SEHEMU 3
Mpendeze Mungu Katika Mwenendo na Shughuli Zako
Ungejibuje ikiwa ungeulizwa, “Yehova anataka nini kutoka kwako?” (Mika 6:8) Mambo yaliyoandikwa na wale manabii 12 yanatusaidia kupata jibu la swali hilo. Kama utakavyoona katika Sura ya 8 hadi ya 10 ya kitabu hiki, vitabu hivyo vinaweza kukusaidia kujua jinsi unavyoweza kuwa msema-kweli nyakati zote na jinsi unavyoweza kuepuka jeuri. Utaona pia kwamba vitabu hivyo vina mashauri mazuri unayoweza kutumia kuhusu maisha ya familia.