Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yc somo la 13 kur. 28-29
  • Timotheo alitaka kuwasaidia watu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Timotheo alitaka kuwasaidia watu
  • Wafundishe Watoto Wako
  • Habari Zinazolingana
  • Timotheo—Alikuwa Tayari na Mwenye Nia ya Kutumikia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Paulo, Sila, na Timotheo
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Timotheo—“Mtoto Halisi Katika Imani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • “Mtoto Wangu Mpendwa na Mwaminifu Katika Bwana”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Wafundishe Watoto Wako
yc somo la 13 kur. 28-29
Timotheo akijifunza kwa mama yake, Eunike na nyanya yake, Loisi

SOMO LA 13

Timotheo Alitaka Kuwasaidia Watu

Timotheo alikuwa kijana ambaye alitamani sana kuwasaidia watu. Alisafiri mahali pengi ili awasaidie watu wengine. Kwa sababu ya kufanya hivyo, alifurahia sana maisha yake. Je, ungependa kusikia hadithi inayomhusu Timotheo?—

Mama na nyanya ya Timotheo walimfundisha kuhusu Yehova

Timotheo alilelewa katika jiji lililoitwa Listra. Nyanya (bibi) yake aliyeitwa Loisi na mama yake, Eunike, walianza kumfundisha Timotheo kuhusu Yehova tangu alipokuwa mdogo. Timotheo alipoendelea kukua, alitaka kuwasaidia watu wengine wajifunze kuhusu Yehova.

Timotheo alipokuwa bado kijana, Paulo alimwomba wasafiri pamoja na kwenda katika maeneo mengine ili wakahubiri. Timotheo alisema: ‘Sawa!’ Alikuwa tayari kwenda na kuwasaidia watu wengine.

Timotheo alisafiri pamoja na Paulo hadi katika jiji lililoitwa Thesalonike, jiji hilo lilikuwa katika eneo la Makedonia. Ili kufika Thesalonike, walihitaji kutembea umbali mrefu sana na baada ya kutembea wapande mashua. Walipofika katika jiji hilo, waliwasaidia watu wengi wajifunze kuhusu Yehova. Lakini watu fulani walikasirika na walijaribu kuwaumiza. Kwa hiyo, Paulo na Timotheo wakalazimika kuondoka na kwenda kuhubiri katika maeneo mengine.

Timotheo akisafiri na Mtume Paulo katika mashua

Timotheo alikuwa na furaha na maisha mazuri

Baada ya miezi michache kupita, Paulo alimwomba Timotheo arudi Thesalonike ili akaone akina ndugu wanaendeleaje. Bila shaka alihitaji ujasiri sana ili arudi katika jiji hilo hatari! Lakini Timotheo alienda kwa sababu alikuwa na wasiwasi kuhusiana na hali ya akina ndugu wa Thesalonike. Alirudi kwa Paulo akiwa na habari njema. Akina ndugu katika Thesalonike walikuwa wanaendelea vizuri sana!

Timotheo alifanya kazi na Paulo kwa miaka mingi. Wakati fulani Paulo aliandika kwamba Timotheo ndiye aliyefaa zaidi kutumwa ili ayasaidie makutaniko. Timotheo alimpenda Yehova, na aliwapenda watu pia.

Je, unawapenda watu na unataka kuwafundisha kuhusu Yehova?— Ukifanya hivyo, utakuwa na furaha sana na pia utakuwa na maisha mazuri kama Timotheo!

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • 2 Timotheo 1:5; 3:15

  • Matendo 16:1-5; 17:1-10

  • 1 Wathesalonike 3:2-7

  • Wafilipi 2:19-22

MASWALI:

  • Timotheo alilelewa katika jiji gani?

  • Kwa nini Timotheo alitaka kusafiri na Paulo?

  • Kwa nini Timotheo alirudi katika jiji la Thesalonike?

  • Unapaswa kufanya nini ili uwe na maisha mazuri kama Timotheo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki