Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 36 uku. 88-uku. 89 fu. 1
  • Ahadi ya Yeftha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ahadi ya Yeftha
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Ahadi ya Yeftha
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Alimfurahisha baba yake na Yehova pia
    Wafundishe Watoto Wako
  • Alipendwa na Mungu na Rafiki Zake Pia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Uaminifu Hutuwezesha Kupata Kibali cha Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 36 uku. 88-uku. 89 fu. 1
Yeftha anararua mavazi yake binti yake anapokuja kumpokea

SOMO LA 36

Ahadi ya Yeftha

Waisraeli walimwasi tena Yehova na kuanza kuabudu miungu ya uwongo. Hata hivyo, miungu hiyo haikuwasaidia waliposhambuliwa na Waamoni. Waisraeli waliteseka kwa miaka mingi. Hatimaye, walimwambia hivi Yehova: ‘Tumekutendea dhambi. Tafadhali tuokoe kutoka kwa adui zetu.’ Kisha, wakaziharibu sanamu zao na kuanza tena kumtumikia Yehova. Yehova hakutaka kuona wakiendelea kuteseka.

Shujaa aliyeitwa Yeftha alichaguliwa ili awaongoze Waisraeli kupigana na Waamoni. Yeftha alimwahidi Yehova hivi: ‘Ukitusaidia kushinda vita hivi, nitakaporudi nyumbani, nitakupa mtu wa kwanza kuja kunipokea.’ Yehova alisikiliza sala ya Yeftha na akamsaidia kushinda vita.

Yeftha aliporudi nyumbani, binti yake, mtoto wake pekee, ndiye alikuwa mtu wa kwanza kuja kumpokea. Alikuwa akicheza dansi na kupiga tari. Yeftha angefanya nini? Alikumbuka ahadi yake na kusema hivi: ‘Ole wangu, binti yangu! Umenivunja moyo. Nilitoa ahadi kwa Yehova. Ili kuitimiza, ninapaswa kukupeleka Shilo ukatumikie kwenye maskani.’ Binti yake akamwambia hivi: ‘Baba, ikiwa umetoa ahadi kwa Yehova, unapaswa kuitimiza. Ninaomba uniruhusu niende milimani na rafiki zangu wa kike kwa miezi miwili. Baada ya hapo nitaenda Shilo.’ Binti ya Yeftha alitumikia kwa uaminifu kwenye maskani maisha yake yote. Kila mwaka rafiki zake walienda Shilo kumtembelea.

Rafiki za binti ya Yeftha wakimtembelea kwenye maskani

“Yeyote anayempenda mwana au binti kuliko anavyonipenda hanistahili.”—Mathayo 10:37

Maswali: Yeftha alitoa ahadi gani? Binti ya Yeftha alitendaje kuhusu ahadi ya baba yake?

Waamuzi 10:6–11:11; 11:29-40; 1 Samweli 12:10, 11

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki