Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • hf seh. ya 4 kur. 12-14
  • Jinsi ya Kupanga Matumizi ya Pesa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kupanga Matumizi ya Pesa
  • Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • 1 PANGENI KWA MAKINI
  • 2 ZUNGUMZIENI MAMBO HUSUSA WAZIWAZI
  • Kupanga Matumizi ya Pesa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Maoni Yenye Usawaziko Kuhusu Pesa
    Amkeni!—2015
  • Pesa
    Amkeni!—2014
  • Je, Pesa Ndio Chanzo cha Uovu Wote?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
hf seh. ya 4 kur. 12-14
Wenzi wa ndoa wakipanga kwa uanglifu jinsi ya kutumia pesa

SEHEMU YA 4

Jinsi ya Kupanga Matumizi ya Pesa

“Kwa shauri mipango yenyewe hufanywa imara.”​—Methali 20:18

Sisi sote tunahitaji pesa ili kuandalia familia zetu mahitaji yao. (Methali 30:8) Ni kweli kwamba “pesa ni ulinzi.” (Mhubiri 7:12) Mkiwa wenzi wa ndoa, huenda ikawa vigumu kwenu kuzungumzia mambo ya pesa, lakini msiruhusu pesa zivuruge ndoa yenu. (Waefeso 4:32) Mume na mke wanapaswa kuaminiana na kushirikiana wanapopanga matumizi ya pesa.

1 PANGENI KWA MAKINI

BIBLIA INASEMA HIVI: “Ni nani kati yenu anayetaka kujenga mnara ambaye haketi kwanza na kuhesabu gharama, ili aone kama ana kiasi cha kutosha kuukamilisha?” (Luka 14:28) Ni muhimu kwenu kupanga pamoja jinsi ya kutumia pesa zenu. (Amosi 3:3) Amueni vitu mnavyohitaji na kiasi mnachoweza kutumia. (Methali 31:16) Kama mna pesa za kununua kitu fulani, hilo halimaanishi kwamba lazima mkinunue. Jitahidini kuepuka madeni. Tumieni tu pesa mlizo nazo.​—Methali 21:5; 22:7.

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Kama pesa fulani zinabaki mwisho wa mwezi, amueni mtakavyozitumia

  • Kama kuna upungufu, fanyeni mipango ya kupunguza matumizi. Kwa mfano, mnaweza kula nyumbani badala ya kula mikahawani

Wenzi wa ndoa wakirekebisha matumizi yao makubwa ya fedha

2 ZUNGUMZIENI MAMBO HUSUSA WAZIWAZI

BIBLIA INASEMA HIVI: “Tunafanya mpango wa unyoofu, si machoni pa Yehova tu, bali pia machoni pa wanadamu.” (2 Wakorintho 8:21) Uwe mnyoofu unapomwambia mwenzi wako kuhusu pesa unazopata na kiasi unachotumia.

Sikuzote shauriana na mwenzi wako unapofanya maamuzi makubwa kuhusu pesa. (Methali 13:10) Kuzungumza kuhusu pesa kutasaidia kudumisha amani katika ndoa yenu. Ona mapato yako, si kama pesa zako, bali kama pesa za familia.​—1 Timotheo 5:8.

Wenzi wakitazama  orodha ya vitu watakavyonunua

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Kubalianeni kuhusu kiasi ambacho kila mmoja anaweza kutumia bila kumjulisha mwenzake

  • Msingoje mpaka tatizo litokee ili mzungumze kuhusu pesa

MAONI YAKO KUHUSU PESA

Ingawa pesa ni muhimu usiruhusu zivuruge ndoa yako au kusababisha mahangaiko yasiyo ya lazima. (Mathayo 6:25-34) Si lazima uwe na pesa nyingi ili ufurahie maisha. Biblia inasema: “Mjilinde na kila namna ya tamaa.” (Luka 12:15) Ndoa yako ni muhimu kuliko kitu chochote ambacho pesa zinaweza kununua. Kwa hiyo, ridhika na vitu mlivyo navyo, na usipuuze kamwe uhusiano wako pamoja na Mungu. Ukifanya hivyo, ndoa yako itakuwa na furaha na utapata kibali cha Yehova.​—Waebrania 13:5.

JIULIZE . . .

  • Tunaweza kufanya nini tukiwa familia ili tuepuke madeni?

  • Ni lini mara ya mwisho mimi na mwenzi wangu tulizungumza waziwazi kuhusu pesa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki