Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • fg somo la 6 maswali 1-5
  • Kuna Tumaini Gani kwa Wafu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuna Tumaini Gani kwa Wafu?
  • Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Wafu Wana Tumaini Lolote?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Inakuwaje kwa Wapendwa Wetu Waliokufa?
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Mtu Aliyekuwa Maiti Siku Nne
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Inakuwaje Tunapokufa?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
fg somo la 6 maswali 1-5

SOMO LA 6

Kuna Tumaini Gani kwa Wafu?

1. Kuna habari gani njema kuwahusu wafu?

Lazaro akikaribishwa na dada zake, Maria na Martha, baada ya kufufuliwa

Yesu alipofika Bethania karibu na Yerusalemu, rafiki yake Lazaro alikuwa tayari amekufa kwa siku nne. Yesu alienda mahali ambapo Lazaro alikuwa amezikwa akiandamana na Martha na Maria, dada za Lazaro. Punde si punde, umati ukakusanyika. Wazia shangwe ambayo Martha na Maria walipata Yesu alipomfufua Lazaro!​—Soma Yohana 11:21-24, 38-44.

Tayari Martha alijua habari njema kuhusu wafu. Alijua kwamba Yehova atawafufua wafu ili waishi tena duniani.​—Soma Ayubu 14:14, 15.

2. Wafu wako katika hali gani?

Adamu alivyoumbwa, na baadaye kifo chake

Mungu alimwambia Adamu hivi: “Wewe ni mavumbi nawe utarudi mavumbini.”​—MWANZO 3:19.

Wanadamu waliumbwa kutoka katika mavumbi. (Mwanzo 2:7; 3:19) Sisi ni viumbe wenye nyama na damu. Hatuna nafsi isiyoweza kufa katika miili yetu ya nyama. Kwa hiyo, hakuna sehemu yoyote inayoendelea kuishi baada ya mtu kufa. Tunapokufa, ubongo wetu hufa pia, nayo mawazo yetu hupotea. Hivyo, Lazaro alipofufuliwa hakusema chochote kuhusu hali yake alipokuwa mfu, kwa kuwa wafu hawajui lolote.​—Soma Zaburi 146:4; Mhubiri 9:5, 6, 10.

Je, Mungu huwatesa watu kwenye moto baada ya kufa? Kwa kuwa Biblia hufundisha kwamba wafu hawajui lolote, fundisho la moto wa mateso ni la uwongo. Fundisho hilo huwafanya watu wamlaumu Mungu kwa jambo ambalo hafanyi. Isitoshe, wazo lenyewe la kuwatesa watu katika moto linamchukiza sana.​—Soma Yeremia 7:31.

Tazama video Wafu Wako Katika Hali Gani?

3. Je, wafu wanaweza kuwasiliana nasi?

Wafu hawawezi kuzungumza wala kusikia. (Zaburi 115:17) Lakini malaika fulani ni waovu, nao wanaweza kuzungumza na watu wakijifanya kuwa watu waliokufa. (2 Petro 2:4) Yehova hutukataza tusijaribu kuwasiliana na wafu.​—Soma Kumbukumbu la Torati 18:10, 11.

4. Ni nani watakaofufuliwa?

Mwanamume aliyefufuliwa katika Paradiso akijifunza kumhusu Mungu. Kisha mwanamume huyo anasaidia kuwafundisha wengine ambao wamefufuliwa.

Mamilioni ya watu walio makaburini watafufuliwa ili waishi tena duniani. Hata watu fulani ambao hawakumjua Mungu na walifanya mambo mabaya, watafufuliwa.​—Soma Luka 23:43; Matendo 24:15.

Watakaofufuliwa watajifunza ukweli kumhusu Mungu na kuonyesha imani yao katika Yesu kwa kumtii. (Ufunuo 20:11-13) Wale watakaofufuliwa na kufanya mema wataweza kufurahia uzima wa milele duniani.​—Soma Yohana 5:28, 29.

5. Ufufuo unatufunulia nini kumhusu Yehova?

Mungu alifanya iwezekane kuwa na tumaini la ufufuo kwa kumtuma Mwana wake afe kwa ajili yetu. Kwa hiyo, ufufuo ni wonyesho wa upendo na fadhili zisizostahiliwa za Yehova. Wafu watakapofufuliwa, ungependa kumwona nani hasa?—Soma Yohana 3:16; Waroma 6:23.

Unaweza kupata habari zaidi katika sura ya 6, 7, na ya 10 kwenye kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki