Wimbo Na. 130
Muujiza wa Uhai
Makala Iliyochapishwa
1. Kila kitoto, tone la mvua,
Kila mwale wa jua, Kila bua—
Zote n’zawadi; toka kwa Mungu,
Miujiza ya Mungu ya kila siku.
(KORASI)
Tuutumieje uhai wetu?
Tumupende Yule atupaye uhai.
Hata tufanyeje, haununuliki.
Bali ni zawadi—Na ni muujiza.
2. Wengine kama, muke wa Yobu,
Husema: ‘Mulaani Mungu ufe.’
Sivyo tulivyo, tunamusifu.
Tunamushukuru kwa uhai wetu.
(KORASI)
Tuutumieje uhai wetu?
Tuwapende na kuwajali wanadamu.
Hata tufanyeje, haununuliki.
Bali ni zawadi—Na ni muujiza.
(Ona pia Ayu. 2:9; Zab. 34:12; Mhu. 8:15; Mt. 22:37-40; Rom. 6:23.)