Wimbo Na. 100
Sisi Ni Jeshi la Yehova!
Makala Iliyochapishwa
1. Sisi ni jeshi lake,
Yehova Mungu,
Ambalo latangaza,
Ufalme wa Mungu.
Yesu anatawala,
Ndiye Mufalme.
Tumejitolea,
Pasipo woga.
(KORASI)
Sisi ni jeshi lake,
Yehova Mungu,
Twatangaza kwamba,
“Anatawala.”
2. Sisi ni watumishi
Wake Yehova.
Twatafuta kondoo
Wanaougua.
Na chakula kuwapa
Bila kuchoka;
Tuwakaribishe
Mikutanoni.
(KORASI)
Sisi ni jeshi lake,
Yehova Mungu,
Twatangaza kwamba,
“Anatawala.”
3. Jeshi lake Yehova
Lafwata Kristo,
Na tayari kwa vita,
Likiwa imara.
Laonyesha busara,
Na ujasiri.
Licha ya hatari,
Liko imara.
(KORASI)
Sisi ni jeshi lake,
Yehova Mungu,
Twatangaza kwamba,
“Anatawala.”
(Ona pia Efe. 6:11, 14; Flp. 1:7; Flm. 2.)