Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yc somo la 4 kur. 10-11
  • Alimfurahisha baba yake na Yehova pia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Alimfurahisha baba yake na Yehova pia
  • Wafundishe Watoto Wako
  • Habari Zinazolingana
  • Alipendwa na Mungu na Rafiki Zake Pia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ahadi ya Yeftha
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Uaminifu Hutuwezesha Kupata Kibali cha Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Ahadi ya Yeftha
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Pata Habari Zaidi
Wafundishe Watoto Wako
yc somo la 4 kur. 10-11
Yeftha akiwa pamoja na binti yake alipokuwa angali msichana mdogo

SOMO LA  4

Alimfurahisha Baba Yake na Yehova Pia

Yeftha akisali kwa Yehova huku jeshi la Israeli likipigana na adui zao

Ni jambo gani ambalo Yeftha anamwahidi Yehova?

Yeftha, arundi nyumbani kutoka vitani, amkumbatia binti yake ambaye amekuja kumlaki

Licha ya kwamba haikuwa rahisi, binti ya Yeftha alitimiza ahadi ambayo baba yake alimwahidi Mungu

Je, unamwona msichana katika picha hii?— Msichana huyu ni binti ya mwanaume fulani aliyeitwa Yeftha. Biblia haitaji jina lake, lakini tunajua kwamba alimfurahisha baba yake na Yehova pia. Sasa, ngoja tujifunze mambo fulani yanayomhusu binti huyo na baba yake, yaani, Yeftha.

Yeftha alikuwa mtu mzuri, na alitumia muda mwingi sana ili kumfundisha mtoto wake kuhusu Yehova. Pia, Yeftha alikuwa mwanaume mwenye nguvu na kiongozi mzuri. Kwa hiyo, Waisraeli wakamwomba Yeftha awaongoze wanapoenda kupigana na adui zao.

Binti ya Yeftha akiokota kuni kwa ajili ya maskani; marafiki wake wamekuja kumtembelea

Marafiki wa binti ya Yeftha walienda kumtembelea kila mwaka

Yeftha alisali kwa Mungu ili amsaidie ashinde. Yeftha alimwahidi Mungu kwamba ikiwa atawashinda adui zake, basi atampa Yehova mtu wa kwanza atakayetoka nje ya nyumba yake atakaporudi nyumbani. Mtu huyo ataishi na kufanya kazi kwenye maskani ya Mungu katika siku zote za maisha yake. Katika siku hizo, maskani ilikuwa mahali ambapo watu walienda ili kumwabudu Mungu. Basi mambo yalikuwa mazuri, Yeftha akawashinda adui zake! Je, unajua ni nani aliyekuwa wa kwanza kabisa kutoka katika nyumba yake aliporudi nyumbani?—

Bila shaka, alikuwa binti ya Yeftha! Huyo ndiye mtoto pekee wa Yeftha, na sasa Yeftha angepaswa kumruhusu aondoke nyumbani. Jambo hilo lilimsikitisha sana Yeftha. Lakini kumbuka kwamba alikuwa ametoa ahadi. Mara moja, binti yake akasema: ‘Baba, ulimwahidi Yehova, kwa hiyo ni lazima uitimize ahadi yako.’

Binti ya Yeftha alikuwa na huzuni pia. Kwani akiwa maskani, hangeweza kuolewa na kupata watoto. Hata hivyo, alitamani sana atimize ahadi ya baba yake na amfurahishe Yehova. Kufanya hivyo kulikuwa jambo la maana zaidi kwake kuliko kuolewa na kupata watoto. Kwa hiyo, akaondoka nyumbani kwao na kwenda kuishi katika maskani, akakaa huko siku zote za maisha yake.

Je, unafikiri jambo alilofanya lilimfurahisha baba yake na Yehova pia?— Bila shaka, baba yake, na Yehova walifurahi sana! Wewe pia, ukiwa mtiifu na ukimpenda Yehova kama binti ya Yeftha, basi utawafurahisha sana wazazi wako na Yehova pia.

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • Kumbukumbu la Torati 6:4-6

  • Waamuzi 11:30-40

  • 1 Wakorintho 7:37, 38

MASWALI:

  • Yeftha alikuwa nani? Alimwahidi Mungu jambo gani?

  • Kwa nini ilikuwa vigumu kwa binti ya Yeftha kufanya jambo ambalo baba yake alimwahidi Mungu?

  • Ni jambo gani ambalo binti ya Yeftha aliliona kuwa la maana zaidi kuliko kuolewa na kupata watoto?

  • Unapaswa kufanya nini ili uwe kama binti ya Yeftha?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki