SEHEMU 2
Mjue Yehova na Umtumikie
Vile vitabu vya manabii 12 vina ujumbe gani unaotuchochea kutaka kumjua Yehova vizuri zaidi? Kwa nini ujumbe wa Yehova uliotolewa na manabii hao ni muhimu leo? Katika Sura ya 4 hadi ya 7 ya kitabu hiki, utajifunza jinsi unavyopaswa kumwabudu Mungu na kufuata viwango vyake. Kwa mfano, anataka uonyesheje haki unaposhughulika na wengine? Naam, utaona kwamba vitabu hivi 12 vya kinabii vinaweza kuboresha maisha yako leo.