Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • hf seh. ya 5 kur. 15-17
  • Jinsi ya Kuishi kwa Amani na Watu wa Ukoo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kuishi kwa Amani na Watu wa Ukoo
  • Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • 1 UWE NA MAONI YANAYOFAA KUHUSU WATU WA UKOO
  • 2 WEKENI MIPAKA INAPOHITAJIKA
  • Uwe Mshikamanifu kwa Mwenzi Wako
    Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
  • Fuata Mwongozo wa Mungu ili Uwe na Ndoa Yenye Furaha
    Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
  • Mtendee Mwenzi Wako wa Ndoa kwa Heshima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Baada ya Siku ya Harusi
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
hf seh. ya 5 kur. 15-17
Mama-mkwe akimtazama kwa dharau jinsi binti-mkwe  wake anavyopika

SEHEMU YA 5

Jinsi ya Kuishi kwa Amani na Watu wa Ukoo

“Jivikeni . . . fadhili, unyenyekevu wa akili, upole, na ustahimilivu.”​—Wakolosai 3:12

Watu wanapofunga ndoa wanaanzisha familia mpya. Ingawa utaendelea kuwapenda na kuwaheshimu wazazi wako, sasa mwenzi wako ndiye mtu muhimu zaidi maishani mwako. Huenda ikawa vigumu kwa baadhi ya watu wa ukoo kukubali jambo hilo. Lakini kanuni za Biblia zinaweza kukusaidia kuwa na usawaziko, ili udumishe amani na watu wa ukoo na wakati uleule ujitahidi kuiimarisha familia yako mpya.

1 UWE NA MAONI YANAYOFAA KUHUSU WATU WA UKOO

Wenzi wa ndoa wakiwa pamoja na wazazi wao

BIBLIA INASEMA HIVI: “Mheshimu baba yako na mama yako.” (Waefeso 6:2) Hata uwe na umri gani, sikuzote unapaswa kuwaheshimu wazazi wako. Kumbuka kwamba mwenzi wako pia, akiwa mwana au binti, anahitaji kuwafikiria wazazi wake. “Upendo hauna wivu,” hivyo usihisi vibaya kwa sababu ya uhusiano wa mwenzi wako pamoja nao.​—1 Wakorintho 13:4; Wagalatia 5:26.

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Epuka kusema mambo kwa ujumla, kama vile “Familia yako hunidharau sikuzote” au “Mama yako hapendi chochote ninachofanya”

  • Jaribu kuelewa maoni ya mwenzi wako

2 WEKENI MIPAKA INAPOHITAJIKA

BIBLIA INASEMA HIVI: “Mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake nao watakuwa mwili mmoja.” (Mwanzo 2:24) Mnapofunga ndoa, huenda wazazi wenu wakahisi kwamba wanapaswa kuendelea kuwatunza, na huenda wakataka kuingilia ndoa yenu kupita kiasi.

Wewe na mwenzi wako mnahitaji kukubaliana kuhusu mipaka ambayo mtawawekea na kuwaeleza kwa upendo. Mnaweza kuwaambia moja kwa moja na waziwazi bila kuwakosea heshima. (Methali 15:1) Mkionyesha unyenyekevu, upole, na subira mtakuwa na uhusiano mzuri na watu wa ukoo na kuendelea “kuvumiliana katika upendo.”​—Waefeso 4:2.

Mume na mke wakijadiliana; mume na mke wakiwapatia  wazazi zawadi

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Ikiwa unahisi kwamba watu wa ukoo wanajihusisha kupita kiasi na maisha yenu, zungumzia jambo hilo pamoja na mwenzi wako kwa utulivu

  • Kubalianeni jinsi mtakavyoshughulikia hali hizo

JITAHIDI KUELEWA

Ni muhimu kuelewa hisia na maoni ya wazazi wako. Hawana nia mbaya. Wanakujali kikweli. Huenda ikawa vigumu kwa wazazi wako kukuona wewe na mwenzi wako kama familia inayojisimamia. Huenda hata wakahisi upweke. Hata hivyo, ukifuata kanuni za Biblia na kuwasiliana waziwazi, utawaheshimu wazazi wako bila kupuuza ndoa yako.

JIULIZE . . .

  • Kwa nini ni jambo la kawaida kwa wazazi wa mwenzi wangu kupendezwa na ndoa yetu?

  • Ninawezaje kumtanguliza mwenzi wangu na wakati uleule kuwaheshimu wazazi wangu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki