Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rk seh. ya 1 uku. 3
  • Je, Mungu Anatujali?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Mungu Anatujali?
  • Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Mimi Mwenyewe Sitawasahau Ninyi’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Imani ya Kweli Ni Nini?
    Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
  • Jinsi Watoto Wanavyobadili Ndoa
    Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
  • Upendo wa Mama Unafunua Upendo wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
rk seh. ya 1 uku. 3

SEHEMU YA 1

Je, Mungu Anatujali?

ULIMWENGU leo umejaa matatizo. Mamilioni ya watu hukabiliana na vita, misiba ya asili, magonjwa, umaskini, ufisadi, na maovu mengine. Huenda wewe pia unakabili mahangaiko kila siku. Ni nani anayeweza kutusaidia? Kuna yeyote anayetujali?

Mama akiwa amembeba mtoto wake

Mungu anatupenda sana hata kuliko jinsi mama anavyompenda mtoto wake

Tunaweza kuwa na hakika kwamba Mungu anatujali kikweli. Anasema hivi katika Neno lake Takatifu: “Je, mke anaweza kumsahau mtoto wake anayenyonya hivi kwamba asimhurumie mwana wa tumbo lake? Hata hawa wanawake wanaweza kusahau, lakini mimi mwenyewe sitakusahau wewe.”a

Je, haifariji kujua hivyo? Mungu anatupenda sana hata kuliko jinsi mama anavyompenda mtoto wake—mojawapo ya hisia zenye nguvu sana za mwanadamu. Mungu hatatuacha kamwe! Tayari ametusaidia kwa njia ya kustaajabisha. Jinsi gani? Kwa kutuonyesha siri ya kuwa na maisha yenye furaha—imani ya kweli.

Kuwa na imani ya kweli kutakupa furaha. Imani hiyo itakusaidia kuepuka matatizo mengi na itakusaidia kushughulikia kwa mafanikio matatizo ambayo huwezi kuepuka. Pia itakusaidia kumkaribia Mungu na kukupa amani ya akili na ya moyoni. Imani ya kweli itakuwezesha kuwa na wakati ujao ulio bora—uzima wa milele katika Paradiso!

Hata hivyo, imani ya kweli ni nini? Na unaweza kuisitawisha jinsi gani?

a Ona Isaya 49:15 katika Maandiko Matakatifu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki