Wimbo Na. 19
Ahadi ya Mungu Kuhusu Paradiso
Makala Iliyochapishwa
1. Mungu wetu ameahidi,
Paradiso kupitia,
Utawala wa Kristo Yesu,
Dhambi, kifo zitoweke.
(KORASI)
Paradiso, Duniani.
Twaiona, kwa imani.
Karibuni, Kristo Yesu,
Atafanya, yote hayo.
2. Karibuni mwana wa Mungu,
Ataanza ufufuo.
‘Utakuwa Paradisoni,’
Kaahidi Yesu Kristo.
(KORASI)
Paradiso, Duniani.
Twaiona, kwa imani.
Karibuni, Kristo Yesu,
Atafanya, yote hayo.
3. Paradiso, katuahidi.
Naye sasa atawala.
Twashukuru Yehova Mungu,
Sifa zake na tuimbe.
(KORASI)
Paradiso, Duniani.
Twaiona, kwa imani.
Karibuni, Kristo Yesu,
Atafanya, yote hayo.
(Ona pia Mt. 5:5; 6:10; Yoh. 5:28, 29.)