Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • hf seh. ya 8 kur. 26-28
  • Majanga Yanapotokea

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majanga Yanapotokea
  • Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • 1 MTEGEMEE YEHOVA
  • 2 JITUNZE WEWE NA FAMILIA YAKO
  • 3 OMBA MSAADA
  • Jinsi ya Kukabiliana na Tatizo la Afya
    Habari Zaidi
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Yehova Anawalinda Watu Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Jinsi ya Kupata Tumaini Katikati ya Hali ya Kukata Tumaini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha
hf seh. ya 8 kur. 26-28
Mume na mke wakiomboleza kwa sababu ya kumpoteza mtoto wao

SEHEMU YA 8

Majanga Yanapotokea

“Nanyi mnashangilia sana katika jambo hilo, ingawa kwa muda kidogo sasa, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa na majaribu ya namna mbalimbali.” ​—1 Petro 1:6

Hata ingawa unajitahidi kuwa na ndoa na familia yenye furaha, mambo yasiyotarajiwa yanaweza kutokea na kufanya upoteze shangwe yako. (Mhubiri 9:11) Kwa upendo, Mungu hutusaidia tunapokabili hali ngumu. Ukifuata kanuni za Biblia, wewe na familia yako mnaweza kukabiliana na hali yoyote ile, hata iwe ngumu kadiri gani.

1 MTEGEMEE YEHOVA

BIBLIA INASEMA HIVI: “Huku mkitupa mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.” (1 Petro 5:7) Sikuzote kumbuka kwamba si Mungu anayesababisha matatizo. (Yakobo 1:13) Kadiri unavyozidi kumkaribia, ndivyo atakavyozidi kukusaidia. (Isaya 41:10) “Mimineni moyo wenu mbele zake.”​—Zaburi 62:8.

Pia, utapata faraja ukisoma na kujifunza Biblia kila siku. Ukifanya hivyo, utaona jinsi Yehova “[anavyo]tufariji katika dhiki yetu yote.” (2 Wakorintho 1:3,  4; Waroma 15:4) Ameahidi kukupa “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote.”​—Wafilipi 4:6, 7, 13.

Mwanamume akiwa hospitali anasali na familia yake

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Sali kwa Yehova akusaidie kuwa mtulivu ili ufikiri kwa makini

  • Fikiria hali zote na uamue jambo linalofaa zaidi unalopaswa kufanya

2 JITUNZE WEWE NA FAMILIA YAKO

BIBLIA INASEMA HIVI: “Moyo wa mtu mwenye uelewaji hujipatia ujuzi, nalo sikio la wenye hekima hutafuta kupata ujuzi.” (Methali 18:15) Uwe na taarifa kamili. Chunguza mahitaji ya kila mshiriki wa familia. Zungumza nao na uwasikilize.​—Methali 20:5.

Vipi ukifiwa na mpendwa wako? Usiogope kuonyesha hisia zako. Kumbuka kwamba hata Yesu ‘alitokwa na machozi.’ (Yohana 11:35; Mhubiri 3:4) Ni muhimu kupumzika na kulala vya kutosha. (Mhubiri 4:6) Kufanya hivyo kutakusaidia kukabiliana na mkazo.

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Uwe na mazoea ya kuwasiliana na familia yako hata kabla majanga hayajatokea. Matatizo yakitokea watajihisi huru kuzungumza nawe

  • Zungumza na watu ambao wamekabili hali kama yako

3 OMBA MSAADA

BIBLIA INASEMA HIVI: “Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote, naye ni ndugu aliyezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.” (Methali 17:17) Rafiki zako wanataka kukusaidia lakini huenda hawajui unachohitaji. Usiogope kuwaambia shida zako. (Methali 12:25) Pia, tafuta msaada kutoka kwa wale walio na ujuzi wa Biblia. Ushauri wa Biblia watakaokupatia utakusaidia.​—Yakobo 5:14.

Utapata msaada unaohitaji ukishirikiana kwa ukawaida na watu wanaomwamini kabisa Mungu na ambao wanatumaini ahadi zake. Pia, utapata faraja unapowasaidia wale wanaohitaji kutiwa moyo. Zungumza nao kumhusu Yehova na ahadi zake. Uwe na mengi ya kufanya katika kusaidia wenye uhitaji, na usijitenge na watu wanaokupenda.​—Methali 18:1; 1 Wakorintho 15:58.

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Zungumza na rafiki wa karibu na ukubali msaada wake

  • Taja mahitaji yako kihususa na kwa unyoofu

JAMBO KUU

Ukihisi umelemewa, kazia fikira uhusiano wako na Mungu. Alipokabili majaribu, Ayubu alisema: “Jina la Yehova na liendelee kubarikiwa.” (Ayubu 1:21, 22) Kama Ayubu, tanguliza jina la Yehova badala ya mahangaiko yako. Mambo yasipoenda ulivyotazamia, usikate tamaa. Mtumaini Mungu kwa moyo wote. “‘Mimi najua vema mawazo ninayofikiria kuwaelekea ninyi,’ asema Yehova, ‘mawazo ya amani, wala si ya msiba, ili kuwapa ninyi wakati ujao na tumaini.’”​—Yeremia 29:11.

JIULIZE . . .

  • Je, ninamtumaini Yehova kwa moyo wote hata katika mambo madogo?

  • Nina sababu gani za kumshukuru Yehova kila siku kwa wema wake?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki