WIMBO NA. 137
Wanawake Waaminifu, Dada Wakristo
Makala Iliyochapishwa
1. Sara, Maria, Ruthu na wengine—
Washikamanifu, wenye uwezo.
Waliomwogopa Yehova Mungu.
Na majina yao tunayajua.
Kuna wengi kama hao pia,
Waliokuwa na imani kwa Mungu.
2. Wema na fadhili na ujasiri;
Wengi huvutiwa na sifa hizo.
Wanawake hao twawakumbuka,
Ambao ni vielelezo bora.
Kama hao, dada zetu pia,
Mwastahili sana pongezi na sifa.
3. Mama, mabinti, wake, na wajane,
Mnaotimiza mengi kwa shangwe.
Wenye kiasi na ujitiisho,
Mungu awapenda, jipeni moyo.
Yehova na awategemeze.
Dumuni imara, mtapata tuzo.
(Ona pia Flp. 4:3; 1 Tim. 2:9, 10; 1 Pet. 3:4, 5.)