Wimbo Na. 140
Maisha ya Painia
Makala Iliyochapishwa
Ni kabla ya jua, usingizi mtamu,
Twaanza kwa sala
Kisha twaenda, kuhubiri.
Tunatabasamu wanasikiliza.
Hata wasiposikiliza,
hatuvunjwi moyo.
(KORASI)
Ni maisha yetu;
Tumeyachagua.
Kuishi atakavyo Mungu.
Tunavumilia,
Kuwe mvua jua.
“Ninakupenda sana wewe Yehova.”
Jua linatua, tumechoka sana,
Twasali kwa shangwe,
moyo umejaa furaha.
Ni maisha yetu, ya kujidhabihu.
Yehova twashukuru,
watumwagia baraka.
(KORASI)
Ni maisha yetu;
Tumeyachagua.
Kuishi atakavyo Mungu.
Tunavumilia,
Kuwe mvua jua.
“Ninakupenda sana wewe Yehova.”
(Ona pia Yos. 24:15; Zab. 92:2; Rom. 14:8.)