Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 100 uku. 232-uku. 233 fu. 2
  • Paulo, Sila, na Timotheo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Paulo, Sila, na Timotheo
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Timotheo—Alikuwa Tayari na Mwenye Nia ya Kutumikia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Timotheo alitaka kuwasaidia watu
    Wafundishe Watoto Wako
  • Timotheo—“Mtoto Halisi Katika Imani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • “Mtoto Wangu Mpendwa na Mwaminifu Katika Bwana”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 100 uku. 232-uku. 233 fu. 2
Paulo, Sila, na Timotheo

SOMO LA 100

Paulo na Timotheo

Eunike, Loisi, na Timotheo akiwa mdogo

Timotheo alikuwa ndugu kijana katika kutaniko la Listra. Baba yake alikuwa Mgiriki, na mama yake alikuwa Myahudi. Mama yake Eunike na nyanya yake Loisi walimfundisha Timotheo kumhusu Yehova tangu alipokuwa mtoto mchanga.

Paulo alipotembelea Listra katika safari yake ya pili ya kuhubiri, alitambua kwamba Timotheo aliwapenda sana akina ndugu na alitaka kuwasaidia. Paulo akamwalika Timotheo asafiri pamoja naye. Hatua kwa hatua, Paulo alimzoeza Timotheo kuwa mhubiri na mwalimu stadi wa habari njema.

Roho takatifu iliwaongoza Paulo na Timotheo kila mahali walipoenda. Usiku mmoja, katika maono, mwanamume fulani alimwambia Paulo aende Makedonia akawasaidie. Kwa hiyo, Paulo, Timotheo, Sila na Luka wakaenda huko kuhubiri na kuanzisha makutaniko.

Katika jiji la Thesalonike lililoko Makedonia, wanaume na wanawake wengi wakawa Wakristo. Lakini baadhi ya Wayahudi wakawa na wivu kumwelekea Paulo na waandamani wake. Wakawakusanya watu wenye kufanya ghasia na kuwakokota akina ndugu hao hadi kwa watawala wa jiji, wakipaza sauti hivi: ‘Watu hawa ni maadui wa serikali ya Roma!’ Uhai wa Paulo na Timotheo ulikuwa hatarini, kwa hiyo wakakimbilia Beroya wakati wa usiku.

Watu kule Beroya walikuwa na tamaa ya kujifunza kuhusu habari njema, na Wayahudi na Wagiriki wakawa waamini. Lakini Wayahudi fulani walipokuja kutoka Thesalonike na kuwachochea watu wafanye fujo, Paulo akaenda Athene. Timotheo na Sila walibaki Beroya ili kuwatia moyo akina ndugu. Baada ya muda, Paulo alimtuma Timotheo arudi Thesalonike akawasaidie akina ndugu kukabiliana na mateso makali. Baadaye, Paulo alimtuma Timotheo ayatembelee na kuyatia moyo makutaniko mengine mengi.

Mtume Paulo akiwa katika kifungo cha nyumbani amefungwa mnyororo ulioshikwa na mlinzi huku akimwambia Timotheo maneno ya kuandika katika barua

Paulo alimwambia Timotheo hivi: ‘Wote wanaotaka kumtumikia Yehova watateswa.’ Timotheo aliteswa na akafungwa gerezani kwa sababu ya imani yake. Alifurahi kwamba alipata nafasi ya kuthibitisha ushikamanifu wake kwa Yehova.

Paulo aliwaambia Wafilipi hivi: ‘Ninamtuma Timotheo kwenu. Atawafundisha jinsi ya kutembea katika kweli, na atawazoeza katika huduma.’ Paulo alijua kwamba angeweza kumtegemea Timotheo. Walifanya kazi pamoja wakiwa marafiki na wafanyakazi wenzi kwa miaka mingi.

“Sina mtu mwingine aliye na mwelekeo kama wake atakayejali kwa unyoofu mahangaiko yenu. Kwa maana wengine wote wanatafuta faida zao wenyewe, si za Yesu Kristo.”​—Wafilipi 2:20, 21

Maswali: Timotheo alikuwa nani? Kwa nini Paulo na Timotheo walikuwa marafiki wa karibu sana?

Matendo 16:1-12; 17:1-15; Wafilipi 2:19-22; 2 Timotheo 1:1-5; 3:12, 14, 15; Waebrania 13:23

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki