Wimbo Na. 86
Wanawake Waaminifu, Dada Wakristo
Makala Iliyochapishwa
1. Sara, Maria, Ruthu na wengine—
Washikamanifu, wenye uwezo.
Walimuogopa Yehova Mungu.
Na majina yao tunayajua.
Kuna wengi kama hao pia,
Waliokuwa na imani kwa Mungu.
2. Wema na fadhili na ujasiri;
Wengi huvutiwa na sifa hizo.
Wanawake hao twawakumbuka,
Ambao ni vielelezo bora.
Dada zetu munaowaiga,
Munasitahili pongezi na sifa.
3. Mama, mabinti, wake, na wajane,
Munaotimiza mengi kwa shangwe.
Wenye kiasi na ujitiisho,
Mungu awapenda, jipeni moyo.
Yehova na awategemeze.
Mubaki imara, mutapata tuzo.
(Ona pia Flp. 4:3; 1 Tim. 2:9, 10; 1 Pet. 3:4, 5.)