Wimbo Na. 80
Sifa ya Wema
Makala Iliyochapishwa
1. Kujua wema wa Mungu,
Hutupa shangwe nyingi.
Baba yetu wa mbinguni,
Sikuzote ni mwema.
Atuonyesha fadhili
Zisizostahiliwa.
Anastahili ibada,
Ndiye twatumikia.
2. Tumeumbwa kwa mufano,
Na sura yake Mungu.
Tuonyeshe sifa zake,
Wema wake tuige.
Wema wa Mungu tukuze,
Nazo sifa nyingine.
Tumuombe roho yake,
Tunda lake tukuze.
3. Wakristo jamaa zetu,
Waone wema wetu,
Pia wengine waone,
Fadhili zake Mungu.
Tutangazapo Ufalme
Na tumaini letu;
Tusiwe na ubaguzi,
Wote wafaidike.
(Ona pia Zab. 103:10; Marko 10:18; Gal. 5:22; Efe. 5:9.)