Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rj seh. ya 5 kur. 12-15
  • Mrudieni “Mchungaji na Mwangalizi wa Nafsi Zenu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mrudieni “Mchungaji na Mwangalizi wa Nafsi Zenu”
  • Mrudie Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • “Nirudieni”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Atakupa Nguvu
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Atakupa Nguvu
    Mwimbieni Yehova
  • Yehova Anakuthamini!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Mrudie Yehova
rj seh. ya 5 kur. 12-15

SEHEMU YA 5

Mrudieni “Mchungaji na Mwangalizi wa Nafsi Zenu”

Je, umekabili mojawapo ya changamoto zilizozungumziwa katika broshua hii? Ikiwa ndivyo, huko peke yako. Watumishi wengi waaminifu wa Mungu katika nyakati za Biblia na leo pia wamekabili changamoto kama hizo. Kama tu Yehova alivyowasaidia kukabiliana na changamoto hizo, ndivyo atakavyokusaidia pia.

Yehova atakutegemeza unapojitahidi kumrudia

UWE na hakika kwamba Yehova atakutegemeza unapojitahidi kumrudia. Atakusaidia kukabiliana na mahangaiko, kuondoa maumivu ya kihisia, na kupata amani ya akili na moyo kwa sababu ya kuwa na dhamiri safi. Kisha unaweza kuchochewa kumtumikia tena Yehova pamoja na waabudu wenzako. Hali yako itafanana na ya baadhi ya Wakristo wa karne ya kwanza, ambao mtume Petro aliwaandikia hivi: “Mlikuwa kama kondoo, wanaopotea njia; lakini sasa mmerudi kwa mchungaji na mwangalizi wa nafsi zenu.”—1 Petro 2:25.

Jambo bora zaidi unaloweza kufanya ni kumrudia Yehova. Kwa nini? Kwa sababu utafanya moyo wa Yehova ushangilie. (Methali 27:11) Kama ujuavyo, matendo yetu yanaweza kumkasirisha Yehova au kumfurahisha. Bila shaka, Yehova hatulazimishi tumpende au tumtumikie. (Kumbukumbu la Torati 30:19, 20) Kuhusiana na hilo, msomi mmoja wa Biblia alisema hivi: “Moyo wa mwanadamu ni kama mlango ambao hauna komeo. Mtu mwingine hawezi kuufungua, lazima mtu mwenyewe aufungue.” Tunachagua kufungua mlango huo kwa kumwabudu Yehova kwa sababu tunampenda sana kutoka moyoni. Tukifanya hivyo, tunampa zawadi yenye thamani kubwa, yaani, utimilifu wetu, na hivyo kuufanya moyo wake ushangilie sana. Kwa kweli, tunapomtolea Yehova ibada anayostahili, tunapata furaha isiyoweza kulinganishwa na kitu kingine chochote.—Matendo 20:35; Ufunuo 4:11.

Dada asiyetenda akikaribishwa tena kwa uchangamfu kutanikoni

Isitoshe, ukirudia ibada ya Kikristo, utatosheleza uhitaji wako wa kiroho. (Mathayo 5:3) Kwa njia gani? Watu wengi ulimwenguni pote hujiuliza hivi: ‘Tulitoka wapi?’ Wana kiu ya kupata majibu ya maswali kuhusu kusudi la maisha. Wanadamu wameumbwa na Yehova wakiwa na uhitaji huo. Alituumba tupate shangwe kwa kumtumikia. Tunapata uradhi mkubwa tunapojua kwamba tunamwabudu Yehova kwa sababu tunampenda.—Zaburi 63:1-5.

Tafadhali usisahau kwamba Yehova anataka umrudie. Unawezaje kuwa na uhakika huo? Fikiria hili: Kwa sala nyingi, broshua hii iliandaliwa kwa makini. Huenda mzee Mkristo au mwamini mwenzako mwingine alikuletea broshua hii. Kisha ukachochewa kuisoma na kukubali ujumbe wake. Hayo yote yanathibitisha kwamba Yehova hajakusahau. Badala yake, anakuvuta kwake kwa wororo.—Yohana 6:44.

Tunaweza kupata faraja kwa kujua kwamba Yehova hawasahau kamwe watumishi wake waliopotea. Dada anayeitwa Donna alikuja kuthamini jambo hilo. Alisema hivi: “Nilipeperuka polepole kutoka katika kweli, hata hivyo mara nyingi nilitafakari andiko la Zaburi 139:23, 24, linalosema: ‘Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu. Unichunguze, na uzijue fikira zangu zinazofadhaisha, Na uone kama ndani yangu mna njia yoyote yenye kuumiza, Na uniongoze katika njia ya mpaka wakati usio na kipimo.’ Nilijua kwamba mimi si sehemu ya ulimwengu, yaani, sikustahili kuwa ulimwenguni, na nilijua kwamba nilipaswa kuwa katika tengenezo la Yehova. Nilianza kutambua kwamba Yehova kamwe hajaniacha; nilichopaswa kufanya ni kumrudia. Ninafurahi sana kwamba nimerudi!”

“Nilianza kutambua kwamba Yehova kamwe hajaniacha; nilichopaswa kufanya ni kumrudia”

Tunasali kwa dhati kwamba wewe pia utafurahia tena “shangwe ya Yehova.” (Nehemia 8:10) Ukimrudia Yehova, hutajuta kamwe.

Majibu ya Maswali Kuhusu Kumrudia Yehova

NIANZIE WAPI?

Dada asiyetenda akisoma Biblia

Huenda mtu aliyekuwa mgonjwa kimwili akahitaji kurudia utendaji wake wa kawaida hatua kwa hatua. Vivyohivyo, unaweza kuimarisha imani yako ukiwa Mkristo kwa kujitahidi kula angalau chakula kidogo cha kiroho kila siku. Usihisi kwamba ni lazima ufanye kila kitu kwa wakati mmoja. Unaweza kutumia dakika chache kusoma au kusikiliza usomaji wa Biblia, kujifunza mojawapo ya machapisho yetu, kuingia kwenye Tovuti ya jw.org, au kutazama programu kwenye televisheni ya tv.jw.org. Pia, jitahidi kuhudhuria mikutano ya kutaniko haraka iwezekanavyo. Zaidi ya hayo, sali kwa Yehova na umwombe akusaidie. ‘Mtupie mahangaiko yako yote, kwa sababu yeye anakujali.’—1 Petro 5:7.

“Nilipoacha kutenda, nilihisi aibu hata kutoa sala. Nilipopata nguvu ya kutoa sala, mzee wa kutaniko letu alinitembelea. Alinisaidia kuthamini kwamba Yehova hajanitupa. Mzee huyo alipendekeza kwamba nianze kusoma Biblia kila siku. Nilipofanya hivyo, nilipata tena nguvu ya kuhudhuria mikutano. Baada ya muda, nilianza tena kuhubiri. Ninafurahi sana kwamba Yehova hakunitupa.”—Eeva.

NDUGU NA DADA WATANIONAJE?

Uwe na hakika kwamba ndugu na dada kutanikoni watakukaribisha kwa uchangamfu. Badala ya kukuchambua au kukuhukumu, watakutendea kwa upendo na kufanya kila wanachoweza ili kukutia moyo.—Waebrania 10:24, 25.

“Nilihisi aibu kurudi kwenye Jumba la Ufalme. Nilikuwa na wasiwasi kuhusu jinsi ambavyo rafiki zangu wangenitendea. Dada yetu mmoja aliyezeeka niliyemwacha kutanikoni miaka 30 iliyopita aliniambia hivi: ‘Karibu nyumbani, Mwanangu!’ Maneno hayo yalinigusa sana moyo. Kwa kweli nilikuwa nimerudi nyumbani.” —Javier.

“Nilienda kwenye Jumba la Ufalme na kuketi viti vya nyuma ili watu wasinitambue. Hata hivyo, wengi walinikumbuka kwa sababu nilihudhuria mikutano nilipokuwa mtoto mdogo. Walinikaribisha na kunikumbatia kwa wororo hivi kwamba nikahisi amani isiyo na kifani. Ni kana kwamba nilikuwa nimerudi nyumbani.”—Marco.

WAZEE WATANISAIDIA JINSI GANI?

Wazee watakutendea kwa fadhili. Watakupongeza kwa sababu unataka kufufua “upendo uliokuwa nao mwanzoni.” (Ufunuo 2:4) Kwa rehema, watakusaidia kurekebisha makosa yoyote uliyofanya, nao watafanya hivyo “katika roho ya upole.” (Wagalatia 6:1; Methali 28:13) Huenda wazee wakapanga ili mtu fulani ajifunze Biblia pamoja nawe, akitumia kitabu kama vile Furahia Maisha Milele! au Mkaribie Yehova. Uwe na hakika kwamba wazee watakufariji na kukutegemeza kwa kila njia.—Isaya 32:1, 2.

“Kwa miaka minane ambayo nilikuwa asiyetenda, wazee waliendelea kunisihi nirudi. Siku moja, mzee mmoja alinionyesha picha alizotupiga. Zilinikumbusha mambo mengi mazuri sana hivi kwamba nikaanza kutamani shangwe niliyokuwa nayo nilipomtumikia Yehova. Kwa upendo, wazee walinisaidia kurudia utendaji wangu wa kiroho.”—Victor.

“Atakupa Nguvu”

Dada wawili wakiimba kwenye Jumba la Ufalme wakitumia kitabu kimoja

Kitabu chetu cha nyimbo, Mwimbieni Yehova, kina nyimbo nyingi ambazo zinaweza kukufariji na kukupa ujasiri unaporudia utendaji wako wa kiroho. Kwa mfano, fikiria maneno ya wimbo namba 60. Wimbo huo wenye kichwa “Atakupa Nguvu,” unategemea maneno ya 1 Petro 5:10.

  1. Kweli yake Mungu amekufundisha,

    Amekuleta katika nuru.

    Aliona moyo wako watamani,

    Kufanya mambo yaliyo mema.

    Kwa sala, ulijiweka wakfu;

    Daima atakuimarisha.

  2. Kamutoa Yesu Mwana wake afe;

    Hivyo ataka ufanikiwe.

    Basi kama Mungu alifanya hivyo,

    Bila shaka atakupa nguvu.

    Imani yako hatasahau;

    Walio wake atawatunza.

    (KORASI)

    Kwa damu ya Mwanaye, alikununua.

    Hukuimarisha, na kukupa nguvu.

    Atakulinda na kukuongoza wewe.

    Hukuimarisha, na kukupa nguvu.

Mwimbie Yehova​—Muziki wa Kuimbwa

Ili kusikiliza muziki wa kuimbwa wa wimbo huu na nyimbo nyingine za Ufalme, angalia kwenye jw.org/sw.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki