SEHEMU 1
Mungu Anaweza Kukusaidia Ujitayarishe kwa Ajili ya Siku Yake Kuu
Nabii mmoja wa Mungu alisema: “Ile siku kuu ya Yehova iko karibu.” (Sefania 1:14) Siku hiyo inakaribia haraka, nasi tunapaswa kuzingatia hilo akilini nyakati zote. Je, unajua kwamba wale wanaoitwa Manabii Wadogo wana jambo la kukujulisha kuhusu siku hiyo kuu? Sura ya 1 hadi ya 3 ya kitabu hiki itakusaidia kuwajua vizuri manabii hao 12 na ujumbe ulio katika vitabu vyao. Hivyo, unaweza kufaidika kutokana na mambo waliyoandika, na kupata mafundisho muhimu yanayoweza kukusaidia maishani mwako.