Wimbo Na. 139
Wafundishe Kusimama Imara
Makala Iliyochapishwa
Ni shangwe kufunza kondoo
Waweze kukomaa.
Yehova amewaongoza
Kweli ni mali yao.
(KORASI)
Yehova, sikia sala
Tunaomba uwatunze.
Katika jina la Yesu: Wawezeshe;
Wasimame tu imara.
Imani walijaribiwa,
Lakini tulisali.
Na pia tukawafundisha;
Imara wamekuwa.
(KORASI)
Yehova, sikia sala
Tunaomba uwatunze.
Katika jina la Yesu: Wawezeshe;
Wasimame tu imara.
Imani na muidumishe,
Yehova mumwamini.
Tiini na kuvumilia,
Uzima mtapata.
(KORASI)
Yehova, sikia sala
Tunaomba uwatunze.
Katika jina la Yesu: Wawezeshe;
Wasimame tu imara.
(Ona pia Luka 6:48; Mdo. 5:42; Flp. 4:1.)