Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 11 uku. 32-uku. 33 fu. 2
  • Jaribu la Imani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jaribu la Imani
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Anajaribu Imani ya Ibrahimu
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Uthibitisho Mkubwa Zaidi wa Upendo wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Yehova Alimwita “Rafiki Yangu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Abrahamu Alikuwa Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 11 uku. 32-uku. 33 fu. 2
Abrahamu na Isaka wakielekea Moria

SOMO LA 11

Jaribu la Imani

Abrahamu alimfundisha mwana wake Isaka kumpenda Yehova na kutumaini ahadi zake. Hata hivyo, Isaka alipokuwa na umri wa miaka 25, Yehova alimwambia Abrahamu afanye jambo fulani ambalo lilikuwa gumu sana. Jambo gani?

Mungu alimwambia Abrahamu: ‘Tafadhali, mchukue mwana wako wa pekee na umtoe akiwa dhabihu kwenye mlima katika nchi ya Moria.’ Abrahamu hakujua ni kwa nini Yehova alimwomba afanye jambo hilo. Hata hivyo, alimtii Yehova.

Asubuhi na mapema siku iliyofuata, Abrahamu, Isaka na watumishi wake wawili walianza safari ya kwenda Moria. Baada ya kusafiri kwa siku tatu, waliiona milima kwa mbali. Abrahamu aliwaambia watumishi wake wabaki, ili yeye na Isaka waende wakatoe dhabihu. Abrahamu alichukua kisu naye Isaka alibeba kuni. Isaka alimuuliza baba yake hivi: ‘Mnyama wa dhabihu yuko wapi?’ Abrahamu akamjibu: ‘Mwanangu, Yehova ataandaa.’

Walipofika mlimani walijenga madhabahu. Kisha, Abrahamu akamfunga Isaka mikono na miguu na kumweka juu ya madhabahu.

Isaka akiwa amefungwa juu ya madhabahu na Abrahamu ameshika kisu

Abrahamu akainua kisu. Mara moja, malaika wa Yehova akaita kutoka mbinguni akisema: ‘Abrahamu! Usimchinje mwana wako! Sasa ninajua kwamba una imani katika Mungu kwa sababu ulikuwa tayari kumtoa mwana wako kuwa dhabihu.’ Kisha, Abrahamu akamwona kondoo akiwa amejinasa kwenye kichaka. Bila kukawia alimfungua Isaka na kutoa dhabihu ya kondoo.

Kuanzia siku hiyo, Yehova alimwita Abrahamu kuwa rafiki yake. Je, unajua ni kwa nini? Abrahamu alifanya kila kitu ambacho Yehova alimwagiza, hata ingawa nyakati fulani hakuelewa sababu za kufanya hivyo.

Abrahamu akimfungua kamba Isaka

Yehova alirudia ahadi yake kwa Abrahamu: ‘Nitakubariki nami nitafanya watoto wako wawe wengi.’ Hilo lilimaanisha kwamba Yehova angewabariki watu wote wema kupitia familia ya Abrahamu.

“Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa pekee, ili kila mtu anayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.”​—Yohana 3:16

Maswali: Abrahamu alionyeshaje kwamba alimtumaini Yehova? Yehova alimwahidi Abrahamu nini?

Mwanzo 22:1-18; Waebrania 11:17-19; Yakobo 2:21-23

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki