 28-29
  • Yesu “Katika Nchi Ya Wayahudi”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu “Katika Nchi Ya Wayahudi”
  • ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Habari Zinazolingana
  • Nchi Ya Ahadi
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • ‘Yehova Alipowasimamisha Waamuzi’
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • B10 Nchi ya Israeli Katika Siku za Yesu
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Israeli Katika Siku Za Daudi Na Sulemani
    ‘Ona Nchi Nzuri’
Pata Habari Zaidi
‘Ona Nchi Nzuri’
gl kur. 28-29

Yesu “Katika Nchi Ya Wayahudi”

Nchi ya Ahadi (Siku za Yesu)

ALIPOKUWA akimhubiria Kornelio, mtume Petro alitaja mambo ambayo Yesu alifanya “katika nchi ya Wayahudi na pia katika Yerusalemu.” (Mdo 10:39) Unafikiri Yesu alitembelea maeneo gani wakati wa huduma yake iliyoathiri historia ya ulimwengu?

“Nchi ya Wayahudi” ilitia ndani Yudea, ambapo Yesu alifanya kazi ya Mungu. (Lu 4:44) Baada ya kubatizwa, Yesu alikaa siku 40 katika nyika ya Yuda (au Yudea), eneo kame na lenye ukiwa ambalo mara kwa mara lilikuwa na waasi na majambazi. (Lu 10:30) Baadaye, Yesu alipokuwa akielekea kaskazini kutoka Yudea alimhubiria mwanamke Msamaria karibu na Sikari.—Yoh 4:3-7.

Vitabu vya Injili vinaonyesha kwamba Yesu alihubiri hasa katika eneo la Galilaya. Ingawa alisafiri kuelekea kusini hadi Yerusalemu ili kuhudhuria sherehe za kila mwaka, alitumia sehemu kubwa ya ile miaka miwili ya kwanza ya huduma yake katika eneo lililo kaskazini mwa Nchi ya Ahadi. (Yoh 7:2-10; 10:22, 23) Kwa mfano, alifunza mambo mengi muhimu na kufanya miujiza yenye kuvutia alipokuwa kwenye Bahari ya Galilaya au karibu na eneo hilo. Kumbuka kwamba alituliza bahari hiyo ilipochafuka na hata akatembea juu yake. Akiwa kwenye mashua, alihubiria umati uliokuwa kwenye fuo zenye changarawe za bahari hiyo. Wafuasi wake wa mapema ambao walikuwa na uhusiano wa karibu naye walitoka katika jamii za wakulima na wavuvi zilizoishi karibu na bahari hiyo.—Mk 3:7-12; 4:35-41; Lu 5:1-11; Yoh 6:16-21; 21:1-19.

Yesu alipokuwa akihubiri huko Galilaya, alifanya Kapernaumu, “jiji lake,” lililokuwa ufuoni kuwa kituo cha huduma yake. (Mt 9:1) Alikuwa kando ya kilima kilichokuwa karibu na mahali hapo wakati wa yale Mahubiri yake maarufu ya Mlimani. Nyakati nyingine, alisafiri kwa mashua kutoka Kapernaumu hadi Magadani, Bethsaida, au maeneo yaliyokuwa karibu.

Ona kwamba ‘jiji la Yesu’ halikuwa mbali na majiji yafuatayo: Nazareti, ambapo alikulia; Kana, ambapo aligeuza maji yakawa divai; Naini, ambapo alimfufua yule mwana wa mjane; na Bethsaida, ambapo alilisha kimuujiza wanaume 5,000 na kumponya kipofu.

Baada ya Pasaka ya mwaka wa 32 W.K., Yesu alielekea kaskazini hadi Tiro na Sidoni, majiji yenye bandari ya Foinike. Kisha akapanua huduma yake hadi kwenye baadhi ya yale majiji kumi ya Kigiriki yaliyoitwa Dekapoli. Yesu alikuwa karibu na Kaisaria Filipi (F2) Petro alipokiri kwamba yeye ndiye Mesiya, na muda mfupi baada ya hapo Yesu aligeuka sura labda akiwa kwenye Mlima Hermoni. Baadaye, Yesu alihubiri katika eneo la Perea lililokuwa ng’ambo ya Yordani.—Mk 7:24-37; 8:27–9:2; 10:1; Lu 13:22, 33.

Yesu alitumia juma lake la mwisho duniani akiwa pamoja na wanafunzi wake huko Yerusalemu, “jiji la yule Mfalme mkuu,” na katika maeneo yaliyokuwa karibu na jiji hilo. (Mt 5:35) Unaweza kuona maeneo yaliyokuwa karibu na Yerusalemu ambayo umesoma katika vitabu vya Injili, kama vile Emau, Bethania, Bethfage, na Bethlehemu.—Lu 2:4; 19:29; 24:13; ona “Eneo la Yerusalemu,” ramani ndogo kwenye ukurasa wa 18.

[Ramani katika ukurasa wa 29]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Nchi ya Ahadi (Siku za Yesu)

Maeneo Katika Siku Za Yesu

Majiji ya Dekapoli

E5 Hipo

E6 Pela

E6 Sikithopoli

F5 Gadara

F7 Gerasa

G5 Dion

G9 Filadelfia

H1 Damasko

H4 Raphana

I5 Kanatha

Barabara Kuu (Ona kichapo)

Njia ya Kawaida Kati ya Galilaya na Yerusalemu (Ona kichapo)

Njia Nyingine Kati ya Galilaya na Yerusalemu, Kupitia Perea (Ona kichapo)

A11 Gaza

B6 Kaisaria

B8 Yopa

B9 Lida

B12 Beeri-sheba

C4 Tolemai

C8 SAMARIA

C8 Antipatrisi

C8 Arimathea

C9 Emau

C10 YUDEA

C11 Hebroni

C12 IDUMEA

D1 Sidoni

D2 Tiro

D3 FOINIKE

D4 GALILAYA

D4 Kana

D5 Sefori

D5 Nazareti

D5 Naini

D7 Samaria

D7 Sikari

D9 Ephraimu

D9 Bethfage

D9 Yerusalemu

D9 Bethania

D10 Bethlehemu

D10 Herodiumu

D10 NYIKA YA YUDA

D12 Masada

E4 Korazini

E4 Bethsaida

E4 Kapernaumu

E4 Magadani

E5 Tiberiasi

E5 Hipo

E6 Bethania? (ng’ambo ya Yordani)

E6 Sikithopoli

E6 Pela

E6 Salimu

E6 Ainoni

E9 Yeriko

F1 ABILENE

F2 Kaisaria Filipi

F4 Gamala

F5 Abila?

F5 Gadara

F7 PEREA

F7 Gerasa

G3 ITURUAEA

G5 Dioni

G6 DEKAPOLISI

G9 Filadelfia

H1 Damasko

H3 TRAKONITISI

H4 Raphana

H12 ARIABIA

I5 Kanatha

[Milima]

D7 Ml. Ebali

D7 Ml. Gerizimu

F2 Ml. Hermoni

[Bahari na Ziwa]

B6 Bahari ya Mediterania (Bahari Kuu)

E4 Bahari ya Galilaya

E10 Bahari ya Chumvi

[Mito]

E7 Yordani Mto

[Chemchemi na Visima]

D7 Jacob’s Fountain

[Picha katika ukurasa wa 28]

Bahari ya Galilaya. Kapernaumu liko upande wa mbele kushoto. Nchi Tambarare ya Genesareti iko upande wa kusini-magharibi mwa picha hii

[Picha katika ukurasa wa 28]

Wasamaria waliabudu kwenye Mlima Gerizimu. Mlima Ebali uko nyuma yake

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki