Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 17 uku. 46-uku. 47 fu. 2
  • Musa Aliamua Kumwabudu Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Musa Aliamua Kumwabudu Yehova
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Kitu Chenye Thamani Zaidi Kuliko Hazina za Misri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Namna Mtoto Musa Alivyookolewa
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Imani ya Wazazi Yathawabishwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Musa—Mtu Halisi au wa Hadithi?
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 17 uku. 46-uku. 47 fu. 2
Binti ya Farao anampata mtoto Musa huku Miriamu akiwatazama kwa karibu

SOMA 17

Musa Aliamua Kumwabudu Yehova

Katika nchi ya Misri, watu wa familia ya Yakobo walikuja kuitwa Waisraeli. Baada ya Yakobo na Yosefu kufa, Farao mwingine alianza kutawala. Aliogopa kwamba Waisraeli wangekuwa wengi na hivyo kuwa na nguvu kuliko Wamisri. Kwa hiyo, Farao huyo aliwafanya Waisraeli kuwa watumwa. Aliwalazimisha kutengeneza matofali na kufanya kazi ngumu kwenye mashamba. Lakini kadiri Wamisri walivyowalazimisha wafanye kazi ngumu, ndivyo walivyozidi kuongezeka. Kwa kuwa Farao hakufurahia jambo hilo, aliagiza wavulana wote Waisraeli wauawe mara tu wanapozaliwa. Je, unaweza kuwazia jinsi Waisraeli walivyoogopa?

Mwanamke Mwisraeli aliyeitwa Yokebedi, alijifungua mtoto wa kiume mwenye sura nzuri. Kwa sababu alitaka kumwokoa, aliamua kumweka ndani ya kikapu, na kumficha kwenye matete yaliyo kandokando ya Mto Nile. Miriamu, dada ya mtoto huyo, alikaa karibu ili aone kitakachotokea.

Binti ya Farao alienda kuoga mtoni na akaona kikapu hicho. Ndani ya kikapu hicho, aliona mtoto akilia, naye akamsikitikia. Miriamu akamwuliza: ‘Ungependa nikutafutie mwanamke atakayemnyonyesha mtoto huyu kwa niaba yako?’ Binti ya Farao alipokubali, Miriamu akamleta Yokebedi, mama yake. Binti ya Farao akamwambia hivi: ‘Mchukue mtoto huyu uninyonyeshee, halafu nitakulipa.’

Musa akikimbia

Mtoto alipokuwa mkubwa, Yokebedi akamleta kwa binti ya Farao, naye akamwita Musa na kumlea kama mtoto wake. Musa alilelewa kama mtoto wa mfalme na angeweza kupata chochote alichotaka. Lakini Musa hakumsahau Yehova. Alijua kwamba yeye alikuwa Mwisraeli, si Mmisri. Na aliamua kumtumikia Yehova.

Alipokuwa na umri wa miaka 40, Musa aliamua kuwasaidia Waisraeli wenzake. Alipomwona Mmisri akimpiga mtumwa Mwisraeli, Musa alimpiga kwa nguvu Mmisri huyo na kumuua. Halafu akamficha ndani ya mchanga. Farao alipogundua jambo hilo, alijaribu kumuua Musa. Lakini Musa akakimbilia nchi ya Midiani. Yehova alimtunza alipokuwa huko.

“Kwa imani, Musa . . alikataa kuitwa mwana wa binti ya Farao, akachagua kuteswa pamoja na watu wa Mungu.”​—Waebrania 11:24, 25

Maswali: Waisraeli walitendewaje walipokuwa Misri? Kwa nini Musa alikimbia kutoka Misri?

Mwanzo 49:33; Kutoka 1:1-14, 22; 2:1-15; Matendo 7:17-29; Waebrania 11:23-27

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki