Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • T-36 kur. 1-4
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Habari Zinazolingana
  • Una Maoni Gani Kuhusu Wakati Ujao?
    Una Maoni Gani Kuhusu Wakati Ujao?
  • Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?
    Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?
  • Je, Kweli Wafu Wataishi Tena?
    Je, Kweli Wafu Wataishi Tena?
  • Je, Kuteseka Kutaisha?
    Je, Kuteseka Kutaisha?
Pata Habari Zaidi
Ufalme wa Mungu Ni Nini?
T-36 kur. 1-4
Watu kutoka malezi tofauti wakisali ufalme wa Mungu uje
Watu kutoka malezi tofauti wakisali ufalme wa Mungu uje
Watu kutoka malezi tofauti wakisali ufalme wa Mungu uje

Ufalme wa Mungu ni nini?

Unafikiri ni . . .

  • kitu kilicho moyoni?

  • kitu kisicho halisi au mfano?

  • serikali iliyo mbinguni?

BIBLIA HUSEMA HIVI

“Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe.”—Danieli 2:44, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

“Kuna mwana ambaye tumepewa; na utawala wa ukuu utakuwa juu ya bega lake.”—Isaya 9:6.

FAIDA ZA KUAMINI JAMBO HILO

  • Serikali yenye uadilifu inayoweza kukufaidi kibinafsi.​—Isaya 48:17, 18.

  • Kuishi katika ulimwengu mpya unaokuja, ukiwa na afya kamili na furaha.​—Ufunuo 21:3, 4.

Watu wakitunza bustani na kufurahia maisha katika paradiso  duniani chini ya utawala wa Mungu

JE, KWELI TUNAWEZA KUAMINI KILE AMBACHO BIBLIA HUSEMA?

Ndiyo, kwa sababu mbili:

  • Yesu alionyesha mambo ambayo Ufalme wa Mungu utatimiza. Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasali ili Ufalme wa Mungu uje na mapenzi ya Mungu yatendeke duniani. (Mathayo 6:9, 10) Yesu alionyesha jinsi sala hiyo itakavyojibiwa.

    Alipokuwa duniani, Yesu alilisha wenye njaa, aliponya wagonjwa, na akafufua wafu! (Mathayo 15:29-38; Yohana 11:38-44) Wakati huo, Yesu alionyesha mambo ambayo Ufalme huo utawafanyia raia wake atakapotawala akiwa Mfalme.—Ufunuo 11:15.

  • Hali zilizo ulimwenguni zinaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu utakuja hivi karibuni. Yesu alitabiri kwamba kabla Ufalme wa Mungu haujaleta amani duniani, ulimwengu ungekumbwa na vita, njaa, na matetemeko ya ardhi.—Mathayo 24:3, 7.

    Tunashuhudia mambo hayo leo. Basi, tunaweza kuwa na hakika kwamba hivi karibuni Ufalme wa Mungu utakomesha matatizo hayo yote.

JAMBO LA KUFIKIRIA

Dunia paradiso ikitawaliwa na Ufalme wa Mungu
Dunia paradiso ikitawaliwa na Ufalme wa Mungu
Dunia paradiso ikitawaliwa na Ufalme wa Mungu

Maisha yatakuwaje chini ya Ufalme wa Mungu?

Biblia inajibu swali hilo kwenye ZABURI 37:29 na ISAYA 65:21-23.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki