Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/08 uku. 1
  • Izingatie Siku ya Yehova Maishani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Izingatie Siku ya Yehova Maishani
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Anaweza Kukusaidia Ujitayarishe kwa Ajili ya Siku Yake Kuu
    Izingatie Siku ya Yehova Maishani
  • Siku ya Yehova—Ujumbe Muhimu
    Izingatie Siku ya Yehova Maishani
  • Siku ya Yehova
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Mpendeze Mungu Katika Mwenendo na Shughuli Zako
    Izingatie Siku ya Yehova Maishani
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 7/08 uku. 1

Izingatie Siku ya Yehova Maishani

1 “Ile siku kuu ya Yehova iko karibu. Iko karibu, nayo inaharakisha sana.” (Sef. 1:14) Sefania na wale wengine 11 wanaoitwa Manabii Wadogo waliizingatia siku ya Yehova maishani. Kuchunguza vitabu vyao vilivyoongozwa na roho katika Funzo letu la Kitabu la Kutaniko kama vinavyoelezwa katika kitabu Izingatie Siku ya Yehova Maishani kutatusaidia kujitayarisha kwa ajili ya siku hiyo yenye kuogopesha.—Sef. 2:2, 3.

2 Mambo ya Pekee: Badala ya kukazia fikira maana za kinabii au maelezo ya mstari kwa mstari kuhusu vitabu hivyo 12 vya kinabii, kitabu Siku ya Yehova kinaeleza jinsi maandishi hayo yaliyoongozwa na roho yanavyohusu hali tunazokabili kila siku maishani. Kinakazia kwa nini maamuzi na matendo yetu yote yanapaswa kuonyesha kwamba tunaiona siku ya Yehova ikiwa karibu. Kinazungumzia pia maisha ya familia, uhusiano wetu na waamini wenzetu, uchaguzi wetu wa burudani, huduma yetu, na maamuzi kuhusu kazi.

3 Sehemu ya 1 ya kitabu hicho inatupa habari zaidi kuhusu manabii hao 12 na vitabu vyao. Manabii hao walikuwa watu wa aina gani? Ni hali gani tunazokabili leo ambazo walikabili pia? Sehemu ya 2 inazungumza kuhusu Yehova na sifa zake. Manabii hao wanafunua nini kumhusu Yehova na utu wake? Sehemu ya 3 inakazia mwenendo wetu na shughuli zetu. Ni katika njia gani tunaweza kumpendeza Mungu kila siku? Sehemu ya 4 inaeleza jinsi tunavyoweza kuwa na shangwe tunapoendelea kuitarajia siku ya Yehova.

4 Panga Sasa Ili Ufaidike: Azimia sasa kufaidika kikamili kutokana na funzo la kitabu Siku ya Yehova, ambalo litaanza juma la Agosti 4, 2008! Panga kuhudhuria Funzo la Kitabu la Kutaniko kila juma. Tayarisha kila somo kwa makini na uchunguze maandiko ili uone yanavyohusiana na habari inayozungumziwa. Tafakari kuhusu habari hiyo kwa kujiuliza hivi, ‘Ninaweza kutumiaje habari hii nyumbani, shuleni, kazini, katika huduma, na katika shughuli zangu pamoja na ndugu na dada zangu Wakristo?’ Fika kwenye funzo la kitabu ukiwa umejitayarisha kutoa maelezo ili ushiriki katika ubadilishanaji wa kitia-moyo.—Rom. 1:12.

5 Funzo letu la kitabu Siku ya Yehova na litutayarishe sasa, ili tuweze ‘kuistahimili’ siku ya Yehova iliyo “kuu na yenye kuogopesha sana.” Kwa hakika, siku hiyo iko karibu sana!—Yoe. 2:11.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki